PDA

View Full Version : Alichofanya Masha kisirudiwe tena!



mwanakijiji
11-28-2008, 10:22 AM
Mojawapo ya vitu vya kushangaza na ambavyo vimezua maswali kwa watu ni kitendo cha Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Lawrence Masha kwenda kutembelea gereza la Keko ambako waliowahi kuwa mawaziri wanashikiliwa rumande.

Hicho peke yake kisingeshangaza isipokuwa mazingira ya safari yake hii yanatufanya tuamini kuwa kama alifanya kwa nia njema basi ameonesha kushindwa kupima maamuzi yake na pia kutufanya tuhoji uwezo wake wa kuwa kiongozi huru hasa saa na wakati huu ambapo Taifa letu limeanza kupambana na ufisadi wa ngazi zajuu.

Mjadala uliopo mbele yetu siyo kwanini yeye Waziri ametembelea Gereza kwani itakuwa ni kituko kama Waziri hatembelei magereza kujiona hali iliyopo au kwa sababu yoyote iliyomo ndani ya kazi yake.

Hata hivyo kitendo cha Waziri Masha kwenda Keko siku moja baada ya marafiki zake wa karibu wa familia kwenda rumande na hasa kwenda kwa gari lake binafsi bila kutoa angalau taarifa kwa vyombo vya habari kuwa atakuwa na ziara ya namna hiyo kinazua maswali ambayo majibu yake hadi sasa hayajatosheleza.

Kama kweli alikuwa katika shughuli za kawaida, iweje iwe katika gereza la Keko na siku moja baada ya kina Basil Mramba na Yona kutupwa huko? Yawezekana mtu akasema kuwa alienda kuangalia hali zao zikoje n.k lakini tutahoji mbona kuna wafungwa wengi wanaoshikiliwa kwenye magereza yetu kwanini hawa kina Mramba na Yona wapate upendeleo huu maalum?

Yawezekana mwingine akasema kuwa alienda pale kuwapelekea ujumbe wa aina fulani au kuchukua ujumbe wa aina fulani. Hilo nalo litatufanya tuhoji kiini cha ujumbe huo. Ni ujumbe gani huo mzito ambao ulishindwa kupitishwa kwa Kamishna wa Magereza au Mkuu wa Gereza kumuhitaji Waziri kwenda kusikiliza? Kama ni suala la rufaa au hali mbaya, si ndio maana watuhumiwa wana mawakili wao na wangeweza kwenda mahakamani kutoa malalamiko yao kama walivyofanya?

Kwa ufupi ni kuwa Waziri Masha ameonesha ukosefu mkubwa wa hekima na upendeleo wa wazi na hivyo kutishia mchakato mzima wa utafutwaji na upatikanaji wa haki katika suala la kina Mramba. Bw. Masha aombe radhi na kuwahakikishia wananchi kuwa jambo kama hilo halitatokea tena kwani siyo tu linahoji uwezo wake wa kuongoza lakini zaidi linatufanya tujiulize kama kweli serikali yetu iko impartial na kumuacha Mkurugenzi wa Mashtaka na Mahakama kufanya kazi yake.

Ni matumaini yetu kuwa kitendo hicho alichokifanya hatokifanya tena katika mazingira kama haya na kwa namna ya kificho kama hivi. Vinginevyo kama kuna mchezo wameamua kucheza basi wajue kuwa wananchi wako macho wakati wote.

M.M.

Mr. XXX
11-28-2008, 07:26 PM
Sasa waziri asiende kufanya kazi zake kama kawaida kwa kuwaogopa nyinyi? Masha alienda pale kama Waziri sasa hamtaki?

duru langu
11-30-2008, 02:02 AM
Sasa waziri asiende kufanya kazi zake kama kawaida kwa kuwaogopa nyinyi? Masha alienda pale kama Waziri sasa hamtaki?

Swala ni timing la hiyo ziara yake. Je alitembelea na mahabusu wengine au ndio aliishia
kuwaona watukuka tu? Je hiyo ziara ilipangwa tangu awali au ni ya dharura?

duru langu
11-30-2008, 02:03 AM
Maadam yeye mheshimiwa na serikali hawaoni kosa basi hakika jambo hilo litarudiwa tu.

dRU
12-03-2008, 06:23 PM
Sasa waziri asiende kufanya kazi zake kama kawaida kwa kuwaogopa nyinyi? Masha alienda pale kama Waziri sasa hamtaki?

Kamwe haitakuwa busara kuingilia urafiki ama ukaribu baina ya familia kwa familia na hakuna mtu mwenye busara akatoa lawama eti kwa nini fulani kenda mtembelea fulani ama hosptalini ama gerezani au hata nyumbani. Hayo ni maswala yao binafsi kabisa na hayana hila yeyote mbele ya jamii.

Swala linakuja wakati kama huu kwamba Mheshimiwa Masha ni waziri wa mambo ya ndani, ni si punde kuna mawaziri wa zamani wamepelekwa huko gerezani na ikatokea yeye kwenda tembelea gereza hilo.. Kwa mtazamo wa haraka haraka ambao hauhitaji mtu kuwa mwenye akili sana kuliona ni kwamba lazima matembezi haya yataunganishwa na matukio hayo ya mawziri kwenda gerezani.

Hivyo basi kwa mtiririko huu wa mawazo, ndipo yakaandikwa haya na ndilo jambo la msingi kulitazama katika swala hili. Ninarudia, kusema kwamba KAMWE hakuna mtu ambaye ataingilia mahusiano ya kifamilia ama kirafiki kwa yeyeote pasi kuwepo utata na hasa utata ambao utaifanya jamii kubwa kufikiria kiyume na matarajio ya wengi.

Kama mimi ningekuwa katika nafasi ya Mheshimiwa Masha basi ningefanya moja kati ya haya, kwenda gerezani kiofisi na kuweka bayana azma ya matembezi ama kwenda kama raia wa kawaida wakati wa saa za kuona wafungwa na kupitia taratibu za kawaida na siyo VIP kuongea na hao marafiki ama ndugu zangu!!! Halina utata asilani!!

Lini tutajifunza busara za kawaida kama hizi jamani!!!? Ni Busara na hekima ya kufikiri itatuwezesha kuepusha lawama nyingi zisizo maana kwetu na hasa VIONGOZI!!!

:confused:

gadiel55
12-06-2008, 08:57 AM
Kwa kweli alichofanya mheshimiwa Masha ni kitendo kizuri na tena cha kibinadamu...LAKINI bahati mbaya sana hakutumia BUSARA wala HEKIMA.

Inaonekana kwamba ana katabia ka kukurupuka tu. Kuna uwezekano kwamba kalewa madaraka huyu bwana. Ana mambo mengi sana sasa hivi yanayoonyesha kwamba hafikirii consequences kabla hajasema au kutenda mambo fulani fulani. Issues za Albino na Mzee Mengi zinakuja kichwani...

mwanakijiji
12-06-2008, 10:02 AM
Lakini hakuna mtu anayeweza kumsaidia na hekima..

dRU
12-06-2008, 11:36 PM
Wallah, ya Musa hayajatulia tunayaona ya Firauni!! Sasa naona mambo mengi yanayolandana na tabia ama hulka za watu yanajitokeza, sasa ni mlolongo wa maajabu ya busara za Mheshimiwa Masha... yoote haya yanahitaji kuangaliwa na kupewa suluhu kwa pande zote ambazo zimeguswa na matamshi ya mheshimiwa... kazi ipo wanakijiji na bado tutaona na kusikia mengi ya kusikitisha na wakati mwingine kujuta .. kwa nini? ilikuwaje? hivi ni kweli? kunani??:(:(:(

Kepa
12-07-2008, 05:22 PM
Lakini hakuna mtu anayeweza kumsaidia na hekima..

Kukubali kuipewa hiyo hekima nacho ni kipaji ndugu yangu. Kuna watu mpaka akukubalie umshauri (siyo kuukubali ushauri uliompa), Ni lazima uwe umemzidi kwa kila kitu... hayo ndio mawazo ya kizamani,

Zamani walipomchagua kiongozi walikuwa wameweka vigezo kwamba kiongozi lazima awe mtu wa tofauti,
Awashinde wote kwa mali
Awashinde wote kwa watoto
Awashinde wote kwa mashamba
Awashinde wote kwa wake. etc. ..... Hawakuwahi kufanikiwa kumpata kiongozi aliyekuwa na vigezo vyote hivyo. ( soma hadithi za bibi)

Siku hizi bado kuna watu (tena wengine ni viongozi wetu), bado wana hako kaji-imani kwamba wakichaguliwa kuongoza inamaanisha kwamba wao wameonikana ni mashine!! yaani wanaubongo wa kujua kila kitu, Hawako tayari kusikiliza mawazo ya wanamapinduzi wala wanamageuzi, wanachama wa chama chao wala wale wa chama pinzani, mwanakitongoji wala mwananchi hata kama wanachoongea/ kushauri ni cha muhimu.

Kwa mtaji huo kwa nini tukose viongozi wanaokurupuka na kutoa matamko au kufanya mambo ya ajabu ajabu ili mradi akili yao inawatuma hivyo?

WAKUBWA WISDOM IS SO EXPENSIVE!!

Monica
12-08-2008, 02:20 PM
Huyu waziri kijana kama anataka kuisaidia TRA kufanya kazi si angewashupalia hawa AGRECO wanaotaka kuondoka bila kulipa kodi kuliko kutafuta mzalendo mwenzake aongezewe kodi bandia iliashindwe kulipaafilisiwe? Kweli elimu sio hekima wala busara hivyo ni vipaji mtu hupewa na bwana. Achia ngazi mheshimiwa bado unasumbuliwa na ujana.

mwanakijiji
12-08-2008, 04:55 PM
Huyu waziri kijana kama anataka kuisaidia TRA kufanya kazi si angewashupalia hawa AGRECO wanaotaka kuondoka bila kulipa kodi kuliko kutafuta mzalendo mwenzake aongezewe kodi bandia iliashindwe kulipaafilisiwe? Kweli elimu sio hekima wala busara hivyo ni vipaji mtu hupewa na bwana. Achia ngazi mheshimiwa bado unasumbuliwa na ujana.

Monica, nadhani hilo ndilo tatizo; kile ambacho nakiita 'youthful arrogance'. Unapochanganya ujana na madaraka wakati mwingine unapata combination ya ajabu sana. Tunachoshuhudia kuhusu Masha ndiyo combination hiyo. It is a shame.

Kepa
12-12-2008, 03:30 AM
Monica, nadhani hilo ndilo tatizo; kile ambacho nakiita 'youthful arrogance'. Unapochanganya ujana na madaraka wakati mwingine unapata combination ya ajabu sana. Tunachoshuhudia kuhusu Masha ndiyo combination hiyo. It is a shame.

Ndio maana kuna mahali humu ndani nilijaribiwa kuuliza umri wa huyu jamaa na namna alivyofanikiwa kupandanisha shule yake na kuezeka haraka sana na cheo kababe. Wajenzi huwa wanasema hivi zege ukitaka liwe imara lazima limwagiliwe maji 21 days, kwa hiyo hata kama unapesa na wafanyakazi milioni huwezi kujenga nyumba na kuimaliza ndani ya week moja, vinginevyo uimara wake utakuwa na maswali kibao. Kama kijana wetu amepata maradhi hayo, maana yake inabidi kufanya re- building all over tutake tusitake