mwanakijiji
12-25-2008, 10:19 PM
Mwandishi Wetu
Daily News; Wednesday,December 24, 2008 @21:15
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimemtaka Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kujibu tuhuma za ubadhirifu wa fedha unaomkabili ndani ya chama chake na kumwacha Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kwa kuwa ni msafi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda, Richard Tambwe alisema CCM imesikitishwa na maneno yaliyotolewa na Mbowe dhidi ya Rais huyo mstaafu kuwa asiende kwenye kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Mbeya Vijijini, vinginevyo watamchafua.
Tambwe alisema baadhi ya magazeti ya jana yalimnukuu Mbowe akisema kuwa Chadema kitamchafua Mwinyi na kumvunjia heshima ikiwa ni pamoja na kubadilisha msimamo wa chama hicho kwa kile walichokiita kumsamehe Rais Mwinyi kwa makosa aliyofanya huko nyuma.
?Tumesikitishwa na kauli hii ambayo inathibitisha upungufu mkubwa wa Mbowe na chama chake ambacho siku zote kimekuwa mstari wa mbele kuchafua majina ya watu bila ya kuwa na ushahidi au ukweli wowote,? alisema Tambwe.
?Mbowe ambaye ni kijana mdogo sana asiyekaribia hata kidogo kwa umri wa baadhi ya watoto wa Rais Mwinyi, alipaswa kuonyesha heshima na adabu kwake kwa kuzingatia kwamba ni kama baba yake,? aliongeza Tambwe.
Alisema badala ya kujiandaa kutaka kumchafua Mzee Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa, jambo ambalo halitafanikiwa kutokana na rekodi yake safi iliyotukuka ya kulitumikia taifa, ni vyema Mbowe na chama chake wakatoa majibu ya tuhuma zinazowakabili kwanza.
Alizitaja tuhuma hizo ni pamoja na Mbowe kufanya udanganyifu wa matumizi ya fedha zilizotolewa na Taasisi ya Westminister Foundation ya Uingereza kupitia chama cha Conservative kwa ajili ya ununuzi wa pikipiki kwa wilaya zote nchini ikiwa ni msaada kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu uliopita ambazo hazikununuliwa.
?Pikipiki ambazo baadhi ya wanachama wakiongozwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti, marehemu Chacha Wangwe wakati huo na wameendelea kulalamikia kwamba fedha za pikipiki hizo zilitumiwa na watu wachache kwa manufaa yao binafsi,? alisema Tambwe.
Tambwe alizitaja tuhuma nyingine kuwa ni madai ya ukabila uliokithiri ndani ya chama hicho uliopelekea wabunge watano kati ya wote wa viti maalumu kutoka Mkoa wa Kilimanjaro na mmoja aliyetoka Kigoma ni ndugu wa karibu na kiongozi mmoja mwandamizi huku viongozi wengine makao makuu wakiwa wanatoka kwenye familia au ukoo mmoja.
Tuhuma ya tatu Tambwe alisema Mbowe pia anadaiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za chama kwa kukidai dola 181,949 sawa na Sh 218,338,546 ambazo hadi Agosti mwaka huu alikwishalipwa Sh milioni 175, akidai kuwa alitumia fedha zake wakati wa uchaguzi na chama kimrudishie wakati hakuna ushahidi wowote jinsi fedha zilivyotumika.
?Ni aibu tena ni kashfa kubwa kwa chama, kwa viongozi wa ngazi yake anayepiga kelele za ufisadi kutofuata taratibu za kitaasisi katika kununua huduma jambo ambalo ni ufisadi mtupu,? alisema Tambwe. Kiongozi huyo aliongeza kuwa Mwinyi atakwenda Mbeya kama alivyopangiwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kuzindua kampeni hizo za CCM Januari 4, mwakani na chama chake kina uhakika wa kushinda. Aidha, alisema Chadema siyo washindani wa CCM kwa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2005, chama hicho cha Demokrasia na Maendeleo kilishika nafasi ya nne.
My Take:
Je, wapinzani kabla ya kukikonyoshea vidole CCM ni lazima kwanza kabisa wajiangalie wao wenyewe? Kwamba kama kwako kuna matatizo basi usioneshe matatizo ya jirani yako?
Daily News; Wednesday,December 24, 2008 @21:15
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimemtaka Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kujibu tuhuma za ubadhirifu wa fedha unaomkabili ndani ya chama chake na kumwacha Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kwa kuwa ni msafi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda, Richard Tambwe alisema CCM imesikitishwa na maneno yaliyotolewa na Mbowe dhidi ya Rais huyo mstaafu kuwa asiende kwenye kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Mbeya Vijijini, vinginevyo watamchafua.
Tambwe alisema baadhi ya magazeti ya jana yalimnukuu Mbowe akisema kuwa Chadema kitamchafua Mwinyi na kumvunjia heshima ikiwa ni pamoja na kubadilisha msimamo wa chama hicho kwa kile walichokiita kumsamehe Rais Mwinyi kwa makosa aliyofanya huko nyuma.
?Tumesikitishwa na kauli hii ambayo inathibitisha upungufu mkubwa wa Mbowe na chama chake ambacho siku zote kimekuwa mstari wa mbele kuchafua majina ya watu bila ya kuwa na ushahidi au ukweli wowote,? alisema Tambwe.
?Mbowe ambaye ni kijana mdogo sana asiyekaribia hata kidogo kwa umri wa baadhi ya watoto wa Rais Mwinyi, alipaswa kuonyesha heshima na adabu kwake kwa kuzingatia kwamba ni kama baba yake,? aliongeza Tambwe.
Alisema badala ya kujiandaa kutaka kumchafua Mzee Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa, jambo ambalo halitafanikiwa kutokana na rekodi yake safi iliyotukuka ya kulitumikia taifa, ni vyema Mbowe na chama chake wakatoa majibu ya tuhuma zinazowakabili kwanza.
Alizitaja tuhuma hizo ni pamoja na Mbowe kufanya udanganyifu wa matumizi ya fedha zilizotolewa na Taasisi ya Westminister Foundation ya Uingereza kupitia chama cha Conservative kwa ajili ya ununuzi wa pikipiki kwa wilaya zote nchini ikiwa ni msaada kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu uliopita ambazo hazikununuliwa.
?Pikipiki ambazo baadhi ya wanachama wakiongozwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti, marehemu Chacha Wangwe wakati huo na wameendelea kulalamikia kwamba fedha za pikipiki hizo zilitumiwa na watu wachache kwa manufaa yao binafsi,? alisema Tambwe.
Tambwe alizitaja tuhuma nyingine kuwa ni madai ya ukabila uliokithiri ndani ya chama hicho uliopelekea wabunge watano kati ya wote wa viti maalumu kutoka Mkoa wa Kilimanjaro na mmoja aliyetoka Kigoma ni ndugu wa karibu na kiongozi mmoja mwandamizi huku viongozi wengine makao makuu wakiwa wanatoka kwenye familia au ukoo mmoja.
Tuhuma ya tatu Tambwe alisema Mbowe pia anadaiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za chama kwa kukidai dola 181,949 sawa na Sh 218,338,546 ambazo hadi Agosti mwaka huu alikwishalipwa Sh milioni 175, akidai kuwa alitumia fedha zake wakati wa uchaguzi na chama kimrudishie wakati hakuna ushahidi wowote jinsi fedha zilivyotumika.
?Ni aibu tena ni kashfa kubwa kwa chama, kwa viongozi wa ngazi yake anayepiga kelele za ufisadi kutofuata taratibu za kitaasisi katika kununua huduma jambo ambalo ni ufisadi mtupu,? alisema Tambwe. Kiongozi huyo aliongeza kuwa Mwinyi atakwenda Mbeya kama alivyopangiwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kuzindua kampeni hizo za CCM Januari 4, mwakani na chama chake kina uhakika wa kushinda. Aidha, alisema Chadema siyo washindani wa CCM kwa kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2005, chama hicho cha Demokrasia na Maendeleo kilishika nafasi ya nne.
My Take:
Je, wapinzani kabla ya kukikonyoshea vidole CCM ni lazima kwanza kabisa wajiangalie wao wenyewe? Kwamba kama kwako kuna matatizo basi usioneshe matatizo ya jirani yako?