PDA

View Full Version : Breaking News: Ajali Arusha



mwanakijiji
01-21-2009, 05:13 PM
Taarifa kutoka Arusha zinasema kuwa kuna magari kama matano yametumbukia katika mto Nduruma nje kidogo ya mji wa Arusha. Kw amujibu wa vyanzo vyetu ajali hiyo imesababishwa na lori la Coca Cola kugongana na magari mengine madogo na kusababisha magari hayo kutumbukia mtoni na mengine kuning'inia kwenye kingo ya mto huo. Hadi hivi sasa kuna watu kadhaa waliofariki na wengine kujeruhiwa. Tutawaletea taarifa kamili hivi punde.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha Bw. Robert Boaz ameiambia KLHN kuwa ajali hiyo imetokea mchana wa leo kwenye barabara ya Arusha Moshi ambalo semi-trailor iligonga basi ambalo nalo likagonga magari mengine madogo. Hadi hivi sasa Bw. Boaz amethibitisha kuwa waliofariki ni watu 16 miongoni mwao ni wanaume 10 na kina mama 6.

Bw. Boaz amesema kuwa walifika eneo la ajali mara moja ambapo waliweza kupata msaada wa wananchi kutoa miili ya marehemu na kuwasaidia majeruhi na kuwakimbiza katika hospitali za Arusha kwa matibabu. "Wananchi wametupatia ushirikiano mkubwa" alisema Bw. Boaz.

Alipoulizwa kuhusu chanzo cha ajali Bw. Boaz alisema kuwa hadi hivi sasa uchunguzi unaendelea ingawa alitoa ushauri kuwa madereva na watumiao vyombo vya usafiri kuwa wanaozinggatia sheria za barabarani ili kuepusha ajali nyingine ambazo kwa kweli si za lazima.

Hii ni ajali kubwa ya tatu kutokea nchini tangu mwaka huu mpya uanze. Ajali moja kubwa nyingine ilitokea karibu wiki moja na kitu iliyopita ambapo watu 27 walikufa baada ya basi la Tashrif kugonga lori la magogo lililokuwa limeegeshwa pembezoni maeneoo ya Hale kwenye barabara ya kuelekea Tanga (Muheza - Segera).

Ajali hiyo ya basi ilitanguliwa na ajali iliyotokea huko Himo Moshi ambapo watu 11 wa familia moja walipoteza maisha yao Januari 4 wakiwa wanarudi kutoka kwenye sherehe za Ubarikio. Basi dogo la (hiace) nalo liliparamia lori lililokuwa limeegeshwa pembezoni.

Ajali za namna hii zimekuwa zikitokea mara kwa mara huku serikali na vyombo vya usalama vikitupa lawama nyingi kwa madereva na watumia barabara wengine kuwa waangalifu wakiwataka wafuate sheria za usalama barabarani.

Matigari
01-22-2009, 04:39 PM
Jambo.

Inasikitisha sana kuona hizi ajali zinatokea mara kwa mara. Imefika point mimi saa nyingine nawakatalia watoto kwenda kwa bibi yao. Wakiondoka nakosa raha mpaka nisikie wamefika, na wanaporudi hivyo hivyo, sina raha mpaka waingie ndani.

Tunachotakiwa ni kujadili suala la elimu ya barabarani, si kwa madereva wa mabasi tu hata sisi wote. Udereva mbaya unachangia sana ajali pamoja na msongamano wa magari ( kwa mfano kama unaona kuwa hutaclear red light, why go into the intersection) Oh nilisahau nobody cares for traffic signs.

Kwa kweli tuwekeane sheria za barabarani, tuzifuate na tusipozifuata tuwajibike. Faini ya shillingi laki mbili kwa kusa dogo ( kama kuvuka red light) itawatia watu adabu. Hii itawezekana tu kama consequences za kutolipa zinakuwa kali.

Tuanze tena kujifunza udereva sisi wote tuache bad habits. NIT mpo?

Najua hii inahitaji utunza data mzuri Nk, lakini hilo linatushinda nini?

mwanakijiji
01-22-2009, 04:43 PM
Jambo.

Inasikitisha sana kuona hizi ajali zinatokea mara kwa mara. Imefika point mimi saa nyingine nawakatalia watoto kwenda kwa bibi yao. Wakiondoka nakosa raha mpaka nisikie wamefika, na wanaporudi hivyo hivyo, sina raha mpaka waingie ndani.

Tunachotakiwa ni kujadili suala la elimu ya barabarani, si kwa madereva wa mabasi tu hata sisi wote. Udereva mbaya unachangia sana ajali pamoja na msongamano wa magari ( kwa mfano kama unaona kuwa hutaclear red light, why go into the intersection) Oh nilisahau nobody cares for traffic signs.

Kwa kweli tuwekeane sheria za barabarani, tuzifuate na tusipozifuata tuwajibike. Faini ya shillingi laki mbili kwa kusa dogo ( kama kuvuka red light) itawatia watu adabu. Hii itawezekana tu kama consequences za kutolipa zinakuwa kali.

Tuanze tena kujifunza udereva sisi wote tuache bad habits. NIT mpo?

Najua hii inahitaji utunza data mzuri Nk, lakini hilo linatushinda nini?

Hivi kweli hakuna jinsi yoyote ya kuepusha ajali hizi zote..

mwanakijiji
01-22-2009, 07:38 PM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salaam za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bwana Isidore Leka Shirima kutokana na vifo vya watu 17 waliofariki kwa ajali mbaya ya barabarani iliyotokea jana tarehe 21 Januari, 2009 na kuhusisha basi la abiria Double Coaster liitwalo Mapenzi ya Mungu na Lori la Kampuni ya Bonite Bottlers.

Watu 16 kati ya waliofariki walikuwa abiria wa basi na mmoja utingo wa Lori. Magari hayo yaligongana katika eneo la daraja la mto Nduruma nje kidogo ya mji wa Arusha. Katika ajali hiyo, watu wengine 14 wamejeruhiwa na kulazwa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Mjini Arusha. Uchunguzi wa awali wa polisi unaonyesha kuwa lori lililoligonga basi, lilikuwa na hitilafu kwenye breki ambazo zilikatika.

?Kwa masikitiko na huzuni kubwa, napenda kwa dhati ya moyo wangu kukutumia salamu za rambirambi wewe Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bwana Isidore Leka Shirima kutokana na vifo vya wenzetu 16 waliofariki papo hapo baada ya basi la Mapenzi ya Mungu kugongana na Lori la Kampuni ya Bonite Bottlers katika eneo la daraja la mto Nduruma. Kupitia kwako nawapa pole familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu na namuomba Mwenyezi Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi Amin.

Kwa watu wote waliojeruhiwa katika ajali hiyo, Rais Kikwete amesema, ?Natambua maumivu makali mnayoyapata hivi sasa kutokana na ajali mbaya iliyotokea, hivyo namwomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na awawezeshe kupona haraka ili muungane tena na familia, ndugu na jamaa zenu?.

Katika salamu zake za rambirambi, Mheshimiwa Kikwete amesema ajali mfululizo zinazotokea hapa nchini hazina budi kuwekewa mikakati madhubuti ya kudhibitiwa kwani mamlaka husika zina uwezo huo. Amesema ni hivi majuzi tu tarehe 10 Januari, 2009 ambapo ajali nyingine iliyotokea mkoani Tanga ikihusisha basi la abiria la Tashrif na Lori la Magogo, ilipoteza maisha ya raia 27 na wengine 18 kujeruhiwa.

?Hatuwezi kuendelea kuvumilia kutokea kwa ajali hizi wakati mamlaka zenye dhamana ya kusimamia Sheria ya Usalama Barabarani zipo?, ameonya Rais Kikwete na kusisitiza, ?tufanye jitihada zote zilizo ndani ya uwezo wetu kupunguza kwa kiwango kikubwa na ikiwezekana kukomesha kabisa ajali hizi za barabarani ambazo katika kipindi kifupi tangu kuanza kwa mwaka mpya, zimeshapoteza maisha ya wenzetu wengi?, amesisitiza Rais Kikwete.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.