mwanakijiji
02-12-2009, 07:41 AM
Hii ibara ya 15:1 ya Katiba ya CCM ni lazima ifutwe kama hawa CCM wanaweza kujadili mambo kwa uhuru. Vinginevyo kwa mtindo huu tutafika pabaya sana. Inasikitisha kuona kana kwamba Spika Sitta ameanza kulewa sifa zisizo na maana na matokeo yake ni kuanza kuliburuza Bunge na papo hapo kuliburuza Taifa.
Kuna jaribio la kulifanya Bunge liwe juu ya Urais na Mahakama:
Mara ya kwanza alisifiwa pale alipompasha Rais Kikwete na kumtaka awe "mkali kidogo" na watu wakampongeza kwa kuweza kusema/kuelekeza ukweli kwa Rais na watu waliona kuwa ni kitu ambacho hakikuwahi kufikiriwa.
Hivi majuzi amegongana na Mahakama na kimsingi kampiga mkwara Jaji Mkuu kitu ambacho ninakipinga kabisa.
Chochote anachopanga kufanya, hivi sivyo jinsi ya kwenda kwani it will backfire!
Kuna jaribio la kulifanya Bunge liwe juu ya Urais na Mahakama:
Mara ya kwanza alisifiwa pale alipompasha Rais Kikwete na kumtaka awe "mkali kidogo" na watu wakampongeza kwa kuweza kusema/kuelekeza ukweli kwa Rais na watu waliona kuwa ni kitu ambacho hakikuwahi kufikiriwa.
Hivi majuzi amegongana na Mahakama na kimsingi kampiga mkwara Jaji Mkuu kitu ambacho ninakipinga kabisa.
Chochote anachopanga kufanya, hivi sivyo jinsi ya kwenda kwani it will backfire!