PDA

View Full Version : Breaking News: Dr.Slaa na Dr. Tarab wategwa kielektroniki



mwanakijiji
02-06-2009, 12:05 AM
http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/national/klhnsiren.gif

KLHN/JF Exclusive:

Na. Mwandishi Wetu

Wabunge wawili wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Dr. Wilbroad Slaa na Dr. Ali Tarab Ali wamekuta vyumba vyao vimetegeshwa vyombo ambavyo vinaamini kuwa kuwa ni vya kunasa mawasiliano bila ya wao wenyewe kujua. Habari kutoka Dodoma ambazo zimethibitishwa na Dr. Slaa zimesema kuwa ugunduzi huo umefuatia taarifa za kijasusi ambazo zilipenyezwa kwa waheshimiwa hao kutoka "vyanzo vya kuaminika" kuwa vyumba vyao vimetegeshwa vyombo hivyo na watu ambao KLHN inasita kuwataja kwa sasa.

Taarifa hizo ambazo zilipenyezwa mapema leo zilidokeza kuwa vyumba vya wabunge hao na bila ya shaka baadhi yao wengine viko katika uchunguzi katika jitihada ya kupata taarifa za nini waheshimiwa hao wanapanga, nani wanakutana nao na wanazungumza nini. Vyanzo vya udokezi huo wa habari za kijasusi ambavyo vimezungumza na KLHN kwa masharti ya kutotajwa jina, wadhifa au idara vinasema kuwa vifaa hivyo vya kielektroniki viliingizwa humo kwa njia za kiufundi wa hali ya juu na ilikuwa ni vigumu kugundulika.

Baada ya kupata taarifa hizo Dr. Slaa (Karatu- CHADEMA) hakuzipa uzito mkubwa sana hadi aliporudi hotelini (Hotel 56 iliyoko upande wa Mashariki wa Bunge - Geti la wageni) majira ya saa 12:30 za jioni. Baada ya kufuatilia na kuulizia wahudumu Dr. Slaa aliomba msaada wa kupekua pekua chumba hicho ili kuona kama taarifa alizopewa zina ukweli wowote. Hata hivyo wakiwa wamekata tamaa waliamua kuangalia chini ya godoro/kitanda na kwa sekunde chache walishangazwa na kukuta kifaa ambacho hawakukitambua kikiwa kinamulikamulika taa nyekundu.

Mara moja taarifa ilitolewa kwa Katibu wa Bunge, Polisi, na waandishi wa habari ambao waliwahi kufika hotelini hapo. Wakati hilo linafanyika Dr. Slaa alitaka kuona kama kati ya wabunge wanne waliopo pale ambao wako karibu naye kama wengine nao wamekabiriwa na kitu kama hicho. Wabunge wawili wa CCM ambao majina yao hayajafahimika hawakukuta kitu kama hicho isipokuwa Dr. Ali Talib Ali (CUF - Konde) anayepakana chumba na Dr. Slaa. Hivyo taarifa hizo nazo zilizidi kuwashtua wabunge hao na hasa lengo na madhumuni ya vitu hivyo.

Hadi hivi sasa vyombo mbalimbali vya usalama vilikuwa vinasubiriwa kufika hotelini hapo ili kuhakikisha kuwa vifaa hivyo ni vitu gani, vya nani, na vimewekwa kwa madhumuni gani.

Endapo itagundulika na kuthibitishwa kuwa vifaa hivyo ni vya kunasia sauti au kunasa mawasiliano itakuwa ni mara ya kwanza kwa kugundulika hadharani kuwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametegeshwa namna hiyo na zaidi ya yote itatishia uhuru wa wao kuzungumza, kukutana, au kuwasiliana na mtu yeyote kama raia huru. Zaidi ya yote wataalamu wa kisheria wameidokeza KLHN kuwa endapo hilo ni kweli "basi yeyote atakayekuwa amefanya hivyo atakuwa amevunja Katiba Ibara 18:1" inayotambua uhuru wa mtu binafsi na kukataza mawasiliano yake kuingiliwa nje ya sheria.

Kwa muda mrefu hata hivyo Dr. Slaa amekuwa akilalamikiwa kuvujisha siri za serikali na amewahi kutishiwa kukamatwa na Polisi kutokana na kudai kuwa anazo nyaraka mbalimbali za serikali. Hivi juzi baadhi ya viongozi wa serikali wameoneshwa kuchukizwa na kukerwa na Dr. Slaa kupata taarifa ya barua ya Waziri wa Mambo ya Ndani (anayesimamia Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji, Uokoaji) kwenda kwa Waziri Mkuu kuhusiana na suala la mradi wa Vitambulisho.

Hata hivyo haijulikani kama vifaa hivi vinahusiana kwa namna yeyote na shughuli za Dr. Slaa katika kuibua kashfa mbalimbali za ufisadi. Ikumbukwe kuwa ni Dr. Slaa na viongozi wengine wa upinzani walioibua ile orodha maarufu ya vitendo vya Aibu ambayo hadi hivi sasa baadhi ya walioatajwa wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na kashfa mbalimbali.

Katika kijarida chetu cha Cheche toleo la wiki hii na katika Mtandao wa JamiiForum, Dr. Slaa aliandika kuwapiga mkwara wale wote watakaojaribu kuficha au kuvuruga masuala mbalimbali ambayo wamekuwa wakiyafanyia kazi.

Juhudi za kupata uongozi wa Polisi zinaendelea na tutawapa taarifa pindi tukijua nini kinachoendelea mjini Dodoma.

Angeris
02-06-2009, 01:28 AM
Tusubiri upelelezi, ni mapema kufahamu nia ya tukio hilo. Wakipatikana waliohusika,itakuwa vizuri ila kama watapatikana.

Siasa ina mambo mengi, hao waheshimiwa esp. Dr.W.Slaa wawe waangalifu.

Hii kiboko kwa kweli,vielekroniki tena chini ya godoro!

mwanakijiji
02-06-2009, 02:26 AM
Tusubiri upelelezi, ni mapema kufahamu nia ya tukio hilo. Wakipatikana waliohusika,itakuwa vizuri ila kama watapatikana.

Siasa ina mambo mengi, hao waheshimiwa esp. Dr.W.Slaa wawe waangalifu.

Hii kiboko kwa kweli,vielekroniki tena chini ya godoro!

TAyari vyomboo vya usalama vimefika na kuchukua vifaa hivyo wa ajili ya uchunguzi. Taarifa itatolewa zaidi baadaye.

911
02-06-2009, 07:45 AM
Katika kudodosa kwangu hapa na pale nimesikia kuwa siku ya trh 4/2 mh. alipelekewa mvinyo na wahudumu na ktk kuangalia kwa umakini ilionyesha kuwa kulikuwa na tatizo kwenye kifuniko.Alipouliza wahudumu ni nani aliyeleta mvinyo huo walimjibu kuwa ni mtu wasiyemfahamu hivyo akawaamuru waende wakautupe.But lilipotokea hili la kuweka "vinasa sauti" na wanausalama kufika wale wahudumu waliitoa ile chupa ya mvinyo kwani hawakuwa wameitupa kama walivyoagizwa.Taarifa ni kuwa wanausalama wameichukua ila nachelea kuasimmilate hii na ungaunga scene!!
Pia the minor difference btn the two equipments ni kuwa kilichokuwa kwa mh. Slaa was blinking...Ni hayo tu kwa sasa!!

mwanakijiji
02-06-2009, 08:47 AM
Katika kudodosa kwangu hapa na pale nimesikia kuwa siku ya trh 4/2 mh. alipelekewa mvinyo na wahudumu na ktk kuangalia kwa umakini ilionyesha kuwa kulikuwa na tatizo kwenye kifuniko.Alipouliza wahudumu ni nani aliyeleta mvinyo huo walimjibu kuwa ni mtu wasiyemfahamu hivyo akawaamuru waende wakautupe.But lilipotokea hili la kuweka "vinasa sauti" na wanausalama kufika wale wahudumu waliitoa ile chupa ya mvinyo kwani hawakuwa wameitupa kama walivyoagizwa.Taarifa ni kuwa wanausalama wameichukua ila nachelea kuasimmilate hii na ungaunga scene!!
Pia the minor difference btn the two equipments ni kuwa kilichokuwa kwa mh. Slaa was blinking...Ni hayo tu kwa sasa!!

ina maan kile kilichokuwa kwa Dr. Tarab hakikuwa kina blink?

911
02-06-2009, 11:15 AM
ina maan kile kilichokuwa kwa Dr. Tarab hakikuwa kina blink?
Naam mkuu,kwa nilivyoambiwa ni hivyo kuwa kilichokuwa kwa Dr Tarab kilikuwa hakiblink.Maybe ni different model au design...Tuwaachie watu wa usalama watupe majibu??Im doubting about the loyalty of these usalama people.

mwanakijiji
02-06-2009, 05:18 PM
Naam mkuu,kwa nilivyoambiwa ni hivyo kuwa kilichokuwa kwa Dr Tarab kilikuwa hakiblink.Maybe ni different model au design...Tuwaachie watu wa usalama watupe majibu??Im doubting about the loyalty of these usalama people.

una maana gani? loyalty yao yawezekana siyo kwa serikali tena!

Japhet
02-06-2009, 08:20 PM
it is possible that whoever is behind this issue has his people stationed within the management of the Hotel. Pia ni dhahili kwamba hao wahudumu hasa waliopeleka mvinyo wanamfahamu mtu alyeleta mvinyo huo. Nina wasiwasi kama uchunguzi utatoa any positive results. Ni bora Dr. Slaa akahama hiyo hotel, it is no more safe for him.

mwanakijiji
02-06-2009, 10:08 PM
it is possible that whoever is behind this issue has his people stationed within the management of the Hotel. Pia ni dhahili kwamba hao wahudumu hasa waliopeleka mvinyo wanamfahamu mtu alyeleta mvinyo huo. Nina wasiwasi kama uchunguzi utatoa any positive results. Ni bora Dr. Slaa akahama hiyo hotel, it is no more safe for him.


sasa inakuwaje endapo watu waliopewa kuchunguza jambo hilo wao wenyewe kwa namna moja au nyingine ndiyo wanahusika na sakata hilo?

911
02-06-2009, 11:36 PM
una maana gani? loyalty yao yawezekana siyo kwa serikali tena!
Nah,namaana kuwa they 'might' be among people behind this game.Kwa very simple kisingizio "usalama wa taifa".Kwani kama wanavyosema kuwa hiyo barua ya hivi karibuni ilikuwa imenyofolea kwenye confidential file la wizara ya mambo ya ndani then mayb they were on their move to try to trace the leak,Wametumwa na nani(mimi sijui)

mwanakijiji
02-07-2009, 12:27 AM
Lakini hiyo reasoning mbona faulty; kwanini wasifikiri kuwa hiyo leak imetokea ofisi ya Waziri Mkuu?

911
02-07-2009, 01:19 PM
Lakini hiyo reasoning mbona faulty; kwanini wasifikiri kuwa hiyo leak imetokea ofisi ya Waziri Mkuu?
Popote pale leak itakapokuwa imetokea,ukweli ni kuwa hiyo 'folio 37' ilinyofolewa wizara ya mambo ya ndani(labda kama sikumwelewa vizuri PM).Mtanzania liliripoti kuwa panafanyika uchunguzi hapo wizarani kujua ni nani aliyevujisha siri za serikali.

Ach-F
02-07-2009, 03:14 PM
Serikali ya CCM ndio iko nyuma ya huu ujinga unaoendelea, badala ya kulikwamua taifa iko busy na mafisadi wake wanaowatisha raia ambao wana uchungu na hii nchi na rais wa Jamuhuri yuko kimya na kutulia kama maji mtungini. The day will come ambapo atatakiwa kujibu maswali. Hii ni sawa na yuke mbunge aliyemwaga uchawi kule bungeni wakati wa usiku - AIBU.

pangamawe
02-10-2009, 12:27 PM
Nimesoma kwa masikitiko makubwa suala la Dr Slaa na mwenzie Dr Taarabu kutegeshewa vinasa sauti kwenye vyumba wanavyoishi huko Dodoma. Hili jambo linahuzunisha ambalo lengo lake kuu ni kumtisha Dr Slaa katika vita yake dhidi ya mafisadi. Naamini lengo kuu lilikuwa ni kujaribu kuwabaini watu wanaompatia Dr Slaa taarifa mbalimbali za siri zinazohusu masuala ya ufisadi yalivyoshamiri serikalini. Nakiri hadharani mimi ni mmoja wa raia wema wa nchi hii ambao tumekuwa tukimpatia Dr Slaa taarifa za siri kuhusu ufisadi kwa vile tumemuona ni mtu mzalendo na hana chembechembe za ufisadi na tukimpa anazifanyia kazi ipasavyo. Tumewahi kuwapa wabunge kadhaa siku za nyuma lakini badala ya kuzifanyia kazi walifanya maelewano na mafisadi wakakatiwa chao na ufisadi ukaendelea as usual. Lazima niseme wazi Dr Taarabu hausiki na hili hata kidogo bali ni lengo la hao waliotumwa na Masha kuvuruga akili za watanzania ili wadhani ni usalama wa taifa waliofanya hivyo kwa lengo la kufuatilia nyendo za wapinzani. Hii ni kazi ya Masha katka jitihada zake za kutaka kumjua aliyempa Dr Slaa taarifa juu ya zabuni ya vitambulisho vya taifa ambayo Masha amekuwa akiingilia kwa ajili ya rushwa ambayo kapewa na kampuni ya Sagem katika makubaliano yaliyofikiwa mwaka jana Masha alipotembelea HQ za Sagem. Nina hakika kama ingekuwa ni usalama wa taifa mapungufu mengi yaliyojitokeza katika vinasa sautyi hivi yasingekuwepo. Mfano ukubwa wa vifaa vyenyewe siamini kama TISS wanatumia vinasa sauti vikubwa namna hiyo, pili brand names na other specifications zilizoandikwa katika vifaa hivyo ingekuwa ni hawa jamaa wa TISS wangehakikisha wanafuta traces zote juu ya identity ya vifaa hivyo. Hii ni kazi ya Masha na mafisadi wenzie. Dr Slaa Aluta contunua!

kilbark
02-11-2009, 12:39 PM
Hawa jamaa wanataka kutuchezea mchezo wa madogori. Hiyo ishu ya Masha kuingilia masula ya zabuni ni kinyume na taratibu za utumishi wa umma suala la usiri na utendaji wa kazi ni vitu viwili tofauti kama huyo Masha angekuwa yukosahihi tusingalisikia haya yote. Kiufupi Masha kaudhihirishia umma kuwa yeye ni fisadi lililokubuhu.