mwanakijiji
12-12-2009, 12:37 AM
Na Joseph Shaluwa (Ijumaa)
Siku chache baada ya Miss Tanzania 2006, Wema Isaack Sepetu kutangaza hadharani kwamba ana ujauzito, wadau mbalimbali wameibuka na maswali kibao na Ijumaa ndilo gazeti pekee linaloweza kukupa kila kitu kuhusu ishu nzima.
Vingi viulizo kutoka kwa wadau hao, vinamwendea Wema ambaye anang?ara pia kwenye kiwanda cha filamu nchini, wakihoji namna ambavyo amenasa ujauzito huo na jinsi anavyojitangaza.
?Ujauzito ni jambo la kheri, ni ukuaji wa hatua, kutoka u-dada kwenda u-mama, lakini kwanini ujitangaze kiivyo? Hili ni jambo la watu wawili tu,? alisema mdau mmoja.
Kigogo mmoja mwenye mchango mkubwa katika tasnia ya filamu, amesema kwamba anachokiona yeye kwa Wema ni kutapatapa, kwani kabla ya kutua kwa Chalz Baba alishakuwa na msululu wa wanaume kabla.
?Inawezekana kabisa anafanya hivi kwa nia ya kumuumiza Kanumba, maana ni hivi karibuni tu ametangaza kutafuta binti wa kuzaa naye, lakini kitu kinachoniumiza kichwa, kwanini hakuzaa na wanaume wote waliotangulia hadi akaamua kuzaa na Chalz Baba?? Alihoji Kigogo huyo ambaye aliomba sana hifadhi ya jina lake.
Prodyuza maarufu wa sinema ambaye filamu zake zinatenda vyema kunako soko, ameliambia Ijumaa kwamba, Wema alifanya haraka sana kubeba mimba ya Chalz kwani wamekuwa katika uhusiano kwa kipindi kifupi sana.
?Walitakiwa kuchunguza kwanza, hawezi kumbebea mimba mapema kiasi hiki, jamaa akimbadilikia itakuwaje? Lakini simuombei mabaya ingawa ni kweli kwamba amewahi sana,? alisema mtayarishaji sinema huyo.
Si Wema wala Chalz Baba waliopatikana kuzungumzia ishu hiyo kwani muda wote simu ya Wema ilipopigwa iliita bila kupokelewa, wakati Chalz Baba hakupatikana kabisa.
Hivi karibuni Wema alitangaza kuwa mjamzito na alieleza wazi kuwa mwenye ?mzigo? huo ni Chalz Baba ambaye naye kupitia vyombo vya habari amekiri kwamba, anajisikia vizuri sana kuwa baba watoto wa Wema.
Swali:
Yaani huyu binti hawezi kuwa na uhusiano mwingine au kufanya kitu kingine isipokuwa lazima jina la Kanumba lihusishwe?
Siku chache baada ya Miss Tanzania 2006, Wema Isaack Sepetu kutangaza hadharani kwamba ana ujauzito, wadau mbalimbali wameibuka na maswali kibao na Ijumaa ndilo gazeti pekee linaloweza kukupa kila kitu kuhusu ishu nzima.
Vingi viulizo kutoka kwa wadau hao, vinamwendea Wema ambaye anang?ara pia kwenye kiwanda cha filamu nchini, wakihoji namna ambavyo amenasa ujauzito huo na jinsi anavyojitangaza.
?Ujauzito ni jambo la kheri, ni ukuaji wa hatua, kutoka u-dada kwenda u-mama, lakini kwanini ujitangaze kiivyo? Hili ni jambo la watu wawili tu,? alisema mdau mmoja.
Kigogo mmoja mwenye mchango mkubwa katika tasnia ya filamu, amesema kwamba anachokiona yeye kwa Wema ni kutapatapa, kwani kabla ya kutua kwa Chalz Baba alishakuwa na msululu wa wanaume kabla.
?Inawezekana kabisa anafanya hivi kwa nia ya kumuumiza Kanumba, maana ni hivi karibuni tu ametangaza kutafuta binti wa kuzaa naye, lakini kitu kinachoniumiza kichwa, kwanini hakuzaa na wanaume wote waliotangulia hadi akaamua kuzaa na Chalz Baba?? Alihoji Kigogo huyo ambaye aliomba sana hifadhi ya jina lake.
Prodyuza maarufu wa sinema ambaye filamu zake zinatenda vyema kunako soko, ameliambia Ijumaa kwamba, Wema alifanya haraka sana kubeba mimba ya Chalz kwani wamekuwa katika uhusiano kwa kipindi kifupi sana.
?Walitakiwa kuchunguza kwanza, hawezi kumbebea mimba mapema kiasi hiki, jamaa akimbadilikia itakuwaje? Lakini simuombei mabaya ingawa ni kweli kwamba amewahi sana,? alisema mtayarishaji sinema huyo.
Si Wema wala Chalz Baba waliopatikana kuzungumzia ishu hiyo kwani muda wote simu ya Wema ilipopigwa iliita bila kupokelewa, wakati Chalz Baba hakupatikana kabisa.
Hivi karibuni Wema alitangaza kuwa mjamzito na alieleza wazi kuwa mwenye ?mzigo? huo ni Chalz Baba ambaye naye kupitia vyombo vya habari amekiri kwamba, anajisikia vizuri sana kuwa baba watoto wa Wema.
Swali:
Yaani huyu binti hawezi kuwa na uhusiano mwingine au kufanya kitu kingine isipokuwa lazima jina la Kanumba lihusishwe?