PDA

View Full Version : Maoni ya Prof Safari wa CUF



dickabudi
05-28-2009, 03:11 PM
Prof Safari


Alisema CUF itaendelea kupoteza umaarufu kila kukicha kwa sababu uwezo wa kuongoza wa Prof. Lipumba na Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad ulishafikia kikomo

"Pale hakuna kitu... hakuna cha Maalim Seif wala Profesa Lipumba," alisisitiza na kuongeza kwamba wamebaki kusimamisha wagombea kwa ajili ya kushamirisha demokrasia lakini sio kwa ajili ya kushinda."



Mr John Chiligati



"Ni kweli aliyeshika namba mbili (Bw, Max) anafahamika sana hasa kutokana na kujihusisha na biashara ya pamba tofauti na yule mama (Bi. Bukwimba) hata kwenye vikao vyetu tulilijadili sana, tuliamua hivyo kwa kizungu wanasema ku-risk lile jimbo ili kuwasaidia akina mama...unajua ukisaidia akina mama unakuwa umesaidia jamii," alisema Bw.Chiligati.

"Hii si mara ya kwanza kwa CCM kufanya maamuzi ya 'ku-risk' jimbo ilishawahi kufanya hivyo kwa Lucy (Bi. Lucy Msafiri) na Tatu (Bi. Tatu Ntimizi) ambao kwenye kura za maoni kwenye majimbo yao walikuwa wameshika nafasi ya tatu.

"Tunachukua 'risk' kusaidia akina mama lakini wale watakaobainika kujihusisha na rushwa kwenye kura za maoni tutawafikisha mahakamani CCM haina mchezo na hilo hata kama mkakati wetu ni kuongeza idadi ya wanawake kwenye vyombo vya maamuzi," alisema.

Tujadili haya kwa nguvu

Akajase
05-28-2009, 07:12 PM
Prof Safari


Alisema CUF itaendelea kupoteza umaarufu kila kukicha kwa sababu uwezo wa kuongoza wa Prof. Lipumba na Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad ulishafikia kikomo

"Pale hakuna kitu... hakuna cha Maalim Seif wala Profesa Lipumba," alisisitiza na kuongeza kwamba wamebaki kusimamisha wagombea kwa ajili ya kushamirisha demokrasia lakini sio kwa ajili ya kushinda."



Mr John Chiligati



"Ni kweli aliyeshika namba mbili (Bw, Max) anafahamika sana hasa kutokana na kujihusisha na biashara ya pamba tofauti na yule mama (Bi. Bukwimba) hata kwenye vikao vyetu tulilijadili sana, tuliamua hivyo kwa kizungu wanasema ku-risk lile jimbo ili kuwasaidia akina mama...unajua ukisaidia akina mama unakuwa umesaidia jamii," alisema Bw.Chiligati.

"Hii si mara ya kwanza kwa CCM kufanya maamuzi ya 'ku-risk' jimbo ilishawahi kufanya hivyo kwa Lucy (Bi. Lucy Msafiri) na Tatu (Bi. Tatu Ntimizi) ambao kwenye kura za maoni kwenye majimbo yao walikuwa wameshika nafasi ya tatu.

"Tunachukua 'risk' kusaidia akina mama lakini wale watakaobainika kujihusisha na rushwa kwenye kura za maoni tutawafikisha mahakamani CCM haina mchezo na hilo hata kama mkakati wetu ni kuongeza idadi ya wanawake kwenye vyombo vya maamuzi," alisema.

Tujadili haya kwa nguvu

Nakubakiana na kauli ya Prof Safari,kutokana na kuwa hata wana-CUF wengine wamaliona hilo na wananung'unika kwa chini chini ila kipo kinachowafanya wasiondoke CUf upesi. wanamatumaini fulani ambayo matokeo yake hayatakuwa ya leo labda miaka kadhaa. katika hicho wanachokitumainia sinauhakika kama kinaweza timia kwangu ni kama ndoto ya alfajiri.

Akiwa nje ya uongozi mkuu wa CUF, Prof S. alitoa hoja nyingi za msingi. Ila kwasababu hata ukiwaangalia kwa macho tu namna ujumla wa maongezi ya wana-CUF waliokuwa pale Diamond Jubilee kwenye Mkutano Mkuu, unajua hapa ni kama 'kumfundisha mjinga ambaye amani yake inatokana na huo'. Ndiyo maana akapigwa chini.

Mpita Njia
05-29-2009, 10:57 AM
Kuna kitu kimoja ambacho watu wengi hawakielewi. Kati ya vyama vya siasa vya upinzani, CCM inaogopa zaidi CUF kuliko chama kingine chochote kwa sababu cheneywe ndicho kinachoongozwa kwa misingi kama ya CCM. Kumbuka kuwa wengi wa viongozi wa juu wa CUF walitoka CCM< wanajua kuongoza chama kwa namna mbalimabli na kwua na mikakati y kukabiliana na mabadiliko ya kisiasa. Tunaweza kuona Chadema au chama kingine kina sifa kubwa mitaani kutokana na mbwembwe, lakini kwa ndani kabisa, kwa kazi ya siasa, kwa CCM, CUF ni hatari zaidi nkuliko hivyo vyama vingine

bulesi
05-29-2009, 06:18 PM
Usisahau pia kuwa kama uchaguzi huko visiwani ukifanyika kwa uhuru na haki; CUF itaishinda CCM hands down! Na hilo CCM inalijua vizuri na ndio maana kila mara wanajitahidi kuiba kura hasa kule Unguja.

MAHESABU
09-21-2010, 12:19 AM
Profesa safari yu wapi huyu....?