mwanakijiji
12-14-2008, 02:38 AM
Kuna kila dalili ya kumrudisha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania ambaye alijiuzulu kufuatia kuhusishwa na kashfa ya Richmond Mhe. Edward Lowassa kwenye nafasi ya uongozi wa juu wa serikali au ndani ya chama.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya kuaminika Mhe. Lowassa anaangaliwa kurudisha kwenye nafasi "yenye nguvu" ili kuhakikisha kuwa wakati CCM inaelekea kwenye uchaguzi mkuu 2010 basi Lowassa ahakikishwe amerudi kwenye upande wa Rais Kikwete baada ya kujikuta amewekwa nje kufuatia kujiuzulu kwake Uwaziri Mkuu mapema mwaka huu.
Inasadikiwa kuwa kurudishwa kwa Lowassa kwenye nafasi ya juu ndiyo njia pekee ya yeye kutokugombea 2010 dhidi ya Rais Kikwete na hivyo kuepusha mgongano kama ule wa Afrika ya Kusini katika ya aliyekuwa Rais Bw. Thabo Mbeki na aliyewahi kuwa Makamu wake Bw. Jacob Zuma.
Tunazo taarifa za uhakika mkubwa ni nafasi gani inaandaliwa kwa ajili ya Lowassa na itatengenezwa vipi.
Fuatilia kijarida cha Cheche ambacho kinaendelea kufuatilia suala hili taratibu.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya kuaminika Mhe. Lowassa anaangaliwa kurudisha kwenye nafasi "yenye nguvu" ili kuhakikisha kuwa wakati CCM inaelekea kwenye uchaguzi mkuu 2010 basi Lowassa ahakikishwe amerudi kwenye upande wa Rais Kikwete baada ya kujikuta amewekwa nje kufuatia kujiuzulu kwake Uwaziri Mkuu mapema mwaka huu.
Inasadikiwa kuwa kurudishwa kwa Lowassa kwenye nafasi ya juu ndiyo njia pekee ya yeye kutokugombea 2010 dhidi ya Rais Kikwete na hivyo kuepusha mgongano kama ule wa Afrika ya Kusini katika ya aliyekuwa Rais Bw. Thabo Mbeki na aliyewahi kuwa Makamu wake Bw. Jacob Zuma.
Tunazo taarifa za uhakika mkubwa ni nafasi gani inaandaliwa kwa ajili ya Lowassa na itatengenezwa vipi.
Fuatilia kijarida cha Cheche ambacho kinaendelea kufuatilia suala hili taratibu.