PDA

View Full Version : JK aitaka Israel kusitisha mapigano



mwanakijiji
01-09-2009, 04:50 PM
JK aitaka Israel isimamishe mashambulizi Gaza


na Mwandishi Wetu


RAIS Jakaya Kikwete ameitaka Serikali ya Israel kusitisha haraka matumizi ya nguvu za kijeshi kwenye Ukanda wa Gaza na badala yake itumie njia ya kidiplomasia ili kutafuta ufumbuzi wa amani na Palestina.

Kwa mujibu taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa vyombo vya habari jana, ilisema wito huo aliutoa juzi alipokuwa akizungumza kwa nyakati tofauti na Balozi wa Palestina, Dk. Nasri Khalli Abu Jaish na Balozi wa Israel nchini, Jacob Kdeidar.

Katika mazungumzo hayo Rais Kikwete aliwaeleza kuwa Tanzania inasikitishwa na machafuko yanayoendelea Palestina, ambako Jumanne wiki hii walishambulia moja ya shule 23 za Umoja wa Mataifa na kuua Wapalestina 50 huku wakiwajeruhi 100.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa kutokana na mashambulizi hayo, vifo vya Wapalestina waliopoteza maisha vinazidi kuongezeka ambapo hadi sasa zaidi ya Wapalestina 700 wamefariki dunia na 3,000 wamejeruhiwa tangu Israel ilipoivamia Gaza.

Rais Kikwete aliwaeleza mabalozi hao kuwa serikali yake inapinga matumizi ya kijeshi katika mgogoro wa Palestina na Israel, kwani njia hiyo si suluhisho la vurugu bali ni kichocheo cha machafuko.

Alisema Tanzania imekata rufaa kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na wanachama wa Quartet kwa ajili ya kupinga mauaji ya Gaza, ambayo yanaendelea kushamiri kwa kasi na kuomba mashirika ya kimataifa kujitokeza kupinga mauaji hayo.

Swali:
Kwanini JK hakumtafuta mwakilishi wa Hamas ili kumpatia ushauri wa kusitisha makombora? kama alivyomuita Balozi wa Israeli na kuitaka nchi yake isitishe vita huko Gaza? Kwanini hajawaita Morgan na Mugabe; au Bashir na viongozi wa Janjaweed na wengine kule Darfur? Vipi kuhusu viongozi wa Somalia? Vita ni vita, na vifo vya raia vyote vinauma!

Akajase
01-09-2009, 07:19 PM
Ninamashaka na msukumo wa msingi hasa uliomfanya JK kuyatamka hayo am kuitaka israel kutekeleza hiyo kauli yake. Amesahau kuwa kulikuwa na vurugu kama hizo hapo kabla Israel na hamas wakaingia makubaliano ya kusimamisha vita/mashambulizi, yakadumu kwa miezi sita tu. Mvunjaji wa makubaliano alikuwa ni Hamas kwa kutupa makombora Israel.Sasa JK alitaka Israel anyamaze watu wake waendelee kufa? pili Israel akaanza kulenga ngome na nyumba ambazo Hamas wanatumia kwa shughuli zao. Hamas na wakazidisha mashambulizi kwenye makazi ya watu wa Israel ilihali wao wanakimbilia kujificha katika nyumba za wapalestina wengine na kutuma makombora toka huko.
JK sielewi anauchungu gani kwa wapalestina wakati watanzania wanakufa kule Mara hasa Tarime.Sina uhakika kama anajua idadi ya watanzania waliokufa kwa mapigano ya koo jumla yake ni ngapi, na kwamba mgogoro huu umedumu kwa muda mrefu kiasi gani hata kuwafanya wakina mama kulia kwa sababu watoto wao wanakimbia mazingira hayo , wazee kushindwa kufanya shughuli za uzalishaji achilia mbali wale waliokufa kwa mikuki.
kingozi mwenye uchungu mkuu na wapalestina lakini ana moyo wa ganzi kwa wakongo weusi wanaouliwa na Nkunda wakati vikosi vya kiitelijinsia vinajua namna nkunda anavyopata silaha. Anaachwa ili maelfu ya wakongo wafe. Anauchungu na wapalestina lakini hakuwahi kutoa tamko la wazi na kali kwa Al Bashir jinsi anavyowaua wasudani wa kusini ( wanaDafur).
Sometime is better to be quite than speaking, and the spoken words hurt those who hear them.

Ach-F
01-10-2009, 02:03 AM
Huyu naye Jakaya anyamaze tu anatia kichefu chefu.

Cool Richie
01-10-2009, 10:45 AM
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Hamas walivunja Makubaliano ya kusitisha mashambulizi baina yao na Israel yaliyowekwa karibu miezi sita iliyopita kwa kuishambulia Usraeli kwa maroket yao. Inelezwa kwamba Israeli ilikaa kimya bila kujibu mashambulizi hayo (pengine kwa kuheshimu makubaliano hayo), mpaka uvumilivu ulipowaishia nao wakaanza kufanya mashambulizi kwa kuua raia wakiwamo watoto na wanawake, na kuharibu miundombinu ya taifa la Palestina.
Kama hali ni hivyo kweli, mi naona wa kulaumiwa zaidi ni Hamas. Lakini kinyume na hivyo, kwa nini Dunia inailaumu Israeli, na JK naye anaunga mkono kauli za Duniai? Au tuseme anajikomba? Ili apate nini sasa?
Jibu ninalolipata hapa ni kwamba, mataifa machanga yakichokoza mataifa makubwa, si kiti, lakini mataifa makubwa yakiwapiga mataifa madogo kwa uchokozi wao ni uonevu!! Huo si ustaarabu hata kidogo. Kama kuna facts zaidi ya hali niliyoileza, naomba kuelezwa hapa.

mwanakijiji
01-10-2009, 07:43 PM
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Hamas walivunja Makubaliano ya kusitisha mashambulizi baina yao na Israel yaliyowekwa karibu miezi sita iliyopita kwa kuishambulia Usraeli kwa maroket yao. Inelezwa kwamba Israeli ilikaa kimya bila kujibu mashambulizi hayo (pengine kwa kuheshimu makubaliano hayo), mpaka uvumilivu ulipowaishia nao wakaanza kufanya mashambulizi kwa kuua raia wakiwamo watoto na wanawake, na kuharibu miundombinu ya taifa la Palestina.
Kama hali ni hivyo kweli, mi naona wa kulaumiwa zaidi ni Hamas. Lakini kinyume na hivyo, kwa nini Dunia inailaumu Israeli, na JK naye anaunga mkono kauli za Duniai? Au tuseme anajikomba? Ili apate nini sasa?
Jibu ninalolipata hapa ni kwamba, mataifa machanga yakichokoza mataifa makubwa, si kiti, lakini mataifa makubwa yakiwapiga mataifa madogo kwa uchokozi wao ni uonevu!! Huo si ustaarabu hata kidogo. Kama kuna facts zaidi ya hali niliyoileza, naomba kuelezwa hapa.

Nadhani mentality ya watu wengi ni kuwa kama mdogo anakurushia mawe, wewe usimjimu kwa mapanga. Wanaona kuwa Hamas ni mchokozi lakini "kauchokozi" kake ka kutuma "vijikombora" haulingani kabisa na majibu ya Israel ambayo ni kuvamia kijeshi na mauaji ya watu zaidi ya 700.

Ach-F
01-12-2009, 12:10 AM
Watu wanakufa kila siku Zimbabwe, Congo, Somalia, Sudan n.k. sasa hawa Palestinians ambao wamewakumbatia Hamas wakiuawa 1000 tu kuna shida gani? Je, wanafahamu idadi ya wanaokufa Somalia au Sudan? Ujinga mtupu acheni wayamalize wenyewe. Waarabu wa Pemba wanajuana kwa vilemba.