PDA

View Full Version : Jenerali Mboma achukua fomu CCM; Mbeya Vijijini



mwanakijiji
12-12-2008, 08:14 PM
Aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania Gen. Robert Mboma leo amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Mbeya vijijini kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Marehemu Richard Nyaulawa.

Mboma anakuwa mwana CCM wa 10 kuchukua fomu hizo. Hivi karibuni kijarida cha Cheche kimamtaja Gen Mboma kuwa ni miongoni mwa watu ambao wanahusika na kampuni ya Meremeta ambayo inadaiwa kuchota mabiilioni ya fedha toka Benki Kuu. Angalia kwenye sehemu ya "File Cabinet"

Ach-F
12-13-2008, 12:56 AM
Aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania Gen. Robert Mboma leo amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Mbeya vijijini kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Marehemu Richard Nyaulawa.

Mboma anakuwa mwana CCM wa 10 kuchukua fomu hizo. Hivi karibuni kijarida cha Cheche kimamtaja Gen Mboma kuwa ni miongoni mwa watu ambao wanahusika na kampuni ya Meremeta ambayo inadaiwa kuchota mabiilioni ya fedha toka Benki Kuu. Angalia kwenye sehemu ya "File Cabinet"

Isije kuwa anakimbilia fomu ili aje kufukia mashimo yake ya meremeta!

mwanakijiji
12-16-2008, 04:51 PM
Inaonekana Gen. Mboma hatapata nafasi ya kujisafisha ndani ya CCM baada ya kubwagwa kwenye kura ya maoni jana..