PDA

View Full Version : Nyaraka za ufisadi zitaendelea kuvuja tu!!!



pangamawe
04-22-2009, 09:43 AM
Jana kama kawaida yake limeanza na mjadala wa kipuuzi ambao umetokana na swali la kipuuzi lililoulizwa na siraju kaboyonga ambaye dhamira inanizuia kumwita mheshimiwa mbunge wa Tabora. Katika swali lake ninaloliita la kipuuzi alitaka kujua serikali inachukua hatua gani kupambana na "wezi" wa nyaraka za serikali wakiwemo wabunge. Katika majibu yake ya kipuuzi vilevile hawa ghasia kasema hatua kali zitachukuliwa kwani wabunge hawana kinga dhidi ya nyaraka za siri za serikali.

Haya ni mambo ya ajabu sana viongozi wengi wa serikali wamejikita kwenye ufisadi huku watumishi wa ngazi za chini wakiteseka kwa mishahara isiyokidhi mahitaji halafu inategemea eti nyaraka za ufisadi huo zisiibiwe. Nilitegemea serikali itoe tamko kama hilo ili kutisha watu wasiibue nyaraka za ufisadi mwingi tarajiwa kwani tunajua CCM inatafuta pesa za kununulia shahada za kupigia kura katika uchaguzi mkuu mwakani hivyo kila aina ya ufisadi unafanyika kuelekea lengo hilo. Watu kama Kaboyonga ambao ni wengi sana miongoni mwa wabunge wa CCM wanachowaza ni nkujipendekeza ili wateuliwe kuwa mawaziri ungetegemea kaboyonga aonyeshe kukerwa na tabu za kimaisha za wapiga kura wake badala yake eti anakerwa nauvujaji wa nyaraka za serikali zinazohusu ufisadi.

Wabunge wengi wa CCM ni tatizo kubwa sana Dr Slaa kashambuliwa kwa vile kataja hadharani kipato cha wabunge, nampongeza sana dr slaa kwa hilo maana wengi wa wabunge wa CCM wako busy na kuji-identify na serikali ili wapewe uwaziri ndiyo maaana nadhani wakati umefika mawaziri wasitokane na wabunge ndipo watu wa aina ya kaboyonga ,nyalandu hawataingia bungeni.

Nwapa shime wazalendo wenzangu waendelee kufichua hila za ufisadi zinazoratibiwa na serikali kwaajili ya uchaguzi mwakani kwani hazina tija yoyote kwa watanzania bali kuwaimarisha madarakani watawala wetu mafisadi. Hivi sasa kuna ufisadi mkubwa sana unaandaliwa na serikali kwa lengo hilohilo la uchaguzi mwakani. Ni mradi wa kurusha live uhamaji wa nyumbu katika hifadhi ya serengeti, mradi huu wa kitapeli utakaogharimu mabilioni ya shilingi unaratibiwa na tapeli mmoja wa kitanzania aishiye nchini marekani aitwaye Dr Tenende ukiwa na baraka zote za ikulu. Huu mradi ni white elephant na unapingwa vikali na wataalamu wa uhifadhi lakini kwa vile lengo ni kukusanya pesa za uchaguzi wakubwa hawataki kusikia kitu. Nitaleta details na nyaraka za mradi huu wa kitapeli unaoitwa WILD BEASTS MIGRATION LIVE BROADCAST

Baraka
04-22-2009, 02:12 PM
Nashukuru sana kwa mada hii. Maana jambo la kwanza wabunge ni akina nani? Ninavyofahamu mimi wanatuwakilisha sisi wananchi ambao hatuwezi kwa uwing wetu kukaa na kupanga mipango. Kama wanatuwakilisha hizo siri za kipato zinatoka wapi? Kuna wakati nakata tamaa hata ya kushiriki kwenye uchaguzi maana sioni kama kuna maana yeyote, ni process ya kuhalalishia wachache ufisadi!!! Nadhani darasa tumelipata hata hao tunaowaita wapinzani, wengi wao yao ni yaleyale ikifikia ulaji hakuna mpinzani wanaungana kujitetea. Inatia aibu sana. Dr. Slaa nadhani ni heshima zaidi tukakuita kwa wadhifa wako wa kisomi kuliko huo uishiwa wa genge la hapo Dodoma. Jinsi wanavyofanya mambo inatia aibu kweli. Nimesikia kuwa kuna Muishiwa mmoja wa upinzani aliwekwa sawa kwa kununuliwa gari na Mjanja wa Kagoda, Dowans na Richmond!!! Natafuta data halafu nitaweka bayana, lakini hii ndiyo inayosababisha watu wenye uchungu na nchi hii kushindwa kufaya kazi. Slaa kataja zake, na wengine waseme kama ni uongo cha ajabu ninini? Hizo ni hela ambazo tunadhulumuwa kama kodi. Naita dhuluma kwa sababu lmalengo ya kodi ni kuleta maendeleo na si kuneemesha wachache. WABUNGE KUWENI NA AIBU. Namshangaa sana Ghasia, kwa kweli anaendana na jina hilo eti nyaraka za serikali, bila 'kuibiwa EPA ingekuwapo? na Richmond na DOWANS je? Halafu unaona watu wanajitia ni washika dini!! Aibu kubwa. Watabzabia tuamke, hata wapinzani waangaliwe wengine ni kama mbegu viza DECI zilizokataa kuota. Tugangamae na hoja

edo
04-22-2009, 10:05 PM
Ninachoelewa mimi ni kwamba serikali yoyote inapaswa kuangalia maslahi ya wananchi wake lakini kinachosikitisha na serikali yetu ya CCM ni kwamba ipo kwa ajili ya kuangalia maslahi ya wachache walio ndani ya serikali yenyewe.Ninasema wachache kwa maana hiyo hiyo ya wachache kwani kwa kweli ni wachache na wanahesabika ukilinganisha ni idadi halisi ya watanzania.

Kwa nini nguvu na mikakati hiyo inayotaka kutumiwa na serikali kuzuia wizi wa nyaraka (zinazoitwa za siri lakini zilizojaa dhambi) isitumike kuhakikisha kwamba mafisadi ambao wakuu wa serikali wanaishi nao,kula nao na hata kushiriki nao vikao vya chama na serikali wanatokomezwa? Likifanyika hilo, hata hizo nyaraka zao watu hawatazihitaji tena.Serikali inaweza kuhofia nyaraka zake kwa sasa lakini kama pengo hili la masikini na matajiri litaendelea kukua kwa kasi kama ilivyo sasa (kutokana na ufisadi kutamalaki), kwa vyovyote vile nchi itaishia kwenye tatizo kubwa zaidi kuliko hata hizo nyaraka.Tatizo hilo litakuwa ni kutoweka kwa amani tuliyonayo nchini. Hakuna wa kuikomboa nchi hii isipokuwa ni mtanzania mwenyewe.Tuamke!!!

Dalali
04-23-2009, 01:23 PM
Nashukuru aliyeuliza swali kwani katusaidia kuelewa mpango kamili wa Serikali.Binafisi napenda kuwekwe bayana kati ya nyaraka za serikali accessiblbe kwa mwananchi na nyaraka za SIRI za serikali kama Usalama wa Taifa nk.
Ghasia alitakiwa kubainisha kuwa Wizi wa EPA, MEREMETA, RICHMOND nayote nisiyoyataja ni nyaraka za siri au la ili kuepuka tuhuma inayomjia.
Hatuna dawa katika mahospitali na Elimu inadorora kila kitu ufinyu wa badget watu wakijilipa 152m kwa siku kwa Richmond na, Hela lukuki za EPA na mikataba mibovu hata mingine inasainiwa nje ya nchi na watu wakiwa Bar.
Ghasia aache kuchezea akili za watu, aache kutukana watu anapozungumzia swala hili broadly.Wananchi tuna hasira kwa maovu mengi yaliyokwisha tendwa.
Dalali

mwanakijiji
04-23-2009, 07:38 PM
Unajua nimeona nimjibu Hawa Ghasia kwa sababu kama Dalali ulivyosema, Ghasia na Kaboyonga hawakuwa wanazungumzia nyaraka za usalama wa Taifa; wao walikwua wanazungumzia nyaraka zilizofichua ufisadi. Na hizi ndizo hawataki watu wawe nazo kwani hadi hivi sasa sijaona au kusikia mwanasiasa yoyote aliyeibuka na nyaraka zinazotishia usalama wa Taifa. Labda hizo za Kagoda!

QUTE
04-23-2009, 10:54 PM
Bunge kuanza tu linaanza na upupu. Haya anayoyaonge Ghasia ndio ambayo walikuwa wanapanga wakati wa likizo yao ya ubunge! hakuna jipya na sisi wananchi tusitegemee mapya.
Inasikitisha sana, wabunge wanashindwa kutumia likizo zao kuongea na wananchi wao ili wabebe kero za wananchi kuzipeleka bungeni wanafungua bunge na mikwara.
Siri zitavuja tu wananchi wameshachoka wataendelea kuwalinda mafisadi mpaka lini? kila lililo na mwanzo halikosi kuwa mwisho