PDA

View Full Version : Kizimbani - Ilivyokuwa katika picha



mwanakijiji
11-26-2008, 02:02 AM
Waheshimiwa watuhumiwa walipofikishwa mahakamanni katika zama za Utandawazi!!

Picha kwa hisani kubwa ya Global Publishers

Habari zilivuja mapema kwenye saa 12 za Asubuhi; wajanja wakawahi kusubiri..

http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/1227606390_askari.gif

Muda ulipofika Mramba na Yona wakaanza kuja taratibu kwa upole tu (nchi nyingine huwa wanatiwa pingu!)

http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/1227606390_mrambaa.gif

Watu wengine walishindwa kujizuia; walichelewa maofisini wengine waliahirisha kwenda maofisi kabisa ili wasikose kuwa mashuhuda, na wengine hapo ndiyo ilikuwa kazini!

http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/thumbs/1227613223_mramba_4.jpg

Katika mazingira ya aina hiyo unakuwa na ka "ucelebrity" wa aina fulani; hivyo lazima usalimie "ndugu, jamaa, na marafiki" kuihakikishia jamii kuwa fisadi hawezi kuwa mtu mcheshi na mkarimu.

http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/thumbs/1227613223_mramba_3.jpg

Mahakamani wakati mwingine mwanga ni hafifu na unaweza usimuone Jaji vizuri, so lazima usafishe "macho yako manne".

mwanakijiji
11-26-2008, 06:00 AM
Polisi wa kawaida tulikuwa tunawaita "ndata" au "njagu" n.k Hivi hawa wa Magereza wanaitwaje?

http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/other/yona.jpg

Kuna tofauti gani kati ya kuomba kura na kuelekea kusiko na kula?

http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/other/yona1.jpg

Unajua Mramba kumbe ni mfupi kweli, yawezekana ndiyo sababu kujitutumua?

http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/other/yona2.jpg

mwanakijiji
11-26-2008, 06:38 PM
Of course we had to find some comedy out of this..

http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/gallery/basil%20yona_phixr.jpg

Ach-F
11-26-2008, 11:02 PM
Marsha lazima ajiuzulu au afukuzwe mara moja hii ni aibu kwa serikali ya CCM na Jakaya Kikwete.

Kepa
11-27-2008, 12:23 AM
Marsha lazima ajiuzulu au afukuzwe mara moja hii ni aibu kwa serikali ya CCM na Jakaya Kikwete.

Halafu akishafukuzwa au kujiuzulu ndo iwe basi tena...... au vile kama Daudi???

Ach-F
11-27-2008, 12:29 AM
Siku zote sijui alikuwa wapi tena anacheka cheka tu kama vile hili ni jambo la mzaha wakati pesa ya walipa kodi inateketea.

Kepa
11-28-2008, 11:16 AM
Siku zote sijui alikuwa wapi tena anacheka cheka tu kama vile hili ni jambo la mzaha wakati pesa ya walipa kodi inateketea.

Hicho ndo kinachonitia hasira, Its like 'Hamniwezi' wakati ametulostisha.

dRU
12-03-2008, 03:36 PM
Marsha lazima ajiuzulu au afukuzwe mara moja hii ni aibu kwa serikali ya CCM na Jakaya Kikwete.

Hivi kale ka tume ka kuchunguza tabia za viongozi kaliishia wapi? Labda kangesaidia tukapata watu makini yumkini kwa kuwa tu kiongozi na si mpaka kuwa waziri!!! JK anahitaji kufufua vijitume hivi ama lah atakuwa akiingia mkenge kwa kuchagua Chui waliyovaa ngozi ya Kondoo!!!
Hakika kwa kipindi hiki kifupi cha mabadiliko ya kisiasa Tanzania tumeona mengi na tutaona mengi ya ajabu na kusikitisha kama mwendo ndiyo huu!!!

Mungu tunusuru kwa hili janga na jingine lolote ambalo lipo mbele yetu ila macho yetu yamekuwa mafupi kuyaona!!!

:confused::(