PDA

View Full Version : Huyu ndiye Masha?



mwanakijiji
03-02-2009, 07:28 PM
Sema Usikike - Mwandishi Maalum

Kama tungekuwa tunatafuta mzungumzaji wa Kiingereza sanifu chenye lafudhi ya Kimarekani, hapana shaka, Lawrence Kego Masha, ndiye mtu safi kwa nafasi hii, kwani katika vitu ambavyo anaviweza hiki kikubwa zaidi anachojivunia.

Lakini kwa bahati mbaya sana, watu wengi hasa wakaazi wa Nyamagana mkoani Mwanza na Watanzania walio wengi hawamjui vizuri Masha Mbunge na Waziri wa Mambo ya Ndani ni mtu wa namna gani.

Namfahamu Masha tangu akiwa kinda Marekani, baadaye Chuo Kikuu Dar-es-Saalam na hatimaye jijini mwanza alipojiunga na siasa, lakini nilikitaa kumuunga mkono pamoja na kuwa ni ndugu wa karibu, kwa sababu namfahamu udhaifu wake kuliko anavyojijua yeye.

Naandika makala haya sina chuki wala kinyongo naye lakini nimesukumwa na kauli zake za hivi karibuni kuhusu albino, sakata la Reginald Mengi, Deep Green na Vitambulisho vya uraia.

Tatizo kubwa la Masha ni kiburi na jeuri ambavyo kwake anadhani ni ujasiri na utendaji kazi mzuri ambao eti hata rais anaufahamu. Sijui huenda akawa sahihi lakini kwangu ni ubatili mtupu.

Masha ana sura mbili. Sura ya kwanza hujitokeza kama mzalendo wa kweli aliyeacha Marekani na na kurudi kutumikia nchi yake kwa sababu anaguswa na matatizo ya nchi yake. Anasema ameacha hata kazi yake ya mamilioni na kuingia katika siasa ili kutumia Watanzania. Ubatili mtupu.

Sura ya pili ni Masha amba ana uchu wa madraka na ndoto zinazoelea angani. Anataka mali kwa kasi sana bila kujali hizo mali zimepatikana kwa njia gani lakini ili mradi ni mwanashera basi kila alichonacho kakipata toka IMMMA Advocates.

Kaingia CCM juzi, kaukwaa ubunge, unaibu waziri na baadaye uwaziri, ghafla akagundua mteremko hapa, akaanza kuangalia mbali kama isemavyo kauli mbiu ya shule ya Sekndari Nsumba0Lenga mbali naye akaanza kuwaza Uwaziri Mkuu 2015 na baadaye Urais kama Mungu akipenda.

Lakini mimi ninayemfahamu, tangu anakutana na mkewe kule Marekani, ninapata taabu sana kuamini kama Masha amepata wapi jeuri aliyo nayo kiasi cha kutaka wengine wafilisiwe eti wanaiandika vibaya serikali. Sijui jeuri ya kuwaambia wazee wenye umri sawa na baba yake kwamba hawana akili na atawashughulikia ipasavyo. Lakini yote hii chanzo chake ni kiburi.

Kama hayati Nyerere angekuwa na kiburi kama cha Masha, basi baba yaeke Ddr. Fortunatus Masha angefia kizuizini, lakini kwa busara alimuokoa na hata kumwambia akimbie nje ya nchi ? ushahidi upo.

Akakaa uhamishoni Marekani na akawazaa akina Masha ambao leo wanataka wale wanaodhani wanahitilafiana kimawazo wafilisiwe au wafikishe vielelezo kwake ndani ya siku saba. Ninapata taabu sana kuamini uwezo wa kuchanganua mambo wa Waziri Mashaa kutokana na kauli zake tata na zilizojaa kiburi. Mathalani, Masha huyu huyu alisema mauaji ya albino ni tatizo dogo tu linalokuzwa na vyombo vya habari, lakini leo hii Waziri mkuu katoa chozi Bungeni, na Rais kasitisha zira Mbeya kuja kupokea maandamano ya kupinga mauaji ya albino. Huyu bado yupo Wizarani anahangaiaka na vitambulisho.

Lakini masha huyu huyu alikuja Mwanza hapa mwaja jana akaulizwa kwenye mkutano wa hadhara kuhusu anachokifahamu juu ya Kampuni ya Kifisadi ya Deep Green Finance Ltd iliyochota shilingi bilioni 10 toka Benki Kuu ya Tanzania na kisha kufunga virago. Akasimama, akanena ?tuliambiwa na serikali kusajili na kuifunga Deep Green Ltd.. ndiyo ninaifahamu sana?. Tafisi yakinifu ni kwamba serikali ndiyo iliyowatuma akina Masha na IMMMA Advocate kusajili na kisha kufunga kampuni ya kifisadi ya Deep Green. Huu ni ubatili mtupu!

Lakini Masha akaenda mbali zaidi akampa Bw. Mengi siku saba awasilishe ushahidi ofisini kwake juu ya madai yake dhidi ya serikali la sivyo atamshughulikia. Hivi tujiulize , ushahidi uwa unapelekwa mahakamani au ofisini kwa WAziri wa mambo ya Ndani? Mwanasheria kama Masha hajui ushahidi huwa unawasilishwa kortini? Ubatili mtupu.

Kana kwamba haitoshi juzi katoka Dodoma akawaambia waandishi wa habari kwamba hajawahi kukutana na kampuni ya SAGEM aliyojaribu kuitetea wala wakala wao. Ningekuwa mwana habari siku hiyo ningemuuliza alijuaje uwezo wake kiutendaji wa kampuni hiyo? Aliwezaje kuitetea kwa nguvu zote mpaka kuandika waraka wa siri kwa Waziri mkuu? Ubatili mtupu.

Lakini kesho yake tena akaendelea na kampuni yake katika radio moja jijini , sijui alialikwa au alijipeleka, na akasema amewahi kukutana n wawakilishi wa Kampuni ya SAGEM lakini siyo nje ya nchi. Sasa ndani ya saa 24Waziri masha anatoa kauli mbili zinazokinzana, lakini kwangu sikushangaa kwa sababu , huyu ndiye Masha ninayemfahamu.

Kule Mwanza akiwa waziri aliwahi kumtukana hadharani Diwani mmoja wa Chama cha Mapinduzi amatusi ambayo hayaandikiki, na akitaka ushahidi atapewa. Bahatti mbaya diwani huyo naye ni kiboko ikambidi Masha akaungama chini ya ulinzi mkaali.

Hakuishia hapo, Masha aliwahi kukunja ngumi hadharani ili apigane na mhariri na mmiliki wa Gazeli la Mzawa James Nhende, katika hoteli ya New Mwanza Hotel. Akatamka hadharani kwamba ana uwezo wa kumpiga na kuml,ipa gharama zote lakini Mungu aliepusha shari.

Waziri wetu, mwanasheria, na mbunge wetu anataka kupigana hadharani kisa kaandikwa vibaya na gazeti la Mzwa. Ubatili mtupu.

Masha katika kipindi kifupi alichokaa madarakani amejenga maadui wengi ndani na nje ya chama, kiasi cha kumchanganya akili, sasa badala ya kuwapa wauaji wa albino siku saba anawapa akina Mzee Mengi.

Masha huyu anatakiwa akamatwe na kushitakiwa kwa kosa la jinai kwani ushahidi upo wa wazi kabisa kwamba mwaka 2000 Oktoba aliwatishia polisi kwa basota yake sambamba na kuwatolea lugha chafu na kashfa juu.

Nanukuu hukumu ya Mahakama Kuu Mwanza, ?nyinyi polisi ni vibaraka wa CCM, wapumbavu, hamtumii akili, kama silaha sisi tunazo?. Sasa kama Davidi Blunkett Waziri wa Mambo ya Ndani (wa Uingereza) alilazimika kujiuzulu mwaka 2006 kwa kosa la kuajiri yaya ambaye alikuwa mhamiaji haramu miaka kumi iliyopita tena bila kujua, leo Masha anajisikiaje kuongoza polisi aliowaita wapumbavu na vibaraka wa CCM? Ubatili mtupu!

Leo, huyu mtu anajitokea kupiga kelelkwa jeuri na kiburi, lakini nina uhakika kuna siku Watanzania watamfahamu, kwani hata kule Nyamgana, leo hiini hati hati na uwezo wa kushinda tena ni asilimia 50. Sababu, jeuri na kiburi. Bahati mbaya sana, Mwanza waliwahi kumkataa Marehemu Bomani na fedha zake na u maarufu aliokuwa nao wakamchagua mwalimu wa sekondari, kaka yangu Paschal Mabiti.

Kama kura za maoni zikipigwa leo, Masha anayejiptapa kwamba hata akiwa wa tatu jina lake lake litarudi, nina shaka sana kama atashinda tena. Na kibaya zaidi ameshaanza kulalamika kwambakuna watu wanatumwa kumuangusha.

Bw. James Nhende, leo ni shujaa si kwa sababu tajiri au mwandishi wa habari, lakini kwa kukataa mapema kabisa kumuunga mkono Masha, akisema ana kiburi na jeuri ya hali ya juu. Alitumiwa wajumbe wa kila namna na zawadi juu akakataa kugeuka nyuma.

Nilikuwa Marekani nikasikia taarifa hizi, nikajua kumbe tunaomjua Masha tuko kadhaa, lakini wengi hawakuelewa, lakini kila kukicha anazidi kujipambanua, na kufanya Watanzania wamjue ni mtu wa aina gani.

Kwa sababu ameota kama uyoga ndani ya chama na hasa katika siasa anguko lake litakuwa ghafla kwa sababu hakujijenga katika misingi imara ya kulea viongozi wetu wa miaka ijayo. Aliomba ubunge akapewa, akalilia uwaziri akapata, ghafla anataka uwaziri mkuu 2015, na siku Edward Lowassa alipojiuzul uwaziri Mkuu miongoni mwa watu walioumia sana ni pamoja na Masha.

Hakuumia eti kwa sababu ni marafiki, hapana, alidhani ndoto yake kisiasa imekufa, na alisikika akisema maneno makali sana dhidi ya viongozi wakuu serikalini, nilikuwepo pale Dodoma hoteli, nikamsikia lakini bahati nzuri sana JK akazidi kumuinua.

Leo amevaa vita ya Lowassa bila kujua akidhani atalipiza kisasi, lakini anasahau kwamba ni mchanga kisiasa ambaye hakusomea hata uanachama wa chama tawala.

Wiki ijayo nitaeleza Masha alivyopata utajiri wa haraka haraka katika kipindi kifupi.

dickabudi
03-03-2009, 11:34 AM
Mwanakijiji

1. Reference za Nhende ziondoe wapo wanaomfahamu kupita unavyotaka kusema. UHURU NA MZALENDO,MFANYAKAZI, MSANII AFRIKA na MZAWA

2. Kuna radio inaanzishwa Mwanza chini ya Naibu Waziri kijana kummaliza Masha, hizo ndizo siasa za kanda ya ziwa

3.Usije ikiwa unapewa hizo information na hilo group au na wewe upo katika hilo group la kummaliza Masha kwa manufaa ya Naibu Waziri huyo asiyetoka kanda ya ziwa lakini nae ni maarufu kwa majungu

4.Tuwe realistic tusitumiwe kwa manufaa ya watu nasi tutaingia kwenye kundi la mafisadi kwani tutapandikiza chuki ambazo si mimi wala wewe tunaonufaika nazo

5.Nape Mosses Nnaiye ni mmoja wanalijua joto la majungu

6.Tuwagroom hawa vijana, tuwarekebishe pale wanapokosea, tuwaache waonyeshe vipaji vya uongozi tusijiingize katika siasa za kukomoana, Taifa halitaenda

mwanakijiji
03-03-2009, 04:58 PM
Mwanakijiji

1. Reference za Nhende ziondoe wapo wanaomfahamu kupita unavyotaka kusema. UHURU NA MZALENDO,MFANYAKAZI, MSANII AFRIKA na MZAWA

2. Kuna radio inaanzishwa Mwanza chini ya Naibu Waziri kijana kummaliza Masha, hizo ndizo siasa za kanda ya ziwa

3.Usije ikiwa unapewa hizo information na hilo group au na wewe upo katika hilo group la kummaliza Masha kwa manufaa ya Naibu Waziri huyo asiyetoka kanda ya ziwa lakini nae ni maarufu kwa majungu

4.Tuwe realistic tusitumiwe kwa manufaa ya watu nasi tutaingia kwenye kundi la mafisadi kwani tutapandikiza chuki ambazo si mimi wala wewe tunaonufaika nazo

5.Nape Mosses Nnaiye ni mmoja wanalijua joto la majungu

6.Tuwagroom hawa vijana, tuwarekebishe pale wanapokosea, tuwaache waonyeshe vipaji vya uongozi tusijiingize katika siasa za kukomoana, Taifa halitaenda

dickabudi.. uzuri wa hapa ni kuwa kama mtu ana info za Masha au kuonesha habari hizi si za ukweli au ni majungu tunakaribisha malumbano hayo hapa. Hoja zote zinakaribishwa.

dickabudi
03-04-2009, 02:21 PM
Mwanakijiji ziangalie vizuri hizo dondoo ni hoja kwani vijiwe vya Mwanza Institute, Kuleana na Mwanza Hotel vinafahamika

Mzee Ally, Mbando na Mzee Nhende wanaeleweka katika vijiwe hivyo ndo maana nachelea kuunganisha taarifa zako naza vijiwe hivyo, Ridhwan Kikwete akiwa mshiriki wa hivyo vijiwe anapokuwa Mwanza

Ach-F
05-17-2009, 06:22 PM
How a deported `EPA mogul` enjoys Dar`s life



http://www.ippmedia.com/media/picture/large/Masha1.jpg
Masha: It`s the government that allowed him to stay in the country.
Je, serikali ni nani? We said Tanzania does not deserve Masha to hold his position ??. ??..




His dodgy deals cost the government $100million in 1994, but he is today walking and living freely in Dar es Salaam despite the Parliamentary recommendations that he should be arrested and prosecuted immediately. The man who in 1994 set up and then stole from the debt buy-back programme that is now known as the External Payment Arrears (EPA) account has been living in the country for the last five years despite being declared a prohibited immigrant.
Vidyadhar G. Chavda, an Indian citizen, first came to Tanzania in 1978 without a penny to his name, according to his own words quoted in a 1994 parliamentary report, but after years of working here as an architect he moved into the finance services industry and orchestrated a number of very lucrative, very shoddy deals. Chavda approached the government with his idea for the creation of the Debt Conversion Programme (DCP) - which sought to reduce the country?s outstanding debts by selling them off to third parties at discounted prices - the deal that cost the country Sh50bn/- ($100m at that time prevailing exchange rate) in taxpayer money from the programme.

?I came to this country without a single penny, a beggar?but I came with a brain worth millions of dollars supported by education and exposure,? Chavda said after the news of his multibillion-shilling scandal broke in 1994. ?The DCP funds were brought totally by my idea and efforts,? he said at the time. ?What I have done is beyond the sphere of understanding Parliament?it is a purely financial issue which nobody is capable of grasping.?

To repair the economic damage caused by his sleazy deals, the Central Bank of Tanzania (BoT) was forced to print billions of shillings in 1994. After his scandal was thoroughly investigated by the Parliamentary Committee chaired by Edward Oyombe Ayila, Chavda was finally deported in 1996, though he was not charged with any wrongdoing. Despite being deported, Chavda had already caused a strong political rift within the ruling party, and then-minister for home affairs Augustine Mrema resigned because he disagreed with the way the scandal was handled.
In its recommendations, the Parliamentary Committee advised Chavda?s immediate arrest and prosecution for fraud, violation of the Foreign Exchange Act of 1992 and giving false statements contrary to section 122, 309 and 346 of the country?s penal code. The Committee further recommended that legal action be taken against all traders and lawyers who conspired with Chavda for economic sabotage, and it urged the concerned authorities to cancel the business licenses for those who collaborated with him, including Subhash Patel.

Surprisingly only one recommendation was implemented - to revoke Chavda?s residence permit and deport him - essentially letting him and his partner off the hook. He is now back in Tanzania where he has been living in the Masaki suburb of Dar es Salaam for the last five years, according to reliable details obtained by The Guardian on Sunday this week.

How he played the game

Having managed to shake the Parliamentary Committee that was formed to investigate him, Chavda carefully planned his comeback in 1997 just three years after he was deported. On March 18, 1997, Chavda, acting through his lawyers Mkono & Company, asked the High Court of Tanzania to issue a witness Summons to allow him to testify on August 5 of that year in a pending civil case brought by his wife against him, Civil Case No 130 of 1993.

His wife, an Indian citizen who had continued living in Tanzania legally after Chavda was deported, was suing him over a family financial dispute. On April 1, 1997, the High Court wrote to the Director of Immigration seeking clarification on the legal position of Chavda?s status once he arrived in the country to testify. As such, the Director of Immigration informed Mkono & Company on September 25, 1997, that Chavda had been given a visa for 30 days to allow him to enter the country only to testify in court. Later findings from the court show, however, that during that 30-day period, the civil case was not scheduled for a hearing and Chavda?s claims that he needed to appear in court lacked grounds. His visa expired and he left the country, but with the intention to come back yet again.

Having identified a loophole in the system that could be exploited, Chavda planned a comeback in January 2002 centred on another ?necessary? appearance in court. Chavda again had his lawyers - this time from the firm Gomba & Tadayo - write to the High Court requesting a Witness Summons to testify in Civil Case No 74 of 1996, a separate civil case filed by the National Bank of Commerce against him for an alleged 800m/- in outstanding loan repayments. He was again allowed to enter the country after being given Entry Visa No 0000695 dated March 4, 2002.

Chavda should have left within 28 days of the visa?s issuance, but he had stayed almost a year until the Director of Immigration caught on and ordered him to leave the country immediately.
According to details in our possession, Chavda then filed Miscellaneous Civil Case No 60 of 2003 asking the court to force the immigration department to grant him a visa so that he could testify in the two civil cases facing him. On March 11, 2004, the High Court issued its ruling in Chavda?s favour, ordering the Director of Immigration to issue a two-year visa to the deportee. One senior immigration official in Dar es Salaam told The Guardian on Sunday this week that the decision to grant Chavda the visa was both illogical and indefensible. ?The law is very clear; he should be outside the country and is only allowed to come once needed or summoned by the court,? said the official, who asked for anonymity on the grounds that he is not the department?s official spokesperson.

?A hearing can?t take two years, it is just one or a few weeks as long as the pending cases are civil cases.? Chavda?s two-year visa expired in April 2006, but again neither of the two cases had been heard, and not even preliminary hearings had been held for either of them.

Following of the expiry of his visa, the office of the Attorney General wrote a letter on May 6, 2006, directing the Director of Immigration to act accordingly. ?Since the ruling date was March 11, 2004 then the time for stay in Tanzania has elapsed, and given the fact that Chavda didn?t appeal against the decision, now act according to the law on this issue,? reads part of the letter signed by D.L Chidowu on behalf of the AG.

Despite the AG?s letter, the immigration department has still not taken any action against Chavda. In a May 25, 2007, letter to Professor Abdullah Safari of Safari Law Chambers - Chavda?s newest lawyer - the AG?s office wrote that it seemed the ministry of home affairs had flipped its position on the matter and was complicit in allowing Chavda to remain in the country.
?The issue of Chavda has taxed much this office. We as advocates of the government and chief legal advisers did our best to defend the position of the government in court to declare Chavda a prohibited immigrant?however it is now clear that the parent ministry [home affairs] has changed its previous position,? reads part of the letter signed by P. J Ngwembe on behalf of the AG. When asked on Friday why Chavda was still being allowed to remain in Tanzania, Minister for Home Affairs Lawrence Masha was deliberately vague.

?It?s the government that has decided that he should stay in the country because he is still needed,? Masha told The Guardian on Sunday. The minister would not elaborate on why Chavda was ?needed? in the country when he was no longer involved in any currently pending civil cases.
The minister?s response is a curious departure from what his boss, Prime Minister Mizengo Pinda, told Parliament on April 30 this year, in response to a question asked by Kigoma North MP Zitto Kabwe.

The Prime Minister said he wasn?t aware whether Chavda was still in the country, but he promised to thoroughly investigate on which grounds the Asian tycoon was allowed to stay in Tanzania if he were.

The senior immigration official said this ?confusion? among top-ranking government officials speaks to the deliberate obfuscation and questionable protection surrounding Chavda and his status in the country. ?This is a man who was supposed to be arrested and charged with criminal offences but surprisingly he is today a free man enjoying the protection of some government officials and a group of Asian traders,? the senior immigration official said.

Kwa nini hawafukuzwi waliomuingiza? Pengine ya BOT ni uongo?

QUTE
05-20-2009, 12:21 AM
Mwanakijiji

1. Reference za Nhende ziondoe wapo wanaomfahamu kupita unavyotaka kusema. UHURU NA MZALENDO,MFANYAKAZI, MSANII AFRIKA na MZAWA

2. Kuna radio inaanzishwa Mwanza chini ya Naibu Waziri kijana kummaliza Masha, hizo ndizo siasa za kanda ya ziwa

3.Usije ikiwa unapewa hizo information na hilo group au na wewe upo katika hilo group la kummaliza Masha kwa manufaa ya Naibu Waziri huyo asiyetoka kanda ya ziwa lakini nae ni maarufu kwa majungu

4.Tuwe realistic tusitumiwe kwa manufaa ya watu nasi tutaingia kwenye kundi la mafisadi kwani tutapandikiza chuki ambazo si mimi wala wewe tunaonufaika nazo

5.Nape Mosses Nnaiye ni mmoja wanalijua joto la majungu

6.Tuwagroom hawa vijana, tuwarekebishe pale wanapokosea, tuwaache waonyeshe vipaji vya uongozi tusijiingize katika siasa za kukomoana, Taifa halitaenda

Napata wasiwasi kama wewe sio mfuasi wa Masha. aondoe kwa sababu gani? hii habari imetoka kwenye gazeti la sema usikike ni gazeti linasomwa na watu wengi pia kama na wewe unazo habari za Nhende zimwage tuzijue halafu tutachuja pumba na mchele. kumpigia debe masha kwa kututisha haitoshi