mwanakijiji
03-19-2009, 05:09 PM
Kuna mpasuko ndani ya CCM, kuna mgongano ndani ya chama tawala, mgongano ambao sasa unaanza kuonekana hadharani tena bila ukungu wowote. Kuna kambi kubwa tatu zinazoshindana na kutafutana kisasi.
a. Kambi ya Lowassa
Kambi hii ni kambi ambayo imejeruhiwa, kutupwa nje ya madaraka na kubebeshwa lawama za ufisadi. Ndani ya kambi hii wapo wanasiasa mashuhuri na wafanyabiashara wakubwa. Yumo Edward Lowassa, Andrew Chenge, Nazir Karamagi, Rostam Aziz, Msabaha, na wengine ambao wanaamini kuwa kujiuzulu kwa Lowassa kulikuwa ni kutokana na uonevu mkubwa.
Kambi hii ina kinyongo na CCM chama tawala kwa jinsi walivyoshughulikia suala la Richmond na hasa kwa kushindwa kukaa na kupanga mkakati wa kujibu hoja za Kamati Teule ya Bunge na hatimaye kuzuia Lowassa asing'oke. Inaamini njama au mchezo ulichezwa ili kumwaibisha Waziri Mkuu na kuhakikisha asingeweza kuendelea na majukumu yake chini ya wingu la kuhusishwa na ufisadi.
Hata hivyo hasira zao kwa kiasi kikubwa ziko dhidi ya Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais wa Tanzania Bw. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kushindwa kusimama na Waziri wake Mkuu wakati ule. Waliona kuwa kwa mtu ambaye alifanya mengi, na alikubali kubeba mzigo mkubwa wa kuhakikisha Kikwete anaingia madarakani the least thing Kikwete angeweza kufanya ni kusema ana imani na Waziri wake Mkuu na kuja kuwa mtetezi wake. Kwa hilo hawajamsamehe Kikwete.
Kambi hii haina mvuto au ushabiki mkubwa kwa wananchi wa kawaida. Haijasimama kukemea ufisadi, haijajitokeza kuonesha kuwa inachukizwa na yaliyotokea Benki Kuu, au kuonesha kwa namna yoyote ile inajali maslahi ya Taifa. Haijafanya hivyo na inaonekana haiwezi kufanya hivyo bila kuonekana ina unafiki.
b. Kambi ya Sitta
Kambi ingeweza pia kuitwa ya kina "mwakyembe" lakini ni wazi ni kambi ambayo kiongozi wa juu aliyemo ni Spika Sitta. Kambi hii inaamini kuwa Sitta angekuwa Waziri Mkuu lakini mchezo ulichezwa kumnyima nafasi hiyo. Lakini kambi hii haikuwa na nguvu mwanzoni hadi pale yalipotokea masuala ya kifisadi yaliyohusisha watu waliomo kwenye kambi ya kwanza. Kwao ilikuwa ni nafasi ya kuua ndege wawili kwa jiwe moja.
Wangeweza kuwashambulia wale inaoamini ni vinara wa vitendo vya ufisadi (baadhi wamo kwenye kambi ya kwanza) na wakati huo huo kujijenga mbele ya jamii na kuonekana ni watetezi wa maslahi ya nchi. Miongoni mwa mashabiki wake ni Mwakyemba, Kumba, Selelii, mama Malecela na wale viongozi wa upinzani Bungeni.
Kambi hii imejipatia umaarufu mkubwa kwa wananchi kwani licha ya baadhi ya wajumbe wake kuwa na historia kama za watu wa kambi ya kwanza, lakini wameweza kujitokeza bila haya na kuanza kutetea maslahi ya nchi huku wakiamini wako katika mapambano dhidi ya mafisadi.
Kambi Maslahi
Kambi hii ya tatu naamini ndiyo kubwa sana Bungeni na kwenye CCM Ni kambi ambayo wajumbe wake wengi wanafuata maslahi tu ya nani mwenye nguvu jiunge naye. Kambi hii iko tayari kusimama na kina Lowassa endapo kwa kufanya hivyo maslahi yao yatalindwa na wako tayari kuwa na kina Sitta endapo kwa kufanya hivyo kutafanya maslahi yao kuwa salama. Kambi hii imeundwa na wabunge wengi walio kimya ambao hawataki kuonekana wamechagua upande.
Ni kambi ambayo tunaweza kusema iko pragmatic. Ni kambi ambayo ina wazee wakongwe ambao wanaangalia kinachoendelea na wengine wanawacheka wale waliompigia debe Kikwete (japo pembeni) wakiamini kuwa walishaurri na kutaka Kikwete asipewe nafasi ya Urais lakini hawakusikilizwa. Hawa ni viongozi ambao wanaamini Tanzania inavuna matunda ya ilichopanda kwa kufuata siasa za sifa na sura.
Kambi hii inaongozwa na wakongwe kina mzee Malecela, Kingunge na wengine. Hawa ni "Wazee wa Chama" ambao wamekuwa hawasikilizwa na kupewa shavu baridi la kusikilizwa zaidi ya kuheshimiwa tuu hadharani. Wengi wa kambi hii hawarudi tena 2010 na sasa wameanza kuandaa watoto wao au warithi wa viti vyao ili kuhakikisha kuwa viti vyao au nafasi zao zinabakia karibu na familia. Kambi hii inaamua kuondoka katika siasa za Tanzania kwa namna hiyo kwa sababu wanaamini zimefikia pabaya na sasa wamechoka mikikimikiki hii ya kisiasa.
Kikwete njia panda
Aliyeko njia panda kwenye haya yote ni Rais Kikwete. Alihusiana na kuwekwa madarakani na kundi la kambi ya kwanza, lakini kazi yake kubwa ya kupambana na ufisadi inatokana na nguvu ya kundi la pili. Hawezi kuwakana walioko kundi la kwanza bila kuonekana msaliti na zaidi ya yote kwa sababu wale waliokundi la kwanza ndio wanajua mambo yake yote machafu tangu akiwa Waziri wa Nishati. NI wao wanajua nani alimsaidia kuingia madarakani na kwa namna gani.
Hawezi kwenda kinyume na wale wenye nguvu ya kambi ya pili kwani hawa ndiyo wanapendwa na wananchi. Kama anataka kuwa katika nafasi ya kushika tena madaraka 2010 hana budi kuwa popular.
Sasa amebakia kuhangaika na kulalamika pembeni.... Afanye nini?
a. Kambi ya Lowassa
Kambi hii ni kambi ambayo imejeruhiwa, kutupwa nje ya madaraka na kubebeshwa lawama za ufisadi. Ndani ya kambi hii wapo wanasiasa mashuhuri na wafanyabiashara wakubwa. Yumo Edward Lowassa, Andrew Chenge, Nazir Karamagi, Rostam Aziz, Msabaha, na wengine ambao wanaamini kuwa kujiuzulu kwa Lowassa kulikuwa ni kutokana na uonevu mkubwa.
Kambi hii ina kinyongo na CCM chama tawala kwa jinsi walivyoshughulikia suala la Richmond na hasa kwa kushindwa kukaa na kupanga mkakati wa kujibu hoja za Kamati Teule ya Bunge na hatimaye kuzuia Lowassa asing'oke. Inaamini njama au mchezo ulichezwa ili kumwaibisha Waziri Mkuu na kuhakikisha asingeweza kuendelea na majukumu yake chini ya wingu la kuhusishwa na ufisadi.
Hata hivyo hasira zao kwa kiasi kikubwa ziko dhidi ya Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais wa Tanzania Bw. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kushindwa kusimama na Waziri wake Mkuu wakati ule. Waliona kuwa kwa mtu ambaye alifanya mengi, na alikubali kubeba mzigo mkubwa wa kuhakikisha Kikwete anaingia madarakani the least thing Kikwete angeweza kufanya ni kusema ana imani na Waziri wake Mkuu na kuja kuwa mtetezi wake. Kwa hilo hawajamsamehe Kikwete.
Kambi hii haina mvuto au ushabiki mkubwa kwa wananchi wa kawaida. Haijasimama kukemea ufisadi, haijajitokeza kuonesha kuwa inachukizwa na yaliyotokea Benki Kuu, au kuonesha kwa namna yoyote ile inajali maslahi ya Taifa. Haijafanya hivyo na inaonekana haiwezi kufanya hivyo bila kuonekana ina unafiki.
b. Kambi ya Sitta
Kambi ingeweza pia kuitwa ya kina "mwakyembe" lakini ni wazi ni kambi ambayo kiongozi wa juu aliyemo ni Spika Sitta. Kambi hii inaamini kuwa Sitta angekuwa Waziri Mkuu lakini mchezo ulichezwa kumnyima nafasi hiyo. Lakini kambi hii haikuwa na nguvu mwanzoni hadi pale yalipotokea masuala ya kifisadi yaliyohusisha watu waliomo kwenye kambi ya kwanza. Kwao ilikuwa ni nafasi ya kuua ndege wawili kwa jiwe moja.
Wangeweza kuwashambulia wale inaoamini ni vinara wa vitendo vya ufisadi (baadhi wamo kwenye kambi ya kwanza) na wakati huo huo kujijenga mbele ya jamii na kuonekana ni watetezi wa maslahi ya nchi. Miongoni mwa mashabiki wake ni Mwakyemba, Kumba, Selelii, mama Malecela na wale viongozi wa upinzani Bungeni.
Kambi hii imejipatia umaarufu mkubwa kwa wananchi kwani licha ya baadhi ya wajumbe wake kuwa na historia kama za watu wa kambi ya kwanza, lakini wameweza kujitokeza bila haya na kuanza kutetea maslahi ya nchi huku wakiamini wako katika mapambano dhidi ya mafisadi.
Kambi Maslahi
Kambi hii ya tatu naamini ndiyo kubwa sana Bungeni na kwenye CCM Ni kambi ambayo wajumbe wake wengi wanafuata maslahi tu ya nani mwenye nguvu jiunge naye. Kambi hii iko tayari kusimama na kina Lowassa endapo kwa kufanya hivyo maslahi yao yatalindwa na wako tayari kuwa na kina Sitta endapo kwa kufanya hivyo kutafanya maslahi yao kuwa salama. Kambi hii imeundwa na wabunge wengi walio kimya ambao hawataki kuonekana wamechagua upande.
Ni kambi ambayo tunaweza kusema iko pragmatic. Ni kambi ambayo ina wazee wakongwe ambao wanaangalia kinachoendelea na wengine wanawacheka wale waliompigia debe Kikwete (japo pembeni) wakiamini kuwa walishaurri na kutaka Kikwete asipewe nafasi ya Urais lakini hawakusikilizwa. Hawa ni viongozi ambao wanaamini Tanzania inavuna matunda ya ilichopanda kwa kufuata siasa za sifa na sura.
Kambi hii inaongozwa na wakongwe kina mzee Malecela, Kingunge na wengine. Hawa ni "Wazee wa Chama" ambao wamekuwa hawasikilizwa na kupewa shavu baridi la kusikilizwa zaidi ya kuheshimiwa tuu hadharani. Wengi wa kambi hii hawarudi tena 2010 na sasa wameanza kuandaa watoto wao au warithi wa viti vyao ili kuhakikisha kuwa viti vyao au nafasi zao zinabakia karibu na familia. Kambi hii inaamua kuondoka katika siasa za Tanzania kwa namna hiyo kwa sababu wanaamini zimefikia pabaya na sasa wamechoka mikikimikiki hii ya kisiasa.
Kikwete njia panda
Aliyeko njia panda kwenye haya yote ni Rais Kikwete. Alihusiana na kuwekwa madarakani na kundi la kambi ya kwanza, lakini kazi yake kubwa ya kupambana na ufisadi inatokana na nguvu ya kundi la pili. Hawezi kuwakana walioko kundi la kwanza bila kuonekana msaliti na zaidi ya yote kwa sababu wale waliokundi la kwanza ndio wanajua mambo yake yote machafu tangu akiwa Waziri wa Nishati. NI wao wanajua nani alimsaidia kuingia madarakani na kwa namna gani.
Hawezi kwenda kinyume na wale wenye nguvu ya kambi ya pili kwani hawa ndiyo wanapendwa na wananchi. Kama anataka kuwa katika nafasi ya kushika tena madaraka 2010 hana budi kuwa popular.
Sasa amebakia kuhangaika na kulalamika pembeni.... Afanye nini?