PDA

View Full Version : Wamarekani wanazidi kumiminika - why?



mwanakijiji
11-10-2008, 06:28 AM
kwa mara nyingine tena TAnzania imekuwa mwenyeji wa msanii wa Kimarekani ambaye amekuja kutumbuiza. Kwa miaka hii michache iliyopita wasanii mbalimbali hasa wale wenye asili ya Afrika wamekuwa wakija Tanzania aidha kwa kutoa burudani au kwa miradi mbalimbali au hata wale wanaokuja kupumzika tu. Je ni kwa kiasi gani tunanufaika kama TAifa na kuitangaza nchi maana kwa kadiri ninavyoona ni kuwa zaidi wasanii hawa wanaambiana wenyewe kwa wenyewe au kupitia channels zao lakini ni wachache ambao wakirudi Marekani wanaitangaza Tanzania.

Inaonekana kana kwamba Tanzania ni siri yao.

http://www.globalpublisherstz.com/uploads/posts/thumbs/1226149696_kat_de_luna_2.jpg

Hapo mwanadada Kat De Luna akiwa Bongo.

Hapa tena mwanadada huyo:

http://images.starpulse.com/Photos/Previews/Kat-DeLuna-s04.jpg

Huko nyuma Beyonce na mumewe Jay Z walitembelea BOngo pia

http://images.starpulse.com/Photos/Previews/Beyonce-Knowles-sb10.jpg

Desert Eagle
11-10-2008, 09:10 PM
Unajua Braza hako ni ka mradi kazuri kwa hawa jamaa wanaitwa promoters thats where they make a lot of money lakini return kwa nchi hakuna ndio walewale mafisadi wanakua hawana na nia njema ya kuitangaza Tanzania...Kwa kifupi hakuna Mwanamuziki aliewika miaka ya hivi karibuni haja kanyaga Tanzania ukiachia ulio wataja wengine ni;

Willy Smith na Jada Pinkett
John Legend
50 Cent
Lloyd banks
Tony Yayo
Ja Rule
Loon na wenzake watatu
Acon
Mya
memphis bleek
wazaire ndio usiseme


Na wengine kibao, tatizo ni kwamba sector ya entertaiment imehodhiwa na wafanya biashara ambao hawajui ni kitu gani kinaweza kukuletea heshima na histori na kukuweka kwenye kumbukumbu bali wao wanajua wamlete nani ili wapate hela ya kula (Ufisadi=Ubinafsi).

Wafanya biashara kama Kusaga sidhani kama ana programme yoyote inayolenga kuitangaza Tanzania zaidi, bali ni malengo ya kibinafsi ndio yamewajaa. Kule africa kusini waandaaji wanajitahidi kuwatembeza wasanii katika sehem za vivutio vya nchi yao lakini kwetu kina kusaga wana mwandalia Ja Rule Lunch na familia na kampuni nzima badala ya kuwa wabunifu wataitangaza vipi Tanzania kupitia yeye,

Ni mtazamo tu

mwanakijiji
11-11-2008, 06:21 PM
sasa hakuna utaratibu mzuri unaoeleweka kwa sababu kitu ambacho ninakiona ni kuwa ujio wa wasanii hawa ni maarufu ndani ya Tanzania lakini sioni habari zao nje ya Tanzania. Ingekuwa ni njia nzuri kweli ya kuwasiliana.


Wanapokuja watu kama hawa wangetolewa hata Press Release ya Kiingereza na sisi wengine tungerusha kwenye tovuti mbalimbali na vyombo mbalimbali vya habari.