mwanakijiji
11-26-2008, 08:27 AM
Sura ya I
?Vivian Tembo, unampokea Charles Mugisha kuwa mume wako wa ndoa, umuenzi na kumtunza, kumpenda na kumlinda katika shida na raha, katika magonjwa na afya mpaka kifo kiwatenganishe?? Padre Amedeus Minja alimuuliza bibi harusi.
?Ndio nampokea!? Vivian alijibu kwa sauti ya upole, lakini iliyonaswa vilivyo na vipasa sauti vya Kanisa la Mtakatifu Joseph Jijini Dar-es-Saalam. Jibu lake hilo lilisababisha mlipuko wa vigelege, hoi hoi, na makofi ambao nusura uziangushe kuta za Kanisa hilo maarufu. Kabla ya chereko chereko hizo kukoma kwaya ya Mtakatifu Joseph iliyokuwa ikiongozwa na Veronica Mwangwi ilirukia na kuanza kuimba kibwagizo chao maarufu cha ?Nimekuchagua wewe, kati ya wanaume wote, uwe msaidizi wangu!? Mara kibwagizo hicho kilipoisha, Padre Minja alimgeukia kijana Mugisha na kumrushia swali hilo hilo.
?Charles Mugisha, unampokea Vivian Tembo kuwa mke wako wa ndoa, umuenzi na kumtunza, kumpenda na kumlinda, katika shida na raha, katika magonjwa na afya mpaka kifo kiwatenganishe? Aliuliza huku akielekeza kinasa sauti upande wa Charles.
Charles alijaribu kufungua mdomo wake na kutoa jibu la ?ndio nampokea?; mdomo haukufunguka. Alijihisi kupatwa na kizungu zungu cha ghafla huku miguu ikimtetemeka kama mianzi ikipigwa na upepo. Alijaribu tena kutamka maneno hayo ya kukubali lakini ulimi wake uligandamana na kaakaa la kinywa chake kama umetiwa gundi ya mbao. Koo lilimkauka na moyo wake ulianza kumwenda mbio huku mdundo wake ukisikika kwa mbali kwenye vipasa sauti vya kanisa hilo. Ukimya mkubwa ulitanda kama ukimya wa kaburi. Hakupiga mtu chafya, wala kujaribu kupigwa mwayo. Wazazi wa bibi harusi, wanawali waliofuatana na bibi harusi wote walikodoa macho kumwelekea Charles, na macho yakawatoka utadhani gololi! Kila mtu alijiuliza ni kitu gani kimemsibu kijana huyo.
Kanisa lilikuwa kimya wakati Charles anatafuta maneno ya kujibu. Padre Minja akaona ajaribu tena kumuuliza kijana huyo aliyevalia suti ya kupendeza ya rangi nyeusi ambayo koti lake lilikuwa na michirizi ya kumetameta ya rangi ya maziwa na kingo zake zikifika hadi magotini. Upande wa kushoto alikuwa amening?iniza ua jekundu la waridi, na miguuni akiwa ametinga viatu vya Armani ambavyo alizawadiwa na rafiki yake toka Italia.
?Charles Mugisha, unampokea Vivian Tembo kuwa mke wako wa ndoa, umuenzi na kumtunza, kumpenda na kumlinda, katika shida na raha, katika magonjwa na afya mpaka kifo kiwatenganishe?? Alirudia tena Padre Minja.
Ndani ya moyo wake na akili zake Charles alikuwa kama birika la chai ambalo lilikuwa likichemsha maji yakachemka na yakiwa tayari kumwagika kutokana na nguvu za msukumo wa joto lake. Alikuwa karibu kupasuka kwa msukumo wa hofu, woga, aibu, hatia, na kila aina ya hisia hasi. Alijaribu kukohoa kidogo kusafisha koo lake. Alimwangalia bibi harusi ambaye wakati huo mdomo wake ulikuwa umebakia wazi kiasi cha kuwa kama mlango unaokaribisha inzi! Charles alimuangalia Vivian na akajaribu tena kutoa kauli ya kukubali. Haikutoka. Alikuwa kama gari lililozima katikati ya reli huku treni likija kwa kasi toka upande mmoja na jitihada zote za kuliwasha zikishindikana.
Vivian aliinua macho yake na kuyagonganisha na ya mchumba wake, mawazoni alikuwa na maswali milioni moja na moja ambayo angependa kumuuliza kimemsibu kitu gani. Alipomuangalia vizuri aligundua kuwa Charles alikuwa amelengwa na machozi na yeye mwenyewe Vivian alijigundua kuwa machozi yameanza kufurika kwenye macho yake na kuanza kufanya michirizi kwenye pande za mashavu yake huku yakiharibu poda, wanja, na vimetameta alivyokuwa amepambwa navyo kwa ajili ya harusi hiyo. Wapenzi hao wawili walijikuta wakibubujikwa na machozi.
Charles alimgeukia Padre Minja na kumwashiria amsogelee ili amnong?oneze kitu.
?Baba Padre, naweza kujibu swali hilo, lakini kabla sijafanya hivyo naomba nafasi ya kuungama kitu kwako na kwa Vivian, tafadhali? Alisema kwa sauti ya upole, ya chini lakini iliyokuwa na uhakika wa kile isemacho. Padre Minja alitingisha kichwa kuashiria amemuelewa. Vivian hakujua Charles amemnong?oneza kitu gani padre huyo, maswali akilini mwake yaliongezeka na kuwa milioni moja na mbili. Padre Minja aliwageukia waumini ambao wote walikuwa kimya wakisubiri kwa hamu kujua ni nini kinaendelea. Waliokuwa wambeya hawakuchelewa kuanza kuzusha uvumi, na wenye simu wakaanza kutumiana ujumbe kuwa Vivian kaachwa altareni!
?Wapendwa katika Bwana!? Padre Minja alianza kuzungumza kwa sauti kakamavu iliyomgutusha kila mtu kanisani humo. ?Tumesikia jibu la bibi harusi, lakini bwana harusi kabla ya kutoa jibu lake, ameniomba twende chemba ili afanya maungamo ya dhati kabla kutoa jibu hilo. Hivyo kwaya itaendelea kuburudisha wakati mimi, bwana harusi na bibi harusi tutakuwa sakristia na pindi tukimaliza tutarudi. Asanteni? Alimaliza huku akiwaongozwa wachumba hao kuelekea kwenye sakristia pembezoni mwa kanisa hilo.
Padre Minja alivuta viti vitatu vilivyokuwa vimekunjwa pembeni ya meza ya na kuviweka katikati ya chumba hicho ambacho mapadre hutumia kubadilishia mavazi na vitu vyenye wakfu huhifadhiwa. Kwaya ya Mtakatifu Joseph iliendelea kuongoza kwa nyimbo mbalimbali kama ile ya ?Nakupenda Maria?, ?Jina Maria? na ?Enendeni Duniani Kote?. Wakati nyimbo hizo zikiendelea kuimbwa, Padre Minja na Vivian walikaa kitako ili kusikiliza maungamo ya Charles Mugisha; maungamo ambayo yalichelewesha ufungaji wa ndoa ya njiwa hao wawili wapendanao. Baada ya sekunde chache kupita na baada ya kuvuta pumzi ndefu, Charles alianza kusimulia ni kitu gani kilimfanya asitishe mwitikio wake wa ndoa. Padre Minja na Vivian kama wanafunzi watulivu darasani, walisikiliza kwa makini.
* * *
Hadi mwaka 1990 nikiwa na miaka 25 nilikuwa bado mimi bikira. Nilikuwa sijawahi kulala na mwanamke zaidi ya kuishia kuwatamani tu kwa nje. Bila ya shaka utajiuliza ilikuwaje nichelewe kiasi hicho kuanza mapenzi. Ukweli wa mambo ni kuwa mimi nilikuwa ni mseminari wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza na mwaka huo ulikuwa ni mwaka wangu wa mwisho kabla sijapandishwa kwenye madaraja ya altare, yaani ushemasi na baadaye Upadre. Moyoni mwangu niliamini kabisa kuwa mimi nilikuwa na wito wa upadre na tangu utoto nilijiandaa kutimiza ndoto hiyo.
Ni kwa sababu hiyo basi niliwakwepa kinadada kama wana ukoma, na kila nikimuona dada mwenye kuvutia nilijikuta nikisali sala ya baba yetu nikirudia rudia maneno ya ?usitutie majaribuni? mara nyingi. Niliweza kutawala tamaa zangu hasa kwa kupenda kujisomea vitabu mbalimbali vya kitaaluma, kuandika, na kufanya kazi nyingi za mikono. Muda wangu mwingi wa ziada nilikuwa natembelea wagonjwa, kushiriki katika kwaya, na kufundisha tuition vijana wa sekondari hasa masomo ya Fizikia na Kemia. Niliyapenda maisha yangu na sikuwa na shaka kabisa kuwa nitakuwa padre mzuri, mcha Mungu, na mtumishi wa watu.
Ndoto yangu hiyo ilipeperuka siku ile isiyo na jina, miezi mitatu kamili kabila sijavikwa ushemasi kwenye ibada ya Misa Takatifu kwenye viwanja vya jangwani ambayo ilikuwa iongozwe na Baba Mtakatifu Yohanne Paulo II akiwa katika ziara yake ya Kichungaji. Nilikuwa katika mapumziko ya mwisho toka seminari ya Kipalapala, siku ile ambapo mambo yote yaliniharibikia na mwelekeo wa maisha yangu kubadilishwa. Wakati wa mapumziko hayo ya karibu miezi miwili nilikuwa nimefikia parokia ya Pugu ambako nilikuwa nasaidia shughuli mbalimbali pale parokiani. Licha ya kusaidia parokia ya Pugu mara nyingi mida ya mchana nilikuwa nakuja St. Joseph kwa kusaidia kazi mbalimbali za ofisini na kupata uzoefu wa kikazi. Nilikuwa ni mwanafunzi wa Padre Peter Mhonda aliyekuwa msaidizi wa Askofu wa Dar. Niliona fahari kila nikija hapa na kushirikia katika misa, huduma mbalimbali na shughuli mbalimbali.
Siku hiyo hata hivyo nilikuwa nimemaliza shughuli zangu mapema St. Joseph na Sr. Maria Goretti alinichukua kwa gari hadi eneo la Tazara ambako nilikuwa kwa kawaida nasubiri mabasi ya kwenda Pugu. Ilikuwa jioni kwenye majira ya saa kumi na mbili hivi wakati jua limeanza kutua ingawa joto la Dar bado liliendelea nilikuwa nimekaa chini ya Kibanda cha kusubiria mabasi kilichoko nje ya jengo la Tazara ikiangalia upande wa Buguruni. Nilikuwa nimevalia nguo za kawaida tu zilizonifanya nionekane kama mfanyakazi wa kampuni fulani na mkononi nilikuwa nimeshika gazeti la Alasiri ambalo ndio lilikuwa limetinga mitaani mida hiyo.
(Itaendelea kesho)
?Vivian Tembo, unampokea Charles Mugisha kuwa mume wako wa ndoa, umuenzi na kumtunza, kumpenda na kumlinda katika shida na raha, katika magonjwa na afya mpaka kifo kiwatenganishe?? Padre Amedeus Minja alimuuliza bibi harusi.
?Ndio nampokea!? Vivian alijibu kwa sauti ya upole, lakini iliyonaswa vilivyo na vipasa sauti vya Kanisa la Mtakatifu Joseph Jijini Dar-es-Saalam. Jibu lake hilo lilisababisha mlipuko wa vigelege, hoi hoi, na makofi ambao nusura uziangushe kuta za Kanisa hilo maarufu. Kabla ya chereko chereko hizo kukoma kwaya ya Mtakatifu Joseph iliyokuwa ikiongozwa na Veronica Mwangwi ilirukia na kuanza kuimba kibwagizo chao maarufu cha ?Nimekuchagua wewe, kati ya wanaume wote, uwe msaidizi wangu!? Mara kibwagizo hicho kilipoisha, Padre Minja alimgeukia kijana Mugisha na kumrushia swali hilo hilo.
?Charles Mugisha, unampokea Vivian Tembo kuwa mke wako wa ndoa, umuenzi na kumtunza, kumpenda na kumlinda, katika shida na raha, katika magonjwa na afya mpaka kifo kiwatenganishe? Aliuliza huku akielekeza kinasa sauti upande wa Charles.
Charles alijaribu kufungua mdomo wake na kutoa jibu la ?ndio nampokea?; mdomo haukufunguka. Alijihisi kupatwa na kizungu zungu cha ghafla huku miguu ikimtetemeka kama mianzi ikipigwa na upepo. Alijaribu tena kutamka maneno hayo ya kukubali lakini ulimi wake uligandamana na kaakaa la kinywa chake kama umetiwa gundi ya mbao. Koo lilimkauka na moyo wake ulianza kumwenda mbio huku mdundo wake ukisikika kwa mbali kwenye vipasa sauti vya kanisa hilo. Ukimya mkubwa ulitanda kama ukimya wa kaburi. Hakupiga mtu chafya, wala kujaribu kupigwa mwayo. Wazazi wa bibi harusi, wanawali waliofuatana na bibi harusi wote walikodoa macho kumwelekea Charles, na macho yakawatoka utadhani gololi! Kila mtu alijiuliza ni kitu gani kimemsibu kijana huyo.
Kanisa lilikuwa kimya wakati Charles anatafuta maneno ya kujibu. Padre Minja akaona ajaribu tena kumuuliza kijana huyo aliyevalia suti ya kupendeza ya rangi nyeusi ambayo koti lake lilikuwa na michirizi ya kumetameta ya rangi ya maziwa na kingo zake zikifika hadi magotini. Upande wa kushoto alikuwa amening?iniza ua jekundu la waridi, na miguuni akiwa ametinga viatu vya Armani ambavyo alizawadiwa na rafiki yake toka Italia.
?Charles Mugisha, unampokea Vivian Tembo kuwa mke wako wa ndoa, umuenzi na kumtunza, kumpenda na kumlinda, katika shida na raha, katika magonjwa na afya mpaka kifo kiwatenganishe?? Alirudia tena Padre Minja.
Ndani ya moyo wake na akili zake Charles alikuwa kama birika la chai ambalo lilikuwa likichemsha maji yakachemka na yakiwa tayari kumwagika kutokana na nguvu za msukumo wa joto lake. Alikuwa karibu kupasuka kwa msukumo wa hofu, woga, aibu, hatia, na kila aina ya hisia hasi. Alijaribu kukohoa kidogo kusafisha koo lake. Alimwangalia bibi harusi ambaye wakati huo mdomo wake ulikuwa umebakia wazi kiasi cha kuwa kama mlango unaokaribisha inzi! Charles alimuangalia Vivian na akajaribu tena kutoa kauli ya kukubali. Haikutoka. Alikuwa kama gari lililozima katikati ya reli huku treni likija kwa kasi toka upande mmoja na jitihada zote za kuliwasha zikishindikana.
Vivian aliinua macho yake na kuyagonganisha na ya mchumba wake, mawazoni alikuwa na maswali milioni moja na moja ambayo angependa kumuuliza kimemsibu kitu gani. Alipomuangalia vizuri aligundua kuwa Charles alikuwa amelengwa na machozi na yeye mwenyewe Vivian alijigundua kuwa machozi yameanza kufurika kwenye macho yake na kuanza kufanya michirizi kwenye pande za mashavu yake huku yakiharibu poda, wanja, na vimetameta alivyokuwa amepambwa navyo kwa ajili ya harusi hiyo. Wapenzi hao wawili walijikuta wakibubujikwa na machozi.
Charles alimgeukia Padre Minja na kumwashiria amsogelee ili amnong?oneze kitu.
?Baba Padre, naweza kujibu swali hilo, lakini kabla sijafanya hivyo naomba nafasi ya kuungama kitu kwako na kwa Vivian, tafadhali? Alisema kwa sauti ya upole, ya chini lakini iliyokuwa na uhakika wa kile isemacho. Padre Minja alitingisha kichwa kuashiria amemuelewa. Vivian hakujua Charles amemnong?oneza kitu gani padre huyo, maswali akilini mwake yaliongezeka na kuwa milioni moja na mbili. Padre Minja aliwageukia waumini ambao wote walikuwa kimya wakisubiri kwa hamu kujua ni nini kinaendelea. Waliokuwa wambeya hawakuchelewa kuanza kuzusha uvumi, na wenye simu wakaanza kutumiana ujumbe kuwa Vivian kaachwa altareni!
?Wapendwa katika Bwana!? Padre Minja alianza kuzungumza kwa sauti kakamavu iliyomgutusha kila mtu kanisani humo. ?Tumesikia jibu la bibi harusi, lakini bwana harusi kabla ya kutoa jibu lake, ameniomba twende chemba ili afanya maungamo ya dhati kabla kutoa jibu hilo. Hivyo kwaya itaendelea kuburudisha wakati mimi, bwana harusi na bibi harusi tutakuwa sakristia na pindi tukimaliza tutarudi. Asanteni? Alimaliza huku akiwaongozwa wachumba hao kuelekea kwenye sakristia pembezoni mwa kanisa hilo.
Padre Minja alivuta viti vitatu vilivyokuwa vimekunjwa pembeni ya meza ya na kuviweka katikati ya chumba hicho ambacho mapadre hutumia kubadilishia mavazi na vitu vyenye wakfu huhifadhiwa. Kwaya ya Mtakatifu Joseph iliendelea kuongoza kwa nyimbo mbalimbali kama ile ya ?Nakupenda Maria?, ?Jina Maria? na ?Enendeni Duniani Kote?. Wakati nyimbo hizo zikiendelea kuimbwa, Padre Minja na Vivian walikaa kitako ili kusikiliza maungamo ya Charles Mugisha; maungamo ambayo yalichelewesha ufungaji wa ndoa ya njiwa hao wawili wapendanao. Baada ya sekunde chache kupita na baada ya kuvuta pumzi ndefu, Charles alianza kusimulia ni kitu gani kilimfanya asitishe mwitikio wake wa ndoa. Padre Minja na Vivian kama wanafunzi watulivu darasani, walisikiliza kwa makini.
* * *
Hadi mwaka 1990 nikiwa na miaka 25 nilikuwa bado mimi bikira. Nilikuwa sijawahi kulala na mwanamke zaidi ya kuishia kuwatamani tu kwa nje. Bila ya shaka utajiuliza ilikuwaje nichelewe kiasi hicho kuanza mapenzi. Ukweli wa mambo ni kuwa mimi nilikuwa ni mseminari wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza na mwaka huo ulikuwa ni mwaka wangu wa mwisho kabla sijapandishwa kwenye madaraja ya altare, yaani ushemasi na baadaye Upadre. Moyoni mwangu niliamini kabisa kuwa mimi nilikuwa na wito wa upadre na tangu utoto nilijiandaa kutimiza ndoto hiyo.
Ni kwa sababu hiyo basi niliwakwepa kinadada kama wana ukoma, na kila nikimuona dada mwenye kuvutia nilijikuta nikisali sala ya baba yetu nikirudia rudia maneno ya ?usitutie majaribuni? mara nyingi. Niliweza kutawala tamaa zangu hasa kwa kupenda kujisomea vitabu mbalimbali vya kitaaluma, kuandika, na kufanya kazi nyingi za mikono. Muda wangu mwingi wa ziada nilikuwa natembelea wagonjwa, kushiriki katika kwaya, na kufundisha tuition vijana wa sekondari hasa masomo ya Fizikia na Kemia. Niliyapenda maisha yangu na sikuwa na shaka kabisa kuwa nitakuwa padre mzuri, mcha Mungu, na mtumishi wa watu.
Ndoto yangu hiyo ilipeperuka siku ile isiyo na jina, miezi mitatu kamili kabila sijavikwa ushemasi kwenye ibada ya Misa Takatifu kwenye viwanja vya jangwani ambayo ilikuwa iongozwe na Baba Mtakatifu Yohanne Paulo II akiwa katika ziara yake ya Kichungaji. Nilikuwa katika mapumziko ya mwisho toka seminari ya Kipalapala, siku ile ambapo mambo yote yaliniharibikia na mwelekeo wa maisha yangu kubadilishwa. Wakati wa mapumziko hayo ya karibu miezi miwili nilikuwa nimefikia parokia ya Pugu ambako nilikuwa nasaidia shughuli mbalimbali pale parokiani. Licha ya kusaidia parokia ya Pugu mara nyingi mida ya mchana nilikuwa nakuja St. Joseph kwa kusaidia kazi mbalimbali za ofisini na kupata uzoefu wa kikazi. Nilikuwa ni mwanafunzi wa Padre Peter Mhonda aliyekuwa msaidizi wa Askofu wa Dar. Niliona fahari kila nikija hapa na kushirikia katika misa, huduma mbalimbali na shughuli mbalimbali.
Siku hiyo hata hivyo nilikuwa nimemaliza shughuli zangu mapema St. Joseph na Sr. Maria Goretti alinichukua kwa gari hadi eneo la Tazara ambako nilikuwa kwa kawaida nasubiri mabasi ya kwenda Pugu. Ilikuwa jioni kwenye majira ya saa kumi na mbili hivi wakati jua limeanza kutua ingawa joto la Dar bado liliendelea nilikuwa nimekaa chini ya Kibanda cha kusubiria mabasi kilichoko nje ya jengo la Tazara ikiangalia upande wa Buguruni. Nilikuwa nimevalia nguo za kawaida tu zilizonifanya nionekane kama mfanyakazi wa kampuni fulani na mkononi nilikuwa nimeshika gazeti la Alasiri ambalo ndio lilikuwa limetinga mitaani mida hiyo.
(Itaendelea kesho)