mwanakijiji
11-20-2008, 12:03 AM
Kuna hii habari ambayo kama kungekuwa hakuna picha ningeweza kuamini lakini hizi picha zinazua maswali mengi zaidi kuhusu habari yenyewe:
Habari yenyewe:
Na Elvan Stambuli
Mama mmoja aitwae Anjelina Renatus (27), amejinyonga kwa kutumia kanga porini na kuacha mtoto wake mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu akilia chini ya mti aliojinyongea.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo la kusikitisha lilitokea hivi karibuni katika Kijiji cha Igagala, Mkoani Tabora.
Akisimulia mkasa huo mume wa marehemu Saidi Matoboke alisema siku hiyo mtoto wao mdogo aliyemtaja kwa jina la Hangwa alikuwa mgonjwa na waliamua kumpeleka katika Hospitali ya Misheni ya Karima ili akatibiwe.
Alisema wakati wanarudi wakiwa katikati ya pori usiku mkewe alimuomba aende akajisaidie na alipomruhusu, hakumuona tena.
Aliongeza kuwa baada ya kumsubiri kwa muda mrefu aliamua kumtafuta katika pori hilo huku akimuita jina bila mafanikio.
Aliamua kurudi nyumbani kwake katika Kitongoji cha Ugasa na asubuhi yake alitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji na ikaamuliwa kazi ya kumtafuta ianze mara moja.
?Mama huyo alipatikana majira ya saa 11 jioni akiwa ananing?inia juu ya mti na mtoto wake akiwa chini akilia, ni wawindaji ndiyo waliomgundua,? alisema Bw. Matoboke.
Aliendelea kusema kuwa wawindaji hao wakati wakiwinda walisikia sauti ya mtoto akilia, mara ya kwanza walidhani ni mnyama na walipofuatilia sauti ilikokuwa ikitokea walimkuta mtoto akiwa chini huku mwili wa mama yake ukining?inia ukiwa uchi wa mnyama.
Habari zinasema viongozi wa Kijiji cha Igagala walitoa taarifa polisi ambao walifika siku ya pili yake ambapo maiti ilichunguzwa na daktari kisha kuamuliwa kuzikwa.
Aidha, mtoto aliyeachwa na marehemu alichukuliwa na msamaria mwema, Bi. Mwajuma Yahya Kahungu ambaye alimpa maziwa.
Hata hivyo sababu ya kujinyonga haijaelezwa licha ya mumewe Bw. Matoboke kudai kuwa amelogwa kwani wakati akiwa kwao Shinyanga aliwahi kufanya jaribio la kutaka kujinyonga.
Katika kuonesha kuwa imani ya kishirikina imewakolea watu wa maeneo hayo, mti aliojinyongea mizizi yake imechimbuliwa kwa madai itatumika kwa dawa ambazo hazikutajwa ni za kutibu nini.
Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bw. Jumanne Gwitagwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na akafafanua kuwa miti wanayojinyongea watu hutumika kwa dawa ya magonjwa mbalimbali ambayo hakuyataja.
Picha:
http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/1226990096_kajinyonga.jpg
http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/thumbs/1226990096_mtoto.jpg
http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/1226990374_kujinyongamamawamtoto.jpg
Kwa kusoma habari hiyo maswali gani unakumbana nayo ambayo yanaweza kukufanya na wewe usiamini maelezo ya Mume? Wiki hii hapa Michigan ni mwaka mmoja tangu jamaa mmoja atokee mbele ya vyombo vya habari akidai mke wake kakimbia na anamtafuta huku akitoa wito arudi. Jamaa huyo alidai kuwa walikorofishana kidogo na mke wake na alikuwa anamhisi kuwa ana cheat anapokuwa safari. Basi watu wakaanza kumtafuta huyo mama... to make the story short Jamaa amehukumiwa kifungo cha maisha kwa kumuua mkewe na kumkatakata vipande vipande mbele ya watoto wao!
Habari yenyewe:
Na Elvan Stambuli
Mama mmoja aitwae Anjelina Renatus (27), amejinyonga kwa kutumia kanga porini na kuacha mtoto wake mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu akilia chini ya mti aliojinyongea.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo la kusikitisha lilitokea hivi karibuni katika Kijiji cha Igagala, Mkoani Tabora.
Akisimulia mkasa huo mume wa marehemu Saidi Matoboke alisema siku hiyo mtoto wao mdogo aliyemtaja kwa jina la Hangwa alikuwa mgonjwa na waliamua kumpeleka katika Hospitali ya Misheni ya Karima ili akatibiwe.
Alisema wakati wanarudi wakiwa katikati ya pori usiku mkewe alimuomba aende akajisaidie na alipomruhusu, hakumuona tena.
Aliongeza kuwa baada ya kumsubiri kwa muda mrefu aliamua kumtafuta katika pori hilo huku akimuita jina bila mafanikio.
Aliamua kurudi nyumbani kwake katika Kitongoji cha Ugasa na asubuhi yake alitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji na ikaamuliwa kazi ya kumtafuta ianze mara moja.
?Mama huyo alipatikana majira ya saa 11 jioni akiwa ananing?inia juu ya mti na mtoto wake akiwa chini akilia, ni wawindaji ndiyo waliomgundua,? alisema Bw. Matoboke.
Aliendelea kusema kuwa wawindaji hao wakati wakiwinda walisikia sauti ya mtoto akilia, mara ya kwanza walidhani ni mnyama na walipofuatilia sauti ilikokuwa ikitokea walimkuta mtoto akiwa chini huku mwili wa mama yake ukining?inia ukiwa uchi wa mnyama.
Habari zinasema viongozi wa Kijiji cha Igagala walitoa taarifa polisi ambao walifika siku ya pili yake ambapo maiti ilichunguzwa na daktari kisha kuamuliwa kuzikwa.
Aidha, mtoto aliyeachwa na marehemu alichukuliwa na msamaria mwema, Bi. Mwajuma Yahya Kahungu ambaye alimpa maziwa.
Hata hivyo sababu ya kujinyonga haijaelezwa licha ya mumewe Bw. Matoboke kudai kuwa amelogwa kwani wakati akiwa kwao Shinyanga aliwahi kufanya jaribio la kutaka kujinyonga.
Katika kuonesha kuwa imani ya kishirikina imewakolea watu wa maeneo hayo, mti aliojinyongea mizizi yake imechimbuliwa kwa madai itatumika kwa dawa ambazo hazikutajwa ni za kutibu nini.
Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bw. Jumanne Gwitagwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na akafafanua kuwa miti wanayojinyongea watu hutumika kwa dawa ya magonjwa mbalimbali ambayo hakuyataja.
Picha:
http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/1226990096_kajinyonga.jpg
http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/thumbs/1226990096_mtoto.jpg
http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/1226990374_kujinyongamamawamtoto.jpg
Kwa kusoma habari hiyo maswali gani unakumbana nayo ambayo yanaweza kukufanya na wewe usiamini maelezo ya Mume? Wiki hii hapa Michigan ni mwaka mmoja tangu jamaa mmoja atokee mbele ya vyombo vya habari akidai mke wake kakimbia na anamtafuta huku akitoa wito arudi. Jamaa huyo alidai kuwa walikorofishana kidogo na mke wake na alikuwa anamhisi kuwa ana cheat anapokuwa safari. Basi watu wakaanza kumtafuta huyo mama... to make the story short Jamaa amehukumiwa kifungo cha maisha kwa kumuua mkewe na kumkatakata vipande vipande mbele ya watoto wao!