mwanakijiji
12-26-2008, 08:42 AM
Katika utawala wa kidemokrasia na katika nchi ambayo inaongozwa na katiba, hakuna chombo muhimu na chenye uzito mkubwa katika kulinda Katiba hiyo kama Jeshi. Mahali popote duniani, Jeshi ndicho chombo cha mwisho kabisa chenye kuweza kulinda Taifa na ndio pekee ambao kwa maisha yao wanaapa kulinda mipaka ya Taifa hilo.
Maana yake, jeshi ndicho chombo pekee chenye uwezo, jukumu, na kuhakikisha Taifa linakuwepo. Polisi wakishindwa, Usalama wa Taifa wakishindwa, Magereza wakishindwa, Wanasiasa wakishindwa, viongozi wa kidini wakishindwa; Jeshi linatakiwa kuweza. Ndiyo ngao yetu pekee ya kuhakikisha kuwa tunaendelea kubakia kuwa huru na kuwa Taifa.
Ninapofikiria kifo cha Brig. Nyirenda ambaye leo watu wanamtaja kama shujaa, ninapowafikiria kina Mwita Kyaro, Walden, Musuguri, Tumainieli Kiwelu na wengine waliopitia jeshi letu na nikiwafikiria hawa kina Mboma na wenzake na sakata zima la Meremeta na dhahabu, ninabakia na swali moja tu:
Jeshi linapohusishwa na ufisadi, na uongozi wake ukakaa kimya, je linaweza kweli kulinda uhuru wetu? Je tuko salama mikononi mwao kama wao wenyewe ndiyo wanatajwa katika ufisadi?
Maana yake, jeshi ndicho chombo pekee chenye uwezo, jukumu, na kuhakikisha Taifa linakuwepo. Polisi wakishindwa, Usalama wa Taifa wakishindwa, Magereza wakishindwa, Wanasiasa wakishindwa, viongozi wa kidini wakishindwa; Jeshi linatakiwa kuweza. Ndiyo ngao yetu pekee ya kuhakikisha kuwa tunaendelea kubakia kuwa huru na kuwa Taifa.
Ninapofikiria kifo cha Brig. Nyirenda ambaye leo watu wanamtaja kama shujaa, ninapowafikiria kina Mwita Kyaro, Walden, Musuguri, Tumainieli Kiwelu na wengine waliopitia jeshi letu na nikiwafikiria hawa kina Mboma na wenzake na sakata zima la Meremeta na dhahabu, ninabakia na swali moja tu:
Jeshi linapohusishwa na ufisadi, na uongozi wake ukakaa kimya, je linaweza kweli kulinda uhuru wetu? Je tuko salama mikononi mwao kama wao wenyewe ndiyo wanatajwa katika ufisadi?