mwanakijiji
11-21-2008, 05:05 PM
Na Saida Said, Buguruni (Dar Leo)
KIJANA David Chacha (28), mkazi wa Tabata Shule amefikishwa Mahakamani kujibu mashitaka ya shambulio la aibu kwa kumshika matiti mwanamke bila ridhaa yake.
Mshitakiwa huyo anayekabiliwa na mashitaka mengine ya shambulio mbele ya Hakimu Mussa Abdallah wa Mahakama ya Mwanzo Buguruni.
Katika mashitaka ya kwanza, imedaiwa kuwa Novemba 2, mwaka huu, saa 2 usiku, Tabata kwenye baa ya Swiss Pub, mshitakiwa David alimpiga mlalamikaji Lovenes na kumkaba shingo.
Katika mashitaka mengine imedaiwa kuwa Novemba 2, mwaka huu, mshitakiwa David alimshika matiti mlalamikaji Lovenes bila ridhaa yake.
Mshitakiwa amekana mashitaka hayo na kesi itatajwa tena Desemba 11, mwaka huu.
Katika kesi nyingine,Yusuf Abdallah (24), mkazi wa Tabata Kimanga amefikishwa Mahakamani hapo akikabiliwa na mashitaka ya kujeruhi.
Imedaiwa mbele ya Hakimu Hamisi Masiku kuwa Novemba 8, mwaka huu, saa 5 asubuhi,Tabata Kimanga, mshitakiwa Yusuf alimjeruhi mlalamikaji Issa Bakari kwa kumkata na wembe chini ya jicho.
Mshitakiwa amekana mashitaka na kesi itatajwa tena Novemba 24, mwaka huu.
My Take:
Hivi hizi tabia za kutomasa matiti ya mtu siyo mke wako/mpenzi wako bila ya ridhaa yake bado zipo? Hivi mtu anafikiria kwa kufanya hivyo ndiyo inakuwaje? GRRRRRRRR
KIJANA David Chacha (28), mkazi wa Tabata Shule amefikishwa Mahakamani kujibu mashitaka ya shambulio la aibu kwa kumshika matiti mwanamke bila ridhaa yake.
Mshitakiwa huyo anayekabiliwa na mashitaka mengine ya shambulio mbele ya Hakimu Mussa Abdallah wa Mahakama ya Mwanzo Buguruni.
Katika mashitaka ya kwanza, imedaiwa kuwa Novemba 2, mwaka huu, saa 2 usiku, Tabata kwenye baa ya Swiss Pub, mshitakiwa David alimpiga mlalamikaji Lovenes na kumkaba shingo.
Katika mashitaka mengine imedaiwa kuwa Novemba 2, mwaka huu, mshitakiwa David alimshika matiti mlalamikaji Lovenes bila ridhaa yake.
Mshitakiwa amekana mashitaka hayo na kesi itatajwa tena Desemba 11, mwaka huu.
Katika kesi nyingine,Yusuf Abdallah (24), mkazi wa Tabata Kimanga amefikishwa Mahakamani hapo akikabiliwa na mashitaka ya kujeruhi.
Imedaiwa mbele ya Hakimu Hamisi Masiku kuwa Novemba 8, mwaka huu, saa 5 asubuhi,Tabata Kimanga, mshitakiwa Yusuf alimjeruhi mlalamikaji Issa Bakari kwa kumkata na wembe chini ya jicho.
Mshitakiwa amekana mashitaka na kesi itatajwa tena Novemba 24, mwaka huu.
My Take:
Hivi hizi tabia za kutomasa matiti ya mtu siyo mke wako/mpenzi wako bila ya ridhaa yake bado zipo? Hivi mtu anafikiria kwa kufanya hivyo ndiyo inakuwaje? GRRRRRRRR