PDA

View Full Version : Hili la Dowans haliishi tu



mwanakijiji
02-23-2009, 05:23 PM
Nguvu za Dowans zaibuka upya

2009-02-23 10:01:37
Na Muhibu Said


Kuna kila dalili kwamba nguvu za kampuni ya Dowans iliyorithi mkataba wa Richmond bado zinasumbua na sasa kamati mbili za Bunge ya Nishati na Madini na ile ya Hesabu za Mashirika ya Umma zinagongana kutokana suala la mitambo ya kampuni hiyo.

Kutokana na uzuri, uimara au upya wa mitambo hiyo, Shirika la Umeme nchini (Tanesco) bado inaililia na inataka kuinunua licha ya maamuzi ya kuachana nayo kutolewa na serikali zaidi ya miezi mitatu sasa.

Hali hii imejitokeza siku mbili tu baada yaTanesco kuibua tena nia yake ya kutaka kuinunua mitambo hiyo yenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 mbele ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.

Wakati Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma ikitaka mwafaka utafutwe kwa kukutanisha wadau wote kwenye suala la ama kununua au la, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, imesisitiza msimamo wake wa kupinga ununuzi huo kwa kuwa ni kinyume cha taratibu.

Akizungumza na Nipashe jana, Mwenyekiti wa Kamati Nishati na Madini, William Shellukindo, ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), alisema mwenye maamuzi ya kununua mitambo hiyo ni serikali kama imeona kuna dharura ya kufanya hivyo.

Hata hivyo, alisema taratibu zilizopo zinataka suala hilo lifikishwe kwanza bungeni ili likajadiliwe na kupata baraka za Bunge.

``Kuna taratibu za kufuata. Anayetakiwa kununua ni serikali kama imeona kuna dharura. Lakini ilete kwanza hoja hiyo bungeni ili ijadiliwe na Bunge,`` alisema Shellukindo.

Alisema ipo pia sheria ya manunuzi inayozuia kununua mitambo chakavu kwa vile hatua hiyo ni ya hatari.

Kutokana na hali hiyo, alisema haoni kuwa ni busara kung?ang?ania kutaka kununua mitambo ya Dowans kabla taratibu zinazohusika hazijafuatwa na kwa kuzingatia pia kwamba, mitambo ya kampuni hiyo haijulikani ilitumika kwa muda gani.

``Tanesco wanadai kuwa Dowans wanalo jenereta jipya. Lakini mitambo yao iliingizwa nchini mwaka 2006 na utekelezaji ulianza Desemba 2007. Sasa hilo jenereta linaweza kuwa jipya? Na hata yale (majenereta) mengine hatujui kama ni mapya,`` alisema.

Alisema inashangaza kuona Tanesco iking`ang`ania kutaka kununua, huku mkononi mwake ikiwa na amri ya mahakama iliyoomba kuzuia kuuzwa kwa mitambo ya Dowans kwa vile inaidai kampuni hiyo.

``Hatuna uhakika Tanesco wanaidai nini Dowans, hilo haliko wazi, tunataka tujue kwanza hilo. Hata hivyo, kama hilo lipo basi si wangekubaliana wabadilishane badala ya kununua,`` alisema Shellukindo.

Kauli hiyo ya Shellukindo imetolewa siku moja baada ya vyombo vya habari jana kuripoti kwamba juzi Tanesco ilifikisha upya dhamira yao katika Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema).

Tanesco iliifikisha dhamira yake hiyo kwenye kamati hiyo miezi miwili baada ya Kamati ya Nishati na Madini inayoongozwa na Shellukindo, kupinga suala hilo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Desemba mwaka jana.

Akizungumza na Nipashe jana, Zitto alisema katika kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam Jumamosi iliyopita, Tanesco walitoa hoja za msingi kuhusu dhamira yake ya kutaka kununua mitambo ya Dowans.

Hata hivyo, alisema waliafikiana wamuombe Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuruhusu kuitisha kikao cha kamati zote mbili (ya Hesabu za Mashirika ya Umma na Nishati na Madini), serikali, Tanesco na Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA) ili wajadili na kufikia mwafaka wa pamoja kuhusu suala la kununua mitambo hiyo ili kuepuka kamati kupingana.

Zitto alisema sababu nyingine ya kamati yake kuomba kibali hicho kwa Spika ni kwa vile Kamati ya Nishati na Madini, haikutoa nafasi ya kukutana na Tanesco ili waeleze kwanini wanataka kununua mitambo hiyo.

``Walikutana tu na Waziri Ngeleja wakapinga Tanesco kununua mtambo huo wa Dowans,`` alisema Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Alisema pia, watatumia fursa ya ruhusu hiyo Spika kujadili kuhusu hatma ya umeme wenye megawati 300 wa Mtwara baada Kampuni ya Barrick kujitoa na hatma ya umeme wa upepo wa Singida.

Alisema kamati yake ilikutana na Tanesco juzi kwa lengo la kukagua hesabu za shirika hilo baada ya kuonekana wanatumia gharama kubwa kulipia umeme na hoja ya kutaka kununua mtambo wa Dowans iliibuka katika kikao hicho.

Hata hivyo, Zitto alisisitiza kwa kusema kuwa: ``Kazi ya Kamati ya Bunge ni ku-oversight (kusimamia) na siyo utendaji wa serikali wa kila siku, kwamba serikali inunue au isinunue.``

Dowans ni mrithi wa kampuni ya Richmond Development Corporation, Kampuni iliyopewa mkataba na serikali wa kuzalisha umeme wa dharura wa megawati 100, lakini ilishindwa na baadaye iligundulika ilikuwa kampuni feki.

Sakata la mkataba wa Richmond ndio ulisababisha kujiuzuku kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, mawaziri Dk Ibrahim Msabaha na Naziri Karamagi. Kutokana na kujiuzulu kwa Lowassa, Baraza lote la Mawaziri lilivunjika Februari mwaka jana.

Tangu wakati huo, kutokana na ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa makataba wa Richmond na maazimio ya Bunge, matukio kadhaa yametokea ikiwa ni pamoja na kumfikisha mmiliki wa Richmond mahakamani.

Aidha viongozi wengine wanachunguzwa na vyombo vya dola juu ya ushiriki wao kwenye mkataba huo.

SOURCE: Nipashe

My Take:
Hili la Dowans lina ugumu gani, kama wanaona bado wanataka kulipwa kwanini tusiamue kununua tu hiyo mitambo yaishe kuliko kuzungushana kama pia?

Ach-F
02-24-2009, 01:07 AM
Mwanakijiji

Tumejaza mijitu mijinga kwenye serikali ya CCM ndio sababu hii shida haiwezi kwisha.

dickabudi
02-24-2009, 11:15 AM
Mwanakijiji, kwa taratibu tuwapate Wahandisi kutoka TANESCO wazungumzie ubora na umadhubuti wa mitambo ya DOWANS, uzuri na uimara wa mitambo hiyo, urefu wa maisha yake na jinsi gani wao kama watalaam wanasemaje na wanaona umuhimu gani kuwa na hiyo mitambo

Pia kutoka kwao tupate aina gani ya mitambo kama hiyo inaweza kuwa mbadala kama hiyo isiponunuliwa

Tuje tuwapate watalaamu wa Manunuzi wathaminishe mitambo hiyo na mitambo mbadala kutoka sehemu nyingine

Tuwapate pia wanasheria watoe mapendekezo ya mkataba wa kuwa na manufaa kwa nchi kupata mitambo ama ya DOWANs kama itakavyoshauriwa na Wahandisi na wataalamu wa manunuzi na kuona lipi lifanyike

Uking'ang'nia Kamati za Bunge utakuwa unarudi palepale kwenye ufisadi kwani si wataalamu wa hizo fani ni blaah blaah watakupa na kusubiri posho za vikao

Tuwasaidie kwa kupata tathimini ya wataalam wa namna hii, naamini kama tunawezapewa barua ya siri ya Wiziri kwenda kwa Waziri Mkuu, hatuwezi shindwa kupata nini wahandisi wa TANESCO na Wataalam wa Manunuzi wanaona kinafaa kwa DOWANS au alternative nyingine, tuwaonyeshe wenzetu UZALENDO ni huu na UFISADI mnaoukumbatia ni upi, kumbuka wabunge walio wengi hata wa upinzani ni wasubiri posho na blaah blaah uzalendo ni mdogo sana

mwanakijiji
02-24-2009, 05:05 PM
Mwanakijiji, kwa taratibu tuwapate Wahandisi kutoka TANESCO wazungumzie ubora na umadhubuti wa mitambo ya DOWANS, uzuri na uimara wa mitambo hiyo, urefu wa maisha yake na jinsi gani wao kama watalaam wanasemaje na wanaona umuhimu gani kuwa na hiyo mitambo

Pia kutoka kwao tupate aina gani ya mitambo kama hiyo inaweza kuwa mbadala kama hiyo isiponunuliwa

Tuje tuwapate watalaamu wa Manunuzi wathaminishe mitambo hiyo na mitambo mbadala kutoka sehemu nyingine

Tuwapate pia wanasheria watoe mapendekezo ya mkataba wa kuwa na manufaa kwa nchi kupata mitambo ama ya DOWANs kama itakavyoshauriwa na Wahandisi na wataalamu wa manunuzi na kuona lipi lifanyike

Uking'ang'nia Kamati za Bunge utakuwa unarudi palepale kwenye ufisadi kwani si wataalamu wa hizo fani ni blaah blaah watakupa na kusubiri posho za vikao

Tuwasaidie kwa kupata tathimini ya wataalam wa namna hii, naamini kama tunawezapewa barua ya siri ya Wiziri kwenda kwa Waziri Mkuu, hatuwezi shindwa kupata nini wahandisi wa TANESCO na Wataalam wa Manunuzi wanaona kinafaa kwa DOWANS au alternative nyingine, tuwaonyeshe wenzetu UZALENDO ni huu na UFISADI mnaoukumbatia ni upi, kumbuka wabunge walio wengi hata wa upinzani ni wasubiri posho na blaah blaah uzalendo ni mdogo sana

hapo unazungumzia common sense.. wenzako hawana common sense. Ukweli ni kuwa at the end of the day hii mitambo ni LAZIMA tuinunue kwa sababu nje ya serikali hakuna mwenye interests nayo na jamaa waliyoileta hawawezi kutengeneza fedha ya kutosha.

Hata kama kuna mitambo mbadala somewhere ambayo inafaa na kwa bei nafuu serikali haitonunua hiyo kwa sababu ya "Dowans tayari ipo".

Sasa usishangae umeme ukianza kukatwa katwa tena hadi watu wasalimu amri. Ndiyo maana mimi nasema tununue tu yaishe kwa sababu najua tutanunua anyway. Kinachoangaliwa kwa kweli ni timing.

Baija Bolobi
02-24-2009, 05:18 PM
Jamani wengine mnapoongea hiyo common sense, inajaribu kuniingia lakini ninapokumbuka mambo mawili napata shida: Kwanza, kwamba mitambo hii ni ya Rostam ikitokea Richmond. Kwamba billioni 60 tumlipe Rostam na bei ya umeme ibaki pale pale. Fedha kaiba BOT, kanunua mitambo, katuuzia, serikali ikavunjwa, WM kafukuzwa, watu mpaka leo wanakulana kama senene, etc. It is too much to pay. Pili, jamani tukubali principle ziwe na gharama kuliko common sense. Bunge limekataa na sheria ya manunuzi haikubali. Kupinda suala hili kutaleta mafuriko mbele ya safari.

Najua mafisadi wametu-conner hapa maana ukiona Dr. Rashid anatetea mitambo hii ujue kuna jambo. Ni huyu Rashid aliyeandika barua ya kujiuzuru pale Lowassa alipomlazimisha awawashie umeme Tanga cement mpaka wakawa hawasalimiani. Leo Dr. Rashidi anatetea tununue mitambo ya Lowassa na Rostam. Afadhali ya kufa na tai shingoni.

dRU
02-24-2009, 06:45 PM
Wajameni, ukisikia mtu kawa zuzu hana mbele wala nyuma basi ujue hapo pana kazi kweli kweli ya kumuokoa mtu kama huyo. Wapo ambao watadiriki kwenda hata kwa akina "toboa tobo" ili mradi pawepo na aina fulani ya kuhangaika ili kunusuru afya na maisha ya mtu ambaye kafikwa na hali kama hii. Vile vile wapo ambao watashangilia na kufurahi kuona mtu huyo anateseka na ikibidi apate mateso zaidi ya hayo maana kwao ni faraja ama kwa namna fulani wanapata mwanya wa kufanya mabaya zaidi ndani ya familia ile, eti kwa kipindi hicho hiyo familia itakuwa imeshikwa zaidi katika kaungalia hali ya mgonjwa wao hivyo hayo mengine hayapewi kipao mbele!!!

Maelezo haya yote yanalenga kuelezea ni jinsi gani sasa nchi yetu ilivyo wingwa na matatizo haya ya ufisadi (ugonjwa) ambao umetufanya watu wote tumetaharuki na kuwa na mshangao tukiuliza nini kitatokea kesho ama nani atakuwa mstari wa mbele katika hii rank ya ufisadi!!!

Tumefika pahala pagumu, kama ikiwa tutashindwa kwa nguvu za pamoja basi hata kwa nguvu binsafi inabidi tupigane.. hatudendewi haki hapa kwa nini lakini tunakaa kimya na kuendelea kulalalama tu na hawa wajinga wajinga ambao kila siku wanatafuta njia ya kutufanya sisi kuwa na ma-mbumbumbu!!! na wao werevu!! Wengi wao katika madaraka (Kisiasa) kama si kura za wizi hawa wasingepita popote, na chimbuko la lote ni hapo hapo kwenye kura hizo za kijanja janja.. hawa wamelemaa kwa hongo na ndiyo njia pekee wanayoijua ili kuzidi kuwepo walipo

Mpita Njia
02-25-2009, 01:34 PM
Mwanakijiji, kwa taratibu tuwapate Wahandisi kutoka TANESCO wazungumzie ubora na umadhubuti wa mitambo ya DOWANS, uzuri na uimara wa mitambo hiyo, urefu wa maisha yake na jinsi gani wao kama watalaam wanasemaje na wanaona umuhimu gani kuwa na hiyo mitambo

Pia kutoka kwao tupate aina gani ya mitambo kama hiyo inaweza kuwa mbadala kama hiyo isiponunuliwa

Tuje tuwapate watalaamu wa Manunuzi wathaminishe mitambo hiyo na mitambo mbadala kutoka sehemu nyingine

Tuwapate pia wanasheria watoe mapendekezo ya mkataba wa kuwa na manufaa kwa nchi kupata mitambo ama ya DOWANs kama itakavyoshauriwa na Wahandisi na wataalamu wa manunuzi na kuona lipi lifanyike

Uking'ang'nia Kamati za Bunge utakuwa unarudi palepale kwenye ufisadi kwani si wataalamu wa hizo fani ni blaah blaah watakupa na kusubiri posho za vikao

Tuwasaidie kwa kupata tathimini ya wataalam wa namna hii, naamini kama tunawezapewa barua ya siri ya Wiziri kwenda kwa Waziri Mkuu, hatuwezi shindwa kupata nini wahandisi wa TANESCO na Wataalam wa Manunuzi wanaona kinafaa kwa DOWANS au alternative nyingine, tuwaonyeshe wenzetu UZALENDO ni huu na UFISADI mnaoukumbatia ni upi, kumbuka wabunge walio wengi hata wa upinzani ni wasubiri posho na blaah blaah uzalendo ni mdogo sana

Tatizo ni kuwa wengi tunaamini kuwa ununuzi wa mitambo hii hauzingatii vigezo ambavyo umevichambua. TUnaamini kuwa hili ni la akina Rostam na Lowassa la kuona kuwa mitambo ambayo waliitumia kuiingiza nchi mkenge through Richmond, sasa wataka kuhakikisha wanaiuza na kupata faida waliyokatizwa kuipata katika dili la awali.
nadhani kwenye kamati ya Mwakyembe kuna kipengele kinachoeleza kwua iwapo serikali, au tanmesco for that matter, inataka kununua mitambo kama hiyo, inaweza kuipata kutoka Marekani (wamelekeza na kiwandani inakotengenezwa) at a far lower price than what was quoted na jamaa wa Richmond.
Lakini, kabla Tanesco hawajapersue alternative hiyo, wanakuja na hoja ya kulazimisha kwua ni lazima tununue mitambo hiyo sasa kwa sababu hali ya umeme ni mbaya kama kwamba hilo ni suala lililojitokeza ghafla.
Katika hoja hiyo, Tanesco wananithibitishia kuwa hawana mipango madhubuti kiasi kwamba hawajuo hata projections za uzalishaji wa umeme katika nchi zikoje-ni watu hatari sana hawa