mwanakijiji
01-05-2009, 05:10 PM
(Kutoka IssaMichuzi)
Mabasi yote ya abiria nchini yatatakiwa kuwa na mikanda na abiria wote watatakiwa kujifunga mikanda hiyo muda wote wa safari wakiwa ndani ya vyombo hivyo vya usafiri, Jeshi la Polisi limetangaza wikiendi hii.
Kamanda wa Trafiki nchini, Afande James Kombe, amesema hatua hiyo inakuja katika jitihada za kupunguza vifo na majeraha makubwa yanayosababishwa kila itokeapo ajali.
Sheria kama hii imekuwa ikitumika nchini Kenya ambako inasemekana imesaidia sana katika kupunguza maafa kwa abiria wakati wa ajali.
Amesema sheria ya mikanda imo katika kanuni za Mamlaka ya usafiri wa barabara na majini (SUMATRA) na kwamba abiria akikutwa hajafunga mkanda ataadhibiwa.
Kamanda huyo amesema wamiliki wa mabasi wameshajulishwa juu ya hatua hiyo na kuwataka wahakikishe kila basi la abiria litaloagizwa liwe na mikanda ya kujifunga abiria.
Amesema tayari shirika la Usafir Dar (UDA) limeshaanza kutekeleza sheria hiyo ya kuweka mikanda kwenye mabasi yake yote ya abiria, na kwamba sharti mojawapo ya kusajili basi la abiria litakuwa ni kuwa na mikanda kwa abiria.
Kuhusu abiria kusimama ndani ya basi, amesema wamiliki wa mabasi hayo inabidi wapate leseni itayowaruhusu kusimamisha idadi maalumu ya abiria wakiwa safarini, na kwamba wataosimama wawekewe mabomba ya kushikilia.
Vile vile Kamanda Kombe amesema hivi sasa wamiliki wa mabasi ya abiria hasa yaendayo mikoani wametii amri ya kuwa na madereva wawili wataokuwa wakipokezana endapo safari itazidi masaa manane. Ameongeza pia kwamba mabasi ya abiria ya masafa marefu yameruhusiwa kusafiri hadi saa sita usiku. Awali ilikuwa mwisho saa 12 jioni.
Kiasi cha ajali 16,640 za barabarani zimerekodiwa kutokea na kusababbisha vifo vya watu 2,362 na majeruhi 14,825 kati ya Januari na Oktoba mwaka uliopita pekee. Wilaya ya Kinondoni inaongoza kwa kuwa na jumla ya ajali za barabarani 3,871 zilizopoteza maisha ya watu 169.
Mkoa wa Lindi ndio wenye ajali chache, ukiwa umerekodi ajali 114 zilizopoteza masiha ya watu 66 mwaka jana.
Swali:
Tuna wasomaji sehemu mbalimbali duniani, ni wapi ambapo mabasi ya abiria yana mikanda? Yawezekana wanatafuta suluhisho la tatizo ambalo kiini chake siyo ukosefu wa mikanda ya abiria?
Mabasi yote ya abiria nchini yatatakiwa kuwa na mikanda na abiria wote watatakiwa kujifunga mikanda hiyo muda wote wa safari wakiwa ndani ya vyombo hivyo vya usafiri, Jeshi la Polisi limetangaza wikiendi hii.
Kamanda wa Trafiki nchini, Afande James Kombe, amesema hatua hiyo inakuja katika jitihada za kupunguza vifo na majeraha makubwa yanayosababishwa kila itokeapo ajali.
Sheria kama hii imekuwa ikitumika nchini Kenya ambako inasemekana imesaidia sana katika kupunguza maafa kwa abiria wakati wa ajali.
Amesema sheria ya mikanda imo katika kanuni za Mamlaka ya usafiri wa barabara na majini (SUMATRA) na kwamba abiria akikutwa hajafunga mkanda ataadhibiwa.
Kamanda huyo amesema wamiliki wa mabasi wameshajulishwa juu ya hatua hiyo na kuwataka wahakikishe kila basi la abiria litaloagizwa liwe na mikanda ya kujifunga abiria.
Amesema tayari shirika la Usafir Dar (UDA) limeshaanza kutekeleza sheria hiyo ya kuweka mikanda kwenye mabasi yake yote ya abiria, na kwamba sharti mojawapo ya kusajili basi la abiria litakuwa ni kuwa na mikanda kwa abiria.
Kuhusu abiria kusimama ndani ya basi, amesema wamiliki wa mabasi hayo inabidi wapate leseni itayowaruhusu kusimamisha idadi maalumu ya abiria wakiwa safarini, na kwamba wataosimama wawekewe mabomba ya kushikilia.
Vile vile Kamanda Kombe amesema hivi sasa wamiliki wa mabasi ya abiria hasa yaendayo mikoani wametii amri ya kuwa na madereva wawili wataokuwa wakipokezana endapo safari itazidi masaa manane. Ameongeza pia kwamba mabasi ya abiria ya masafa marefu yameruhusiwa kusafiri hadi saa sita usiku. Awali ilikuwa mwisho saa 12 jioni.
Kiasi cha ajali 16,640 za barabarani zimerekodiwa kutokea na kusababbisha vifo vya watu 2,362 na majeruhi 14,825 kati ya Januari na Oktoba mwaka uliopita pekee. Wilaya ya Kinondoni inaongoza kwa kuwa na jumla ya ajali za barabarani 3,871 zilizopoteza maisha ya watu 169.
Mkoa wa Lindi ndio wenye ajali chache, ukiwa umerekodi ajali 114 zilizopoteza masiha ya watu 66 mwaka jana.
Swali:
Tuna wasomaji sehemu mbalimbali duniani, ni wapi ambapo mabasi ya abiria yana mikanda? Yawezekana wanatafuta suluhisho la tatizo ambalo kiini chake siyo ukosefu wa mikanda ya abiria?