mwanakijiji
11-06-2008, 11:35 PM
Habari Leo
?Sote tumeishi katika mfumo ule wa kiuchumi na tunajua ni kiasi gani tuliteseka. Upinzani huu dhidi ya mageuzi ya sasa ya kiuchumi, ni kelele za kisiasa tu kutoka kwa watu wanaojifanya wamesahau hali ilivyokuwa wakati huo,? amesema Rais leo, Alhamisi, Novemba 6, 2008, mjini Arusha.
Rais Kikwete amesema kuwa pamoja na kwamba upinzani huo wa kisiasa utaendelea kujitokeza hapa na hapa na kila baada ya muda, Tanzania kamwe haitarudi nyuma wala kuacha mageuzi yake ya sasa ya kiuchumi ambayo yameleta manufaa makubwa kwa wananchi.
?Kamwe hatutarudi nyuma, katika uchumi unaodhibitiwa na dola, ? amesisitiza Rais Kikwete wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika ya Shirika la Fedha Duniani (IMF) Mama Antoinette Sayeh kwenye ukumbi wa mikutano wa AICC mjini Arusha.
Rais amekutana na Mkurugenzi huyo baada ya kuwa amefungua Mkutano wa 14 wa Vyombo vya Fedha katika Tanzania unaohudhuriwa na watalaam mbali mbali wa masuala ya fedha kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Mikutano hiyo ambayo hufanyika kila mwaka huandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) na Mama Sayeh yuko nchini kuhudhuria mkutano huo.
Waziri wa Fedha na Mipango ya Uchumi, Mustafa Mkullo; Katibu Mkuu wa Wizara iyo, Gray Mgonja; Gavana wa BOT, Profesa Benno Ndullu na gavana wasaidizi ? Dk Enos Bukuku, Juma Reli na Lilla Mkila wamehudhuria mazungumzo hayo kati ya Rais Kikwete na Mama Sayeh.
Rais Kikwete amesema kuwa baadhi ya wanasiasa, kwa sababu zao tu za kisiasa, wamekuwa wakiibuka na upinzani dhidi ya mageuzi hayo muhimu, lakini akaongeza kusema kuwa tatizo la wanasiasa hao ni kwamba wamesahau hali ya uchumi na maisha ya wananchi yalivyokuwa wakati uchumi ukimilikiwa na dola.
?Mara watataka Serikali kuyafukuza makampuni ya madini, mara watasema kuwa nchi haihitaji wawekezaji. Uzuri ni kwamba haya hayatoki kwa wananchi. Ni ya sisi wanasiasa. Na unajua tena mwenendo wetu wanasiasa, kwa kadri unavyopigiwa makofi?Wakati mwingine baadhi yetu tunasahau haraka,? amesema Rais na kusisitiza:
?Lakini napenda kukuhakishia kuwa hakuna kurudi nyuma. Tumefanya maamuzi, tumeona faida ya maamuzi hayo. Mageuzi yamesaidia sana nchi yetu. Tutaendelea, na maneno haya ya wanasiasa yatafikia siku yataisha tu.?
Rais Kikwete pia amemweleza Mkurugenzi huyo kuhusu hatua ambazo zimechukuliwa mpaka na Serikali katika kumaliza tatizo la Malipo ya Madeni katika Akaunti ya Nje (EPA) katika BOT.
?Tumefanya kila linalowezekana kuhusu EPA. Kumbuka haya ni madeni ya karibu miaka 30 iliyopita. Lakini sasa tumefikia kwenye hatua za kisheria. Tumeanza mchakakato wa kisheria. Tumejifunza mengi kuhusu mifumo yetu ya udhibiti na muhimu hapa ni kuhakikisha kuwa jambo kama hili halirudiwi tena,? amesema Rais na kuongeza:
?Dhamira yetu sasa ni kuongozwa na utawala wa kisheria, na siyo kuruhusu wanasiasa kutumia EPA kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe. Sasa kila kila kitu kiko mikononi mwa DPP (Mkurugenzi wa Mashitaka wa Serikali).
Mwisho wa siku yeye ndiye mwenye madaraka na mamlaka ya mwisho kisheria. Mamlaka yake ni ya kikatiba, na wala haliwezi kuwa suala la uamuzi wa kisiasa.
Kamwe hata mimi siwezi kumwingilia.?
?Sote tumeishi katika mfumo ule wa kiuchumi na tunajua ni kiasi gani tuliteseka. Upinzani huu dhidi ya mageuzi ya sasa ya kiuchumi, ni kelele za kisiasa tu kutoka kwa watu wanaojifanya wamesahau hali ilivyokuwa wakati huo,? amesema Rais leo, Alhamisi, Novemba 6, 2008, mjini Arusha.
Rais Kikwete amesema kuwa pamoja na kwamba upinzani huo wa kisiasa utaendelea kujitokeza hapa na hapa na kila baada ya muda, Tanzania kamwe haitarudi nyuma wala kuacha mageuzi yake ya sasa ya kiuchumi ambayo yameleta manufaa makubwa kwa wananchi.
?Kamwe hatutarudi nyuma, katika uchumi unaodhibitiwa na dola, ? amesisitiza Rais Kikwete wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika ya Shirika la Fedha Duniani (IMF) Mama Antoinette Sayeh kwenye ukumbi wa mikutano wa AICC mjini Arusha.
Rais amekutana na Mkurugenzi huyo baada ya kuwa amefungua Mkutano wa 14 wa Vyombo vya Fedha katika Tanzania unaohudhuriwa na watalaam mbali mbali wa masuala ya fedha kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Mikutano hiyo ambayo hufanyika kila mwaka huandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) na Mama Sayeh yuko nchini kuhudhuria mkutano huo.
Waziri wa Fedha na Mipango ya Uchumi, Mustafa Mkullo; Katibu Mkuu wa Wizara iyo, Gray Mgonja; Gavana wa BOT, Profesa Benno Ndullu na gavana wasaidizi ? Dk Enos Bukuku, Juma Reli na Lilla Mkila wamehudhuria mazungumzo hayo kati ya Rais Kikwete na Mama Sayeh.
Rais Kikwete amesema kuwa baadhi ya wanasiasa, kwa sababu zao tu za kisiasa, wamekuwa wakiibuka na upinzani dhidi ya mageuzi hayo muhimu, lakini akaongeza kusema kuwa tatizo la wanasiasa hao ni kwamba wamesahau hali ya uchumi na maisha ya wananchi yalivyokuwa wakati uchumi ukimilikiwa na dola.
?Mara watataka Serikali kuyafukuza makampuni ya madini, mara watasema kuwa nchi haihitaji wawekezaji. Uzuri ni kwamba haya hayatoki kwa wananchi. Ni ya sisi wanasiasa. Na unajua tena mwenendo wetu wanasiasa, kwa kadri unavyopigiwa makofi?Wakati mwingine baadhi yetu tunasahau haraka,? amesema Rais na kusisitiza:
?Lakini napenda kukuhakishia kuwa hakuna kurudi nyuma. Tumefanya maamuzi, tumeona faida ya maamuzi hayo. Mageuzi yamesaidia sana nchi yetu. Tutaendelea, na maneno haya ya wanasiasa yatafikia siku yataisha tu.?
Rais Kikwete pia amemweleza Mkurugenzi huyo kuhusu hatua ambazo zimechukuliwa mpaka na Serikali katika kumaliza tatizo la Malipo ya Madeni katika Akaunti ya Nje (EPA) katika BOT.
?Tumefanya kila linalowezekana kuhusu EPA. Kumbuka haya ni madeni ya karibu miaka 30 iliyopita. Lakini sasa tumefikia kwenye hatua za kisheria. Tumeanza mchakakato wa kisheria. Tumejifunza mengi kuhusu mifumo yetu ya udhibiti na muhimu hapa ni kuhakikisha kuwa jambo kama hili halirudiwi tena,? amesema Rais na kuongeza:
?Dhamira yetu sasa ni kuongozwa na utawala wa kisheria, na siyo kuruhusu wanasiasa kutumia EPA kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe. Sasa kila kila kitu kiko mikononi mwa DPP (Mkurugenzi wa Mashitaka wa Serikali).
Mwisho wa siku yeye ndiye mwenye madaraka na mamlaka ya mwisho kisheria. Mamlaka yake ni ya kikatiba, na wala haliwezi kuwa suala la uamuzi wa kisiasa.
Kamwe hata mimi siwezi kumwingilia.?