Mponjoli
04-03-2009, 05:41 PM
Kyela, wilaya iliyoko kwenye bonde la ziwa Nyasa, hukumbwa na mafuriko kila wakati. Mafuriko haya ambayo huja taratibu hutokana na mvua nyingi zinazonyesha katika milima ya Livingstone, na Rungwe ,na milima ya Mlanje huko Malawi.Mvua hizi hugharikisha mito Mikuu minne ya wilaya ya Kyela: mto Kiwira, Songwe, Mbaka na Lufilyo.
Kila mafuriko haya yakitokea,huacha janga kubwa la makazi, njaa na milipuko ya magonjwa.
HOJA:.
Je Kuna mipango yoyote madhubuti ya kudhibiti mafuriko haya kwa kutunza hayo maji yanayozidi kwenye mabwawa na kuyatumia kwa kazi ya umwagiliaji maji wakati wa kiangazi?
Siyo siri kwamba Wilaya hii hukumbwa na njaa karibu kila msimu na ndio soko kuu ya mazao toka Mbeya, Rungwe ,Makete na Malawi. Kinachosikitisha ni kwamba kuna mito mikuu minne iliyo na umbali usiozidi km 20 kati ya kila mmoja. Sijui kama kuna mikakati yoyote ya kutumia utajiri huu kuondoa baa hili la njaa, na pia kudhibiti mafuriko ya kila mwaka.
Nadhani imefika wakati wanasiasa wetu watuonyeshe ni jinsi gani wanakerwa na hali hii na waonyeshe uthubutu wa kupambana na hali hizi.
Kila mafuriko haya yakitokea,huacha janga kubwa la makazi, njaa na milipuko ya magonjwa.
HOJA:.
Je Kuna mipango yoyote madhubuti ya kudhibiti mafuriko haya kwa kutunza hayo maji yanayozidi kwenye mabwawa na kuyatumia kwa kazi ya umwagiliaji maji wakati wa kiangazi?
Siyo siri kwamba Wilaya hii hukumbwa na njaa karibu kila msimu na ndio soko kuu ya mazao toka Mbeya, Rungwe ,Makete na Malawi. Kinachosikitisha ni kwamba kuna mito mikuu minne iliyo na umbali usiozidi km 20 kati ya kila mmoja. Sijui kama kuna mikakati yoyote ya kutumia utajiri huu kuondoa baa hili la njaa, na pia kudhibiti mafuriko ya kila mwaka.
Nadhani imefika wakati wanasiasa wetu watuonyeshe ni jinsi gani wanakerwa na hali hii na waonyeshe uthubutu wa kupambana na hali hizi.