PDA

View Full Version : Sihami CCM - Mwakyembe



mwanakijiji
01-15-2009, 08:18 PM
Dk. Mwakyembe awakatalia wapiga kura kuondoka CCM (Mwananchi)
Richard Kilumbo,Kyela

MBUNGE wa Jimbo la Kyela Dk Harrison Mwakyembe,amesema hana mpango na wala hafikirii kukiacha Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kujiunga vyama vya upinzani nchini.

DK. Mwakyembe alisema hakuna Chama chochote cha upinzani kinachoweza kufananishwa kwa ubora , umakini, uzuri wa sera na hata uwingi wa wanachama na CCM.

Kauli hiyo aliitoa juzi kwenye mkutano wake na wananchi wa jimbo lake uliofanyika viwanja vya Siasa mjini hapa ambapo baadhi ya wananchi walimtaka kuihama CCM ili afanye kazi ya kufichua mafisadi kupitia kambi ya upinzani.

Mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Erick Satta mkazi wa mjini hapa alisema wananchi wa jimbo lake wanamwamini mbunge huyo kwa kiwango kikubwa, lakini wanaingiwa na shaka na mahali aliko (CCM)ambako alisema wananchi wanaamini, mbunge wao anabanwa, na hawezi kusema lolote linalopingana na sera na itikadi ya Chama.

Satta alisema ili aweze kufanikisha azma ya kuwakomboa wananchi wa Tanzania mbunge huyo hana budi kubadilika na kujiunga na mageuzi ambako ataungwa mkono kutoka kwa wananchi na viongozi wenzake wa vyama vya upinzani.

Alimtaka mbunge huyo kukubaliana na matakwa ya wananchi wengi wanaomshinikiza kuihama CCM kwa madai kimejaa mafisadi wasiowezwa kushughulikiwa na kiongozi wa ndani ya Chama hicho.

" Tunakupenda,tuko nawe na tutakuchagua mwaka 2010, ukiwa ndani ya Chama kingine, cha Siasa na siyo CCM" alisema Satta.

Akijibu hoja kwa kupinga msimamo huo, Dk. Mwakyembe aliwabeza wale wote wanaomshinikiza kuihama CCM na kusisitiza kwamba, hapa nchini hakuna Chama cha siasa kilicho makini na chenye sera safi zinazotekelezeka na chenye wanachama wengi kuliko CCM.

Dk. Mwakyembe alisema, mtu yeyote anayetaka kupambana na maovu yanayofanywa na baadhi ya watu walio na nia mbaya na Taifa lao hana budi kuendelea kubaki ndani ya CCM.

"Ukitaka kufanya mambo yako vizuri,na unataka usikilizwe, uishi maisha marefu ni bora, ubaki CCM kuliko ukawa kwenye upinzani na kupayuka mambo bila ushahidi wa kutosha.

Alisema utetezi na uchungu wa mtu yoyote hauwezi kusikika, na kufanyiwa kazi kwa kina, kama utafanywa na wapinzani walio nje ya CCM.

Akitetea msimamo wake alisema ni lazima watu washindane na kubezana kwa hoja kuliko kuleta ubishi usio na manufaa.

"Fikiria ujasiri unaofanywa na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete , ni mkubwa mno, lakini wapo watu wanaobeza jambo ambalo hata CCM ingefanya nini, wapo watu ambao wataendelea kubeza tuu.

Alisema, Rais Kikwete amefanya mambo mengi na yenye ushujaa kwa kuweza kuwafikisha viongozi waandamizi aliowahi kufanya nao kazi katika awamu mbalimbali akiwa Waziri , lakini amefanikisha kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya dola wakituhumiwa kuitia hasara Serikali ya awamu ya tatu kwa kuruhusu msamaha wa kodi ya Sh 11 bilioni.

"Hivi, ni nani kati yenu, anayeweza kuruhusu rafiki yake wa karibu akamatwe, hata kama amekosea?, na ni Kiongozi gani katika awamu zote tatu zilizopita aliyeweza kuwa jasiri akaruhusu marafiki na viongozi wenzake wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya dola kama si Rais Kikwete"aliwauliza wananchi Dk.Mwakyembe.

Hata hivyo, pamoja na kusifia mafanikio mbalimbali yaliyoletwa na Serikali ya awamu ya nne, Dk Mwakyembe alizungumzia pia kazi nzuri iliyofanywa na Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, ambaye alisema aliimarisha na kuinua Uchumi wa nchi.

Kuhusu sakata la kukatika katika kwa umeme wilayani Kyela , mbunge huyo alisema atayapeleka mawazo ya wananchi waliomtaka mbunge wao ayafikishe mambo hayo kwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngereja ya kuruhusu wananchi wa Kyela wautumie umeme unaozalishwa na Kiwira Coal Mine ili kuepuka na kero hiyo.

mfumwa
01-17-2009, 08:52 AM
"Ukitaka kufanya mambo yako vizuri,na unataka usikilizwe, uishi maisha marefu ni bora, ubaki CCM kuliko ukawa kwenye upinzani na kupayuka mambo bila ushahidi wa kutosha.

Vyama vya siasa ni kama vyombo cha usafiri (gari, meli, ndege, treni). Unaweza kuta magari yoye ni bora, lakini madereva na makondakta wao wanatofautiana. Hivyo kuhama chama si kosa, hata kama kina sera nzuri wakati kinapokosa dira. Na upinzani si dhambi.

Ila kauli ya kusema ukitaka mambo yako yawe mazuri inanikumbusha kauli ya Mheshimiwa Waziri Mkuu katika awamu ya tatu, aliposema ukitaka biashara zako ziende vizuri basi uwe CCM. Na kuhusu kuwa na maisha marefu ukiwa CCM hilo ni gumu kulielewa Mheshimiwa Mwakyembe alikuwa na maana gani.

Dua
01-18-2009, 12:29 AM
Ulitegemea Mwakyembe aseme nini? Yeye na JK lao moja tangu walipokuwa mawaziri. Nothing new there, a lost generation. By the way Mkono mtupu haulambwi. Hivi ni chama gani cha upinzani ambacho kingemtaka/kumwomba Mwakyembe ajiunge nacho?

dickabudi
02-04-2009, 10:24 AM
Upinzani bado kuna kazi vyama vya upinzani bado ni kampuni za binafsi, kumdanganya afisa masjala wizarani na kupata vielelezo nusu nusu vya kutafuta umaarufu si kulisafisha taifa, angalia kwa makini ripoti iliyomlazimisha Mh Lowassa kujiuzulu, utaona umahiri na umakini wa Mwakyembe

Ni afadhali hata CCM tunakoona watu wakibadilishana madaraka, wakifichuana kwenye maovu na kurekebishana, si huko unakokuita kwa wapinzani

Mtu anajitangazia kuwa mgombea urais kabla hata ya miaka minne uchaguzi kufanyika kana kwamba ameagana na Maulana, huyu akipewa rungu tutafika kweli???

Nsaji Mpoki
02-04-2009, 12:48 PM
Mimi nafikiri ni wajibu wetu sote kushiriki katika jambo zima la uendeshaji wa nchi yetu.Ni bahati mbaya wengi wa Watanzania wanasubiri malaika atelemuke aje afanye mabadiliko bila ya wao kushiriki kwa dhati.Tukijitambua nafsi zetu na kushiriki kikamilifu kuleta mabadiliko,basi uongozi imara utapatikana wa kujenga mustakabali wa Taifa letu.Nasisitiza tena wote sisi kwa ujumla tunatakiwa kuwa wadau wa mabadiliko tunayoyataka,bila sisi kuwa washiriki matokeo tunayoyatarajia hayawezi kutokea kamwe.

Mchungaji Ladslaus
02-17-2009, 11:39 PM
Hapa Dr. H. Mwakyembe amesema kweli kuwa "hakuna Chama chochote cha upinzani kinachoweza kufananishwa kwa ubora , umakini, uzuri wa sera na hata uwingi wa wanachama na CCM.

Nawashauri wana jamvini wote ambao sio wana CCM mjiunge na CCM.

CCM ni Nambari wani.

Angeris
02-18-2009, 12:17 AM
Hapo alipo Hon.Mwakyembe ndo panamfaa huko CCM. Upinzani una raha yake ya kutupa changamoto kisiasa nchini ila CCM ndiyo yenyewe kiutawala.

Daywell
03-01-2009, 02:15 PM
mwakyembe uondoke uende wapi komaa humo humo nje kuna nje kuna mbwa mwitu!