PDA

View Full Version : Ukurasa wa mbele



mwanakijiji
01-13-2009, 12:14 AM
Wapendwa wanakijiji, bila ya shaka utakuwa umeona tofauti katika ukurasa huu hasa kwenye logo. Tuko kwenye utaratibu wa kuanza kuroll out vikolombwezo mbalimbali ambavyo vitakufanya uone fahari kuwa kijijini hapa kuliko kwenda mjini! Siku chache zijazo tutawawekea mahali pa kuweka picha zenu za mambo mbalimbali na utakuwa na uhuru wote wa kusimamia picha hizo, kinyume na tovuti nyinginee utakuwa na uhuru wa kuruhusu watu watolee maoni au wasitolee maoni n.k

Lakini zaidi tunataka pawe mahali ambapo watu watakuwa salama katika picha zao na kwa vile tuko US sheria za nchi hii kuhusu mambo ya usalama wa kwenye mtandao (cyber laws) zipo na tutazikimbilia wakati wowote kuna tatizo, to the full extent of the law. Hata hivyo tunatarajia zaidi kuwa na picha za matukio mbalimbali.

Hivyo, ingawa ukurasa wa mwanzo sasa hivi uko kwenye Forum, ukurasa wa mbele wa tovuti (home page) inabakia pale pale na habari zinaendelea kutiririka kama kawaida. Hivyo ukiwa kwenye forum usisite kutembelea "home" page kwani yaweza kuwa na vitu ambavyo havipo huku kwenye forum.

All breaking news, zitakuwa zinapatikana kwa kawaida ukurasa ule wa mbele na hapa, lakini habari nyingi zaidi zitakuwa zinapatikana huko kwenye ukurasa wa nyumbani.

Na yote haya yanakuja kwako bureeeeee!!

ponda
01-22-2009, 03:08 PM
kwahiyo tuhame JF?

Unasubiri NINI? au unapendelea UBABE wa kule?
Hivi kuna tofauti kati ya Mwanakijiji na Mzee Mwanakjj?

mwanakijiji
01-22-2009, 04:42 PM
Unasubiri NINI? au unapendelea UBABE wa kule?
Hivi kuna tofauti kati ya Mwanakijiji na Mzee Mwanakjj?

Huyo aliyejiandikisha kama Mzee Mwanakjj ni miongoni mwa mahasimu wangu wa muda mrefu. Kwa sababu hiyo siyo tu amefungiwa lakini hata IP anayotumia itafungiwa.

mfumwa
01-22-2009, 10:46 PM
Huyo aliyejiandikisha kama Mzee Mwanakjj ni miongoni mwa mahasimu wangu wa muda mrefu. Kwa sababu hiyo siyo tu amefungiwa lakini hata IP anayotumia itafungiwa.

Hongera Mwanakijiji kwa wazo lako la kuboresha hiki kijiji. Lakini nami nina wazo moja, huyu jamaa "Mzee Mwanakjj" huna haja ya kumfungia, kama unavyosema ni hasimu wako. Duniani huwezi kosa mahasimu, na mahasimu ndio wakati fulani wanajenga. Kama atakuwa anatumia lugha za matusi, kweli huyo hafai, lakini kama ni upinzani tu, haina haja ya kumfungia. Ni mawazo yangulakini...

mwanakijiji
01-22-2009, 11:13 PM
Hongera Mwanakijiji kwa wazo lako la kuboresha hiki kijiji. Lakini nami nina wazo moja, huyu jamaa "Mzee Mwanakjj" huna haja ya kumfungia, kama unavyosema ni hasimu wako. Duniani huwezi kosa mahasimu, na mahasimu ndio wakati fulani wanajenga. Kama atakuwa anatumia lugha za matusi, kweli huyo hafai, lakini kama ni upinzani tu, haina haja ya kumfungia. Ni mawazo yangulakini...

mfumwa... siyo mtu wa hivyo. Mimi kutofautiana mawazo na mtu yeyote inakaribishwa kwa moyo wote. Ila huyu alipoingia jana aliingia na matusi lukuki, akabandika mapicha ya ngono za mashoga kuanzia eneo hili, na akawa ameregister kwa kutumia emails zenye "mwanakijiji" na "mzee.mwanakijiji".

Hofu yangu ni kuwa ana lengo la kulaghai watu hasa wale wanaoniamini, mwisho anaweza kupokea private messages za kwangu na hivyo kufanya madhara makubwa sana kwa kijiwe chetu hiki. Hakuingia kwa nia njema. Aliingia kama adui si mpinzani wa hoja.

mfumwa
01-22-2009, 11:17 PM
mfumwa... siyo mtu wa hivyo. Mimi kutofautiana mawazo na mtu yeyote inakaribishwa kwa moyo wote. Ila huyu alipoingia jana aliingia na matusi lukuki, akabandika mapicha ya ngono za mashoga kuanzia eneo hili, na akawa ameregister kwa kutumia emails zenye "mwanakijiji" na "mzee.mwanakijiji".

Hofu yangu ni kuwa ana lengo la kulaghai watu hasa wale wanaoniamini, mwisho anaweza kupokea private messages za kwangu na hivyo kufanya madhara makubwa sana kwa kijiwe chetu hiki. Hakuingia kwa nia njema. Aliingia kama adui si mpinzani wa hoja.

Kama analeta picha za ngono, huyo fungia mpaka IP address, hafai kabisa. Hapo nakuunga mkono hawezi kuchafua hali ya hewa.