mwanakijiji
12-18-2008, 04:59 PM
Ngeleja: Tuko tayari kutoa taarifa ya Kiwira bungeni
2008-12-18 12:35:30
Na Joseph Mwendapole (Nipashe)
Wizara ya Nishati na Madini, imeahidi kupasua jipu hivi karibuni kuhusu nani mmiliki wa mgodi wa wa makaa ya mawe wa Kiwira, ambao unahusishwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.
Akizungumza na Nipashe jana, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema kwa kuwa suala hilo liliibuliwa bungeni, basi jibu hilo watalitoa huko huko bungeni.
Alipoulizwa Wizara yake inatarajia kutoa jibu hilo katika mkutano upi wa Bunge, Ngeleja alisema hilo linategemea zaidi ratiba itakayopangwa na Bunge.
Alisema tayari wizara yake ina taarifa ya kutoa kuhusu mgodi huo na kwamba wanachosubiri ni kusoma taarifa hiyo watakapopewa muda.
Mgodi huo umekuwa ukihusishwa na aliyekuwa Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona.
Kwa pamoja wanadaiwa kujiuzia mgodi huo kwa Sh. milioni 700 wakati thamani halisi ya mgodi huo ni Sh. bilioni nne.
Inadaiwa kuwa licha ya kujimilikisha mgodi huo kwa bei hiyo ya kutupa na kumiliki asilimia 80 kwa kutumia Kampuni yao ya TanPower Resources Limited, kiasi walicholipa ni Sh. milioni 70 tu kati ya Sh. milioni 700.
Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP), nayo ilikaririwa siku chache zilizopita ikisema kuwa itatoa taarifa ya uchunguzi wa mgodi wa Kiwira hivi karibuni, ambapo DPP, Elieza Feleshi, alisema ofisi yake bado inalifanyia uchunguzi suala hilo.
Alipoulizwa kwanini uchunguzi huo unachukua muda mrefu, Feleshi alisema wanafanya uchunguzi huo kwa umakini ili kutenda haki kwa pande zinazohusika.
``Bado tunalifanyia kazi ila halitakaa sana kila kitu kitawekwa hadharani hivi karibuni msiwe na haraka tuacheni tufanye kazi kwanza,`` alisema Feleshi.
Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro (CCM), alikuwa wa kwanza kuibua tuhuma katika mkutano wa Bunge wa Aprili mwaka huu, alipowataja bungeni Mkapa na Yona kuwa wanamiliki mgodi huo na walijiuzia kwa bei ya kutupa na kupendekeza kuwa wanastahili kuchunguzwa na kuchukuliwa hatua.
Kimaro alisema mwaka 2004, Mkapa kwa kushirikiana na Yona, walianzisha Kampuni ya TanPower Resources Ltd na mwaka mmoja baadaye wakauziwa machimbo ya Kiwira kimya kimya.
Alisema katika mauziano hayo ya siri, TanPower Resources Limited, ilikuwa iilipe serikali Sh. milioni 700 katika mradi huo uliogharimu zaidi ya Sh. bilioni 4.
Hata hivyo, Kimaro alisema cha kushangaza ni kwamba, kampuni hiyo ilifanya malipo ya awali ya Sh. milioni 70 tu.
Kimaro alisema mwaka 2006, Mkapa na Yona, waliingia mkataba na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa ajili ya kufua umeme kwa makubaliano ya kulipwa `capacity charge` (gharama za uwekezaji bila kujali kwamba wamefua umeme au la) ya Sh. milioni 146 kila siku (dola 3.6 milioni kwa mwezi) pasipo kufuata utaratibu.
2008-12-18 12:35:30
Na Joseph Mwendapole (Nipashe)
Wizara ya Nishati na Madini, imeahidi kupasua jipu hivi karibuni kuhusu nani mmiliki wa mgodi wa wa makaa ya mawe wa Kiwira, ambao unahusishwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.
Akizungumza na Nipashe jana, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema kwa kuwa suala hilo liliibuliwa bungeni, basi jibu hilo watalitoa huko huko bungeni.
Alipoulizwa Wizara yake inatarajia kutoa jibu hilo katika mkutano upi wa Bunge, Ngeleja alisema hilo linategemea zaidi ratiba itakayopangwa na Bunge.
Alisema tayari wizara yake ina taarifa ya kutoa kuhusu mgodi huo na kwamba wanachosubiri ni kusoma taarifa hiyo watakapopewa muda.
Mgodi huo umekuwa ukihusishwa na aliyekuwa Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona.
Kwa pamoja wanadaiwa kujiuzia mgodi huo kwa Sh. milioni 700 wakati thamani halisi ya mgodi huo ni Sh. bilioni nne.
Inadaiwa kuwa licha ya kujimilikisha mgodi huo kwa bei hiyo ya kutupa na kumiliki asilimia 80 kwa kutumia Kampuni yao ya TanPower Resources Limited, kiasi walicholipa ni Sh. milioni 70 tu kati ya Sh. milioni 700.
Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP), nayo ilikaririwa siku chache zilizopita ikisema kuwa itatoa taarifa ya uchunguzi wa mgodi wa Kiwira hivi karibuni, ambapo DPP, Elieza Feleshi, alisema ofisi yake bado inalifanyia uchunguzi suala hilo.
Alipoulizwa kwanini uchunguzi huo unachukua muda mrefu, Feleshi alisema wanafanya uchunguzi huo kwa umakini ili kutenda haki kwa pande zinazohusika.
``Bado tunalifanyia kazi ila halitakaa sana kila kitu kitawekwa hadharani hivi karibuni msiwe na haraka tuacheni tufanye kazi kwanza,`` alisema Feleshi.
Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro (CCM), alikuwa wa kwanza kuibua tuhuma katika mkutano wa Bunge wa Aprili mwaka huu, alipowataja bungeni Mkapa na Yona kuwa wanamiliki mgodi huo na walijiuzia kwa bei ya kutupa na kupendekeza kuwa wanastahili kuchunguzwa na kuchukuliwa hatua.
Kimaro alisema mwaka 2004, Mkapa kwa kushirikiana na Yona, walianzisha Kampuni ya TanPower Resources Ltd na mwaka mmoja baadaye wakauziwa machimbo ya Kiwira kimya kimya.
Alisema katika mauziano hayo ya siri, TanPower Resources Limited, ilikuwa iilipe serikali Sh. milioni 700 katika mradi huo uliogharimu zaidi ya Sh. bilioni 4.
Hata hivyo, Kimaro alisema cha kushangaza ni kwamba, kampuni hiyo ilifanya malipo ya awali ya Sh. milioni 70 tu.
Kimaro alisema mwaka 2006, Mkapa na Yona, waliingia mkataba na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa ajili ya kufua umeme kwa makubaliano ya kulipwa `capacity charge` (gharama za uwekezaji bila kujali kwamba wamefua umeme au la) ya Sh. milioni 146 kila siku (dola 3.6 milioni kwa mwezi) pasipo kufuata utaratibu.