PDA

View Full Version : Nani alaumiwe?



mwanakijiji
11-13-2008, 11:58 PM
Mama ambaye ni mtu ambaye jina lake watu wanalifahamu tukilitaja; anaipenda kazi yake na anajitahidi kweli kuiangalia nyumba yake lakini majukumu ya kazi n.k yanamfanya awe busy muda mrefu na hivyo kulazimu kuwa na msaidizi nyumbani.

Kaenda mkoa fulani ambako rafiki yake alimuunganisha na binti aliyemaliza darasa la saba ili aje kumsaidia kumuangalia Junior na mdogo wake ambao ndio wameanza chekechea tu.

Kabinti kalipokuja kalikuwa kadogo dogo tu lakini mwaka wa kwanza na wa pili kakaanza kuchanuka kama maua. Mama akawa amemuahidi kumtafutia sekondari ya jioni ili ajiendeleze n.k Baba mwanzoni alikuwa hamuangalii namna hiyo hadi siku moja wamegongana wakati binti ametoka bafuni...

Wazo baya likaanza kumuingia Baba fulani, akajaribu kukwepa lakini kwa mawazo yake akawa anaona kuwa mkewe hampi mambo yanavyopasa halafu yuko busy sana kufanya mambo yale ya ujana wao. Siku moja wakati mama amesafiri kwenda Morogoro kikazi jamaa akasema leo ni leo.

Watoto wakiwa wamelala, akamuita yule binti akijifanya kuwa amekunywa akaanza kuka"sumbua" mara "njoo kaa hapa". n.k mwisho akatumia nguvu kukaingia akamuahidi maisha mazuri fedha ya matumizi n.k n.k

Mtumishi akaanza kunawiri na kupendeza zaidi na zaidi.. Mama mwenye nyumba akawa anafikiria ni kukomaa tu; mwisho kikaanza kiburi ndani ya nyumba...

Siku moja ikafika kuwa binti anaanza kuonesha dalili za mimba.. Mama kumuuliza mtoto hataki kusema anataka kurudi kwao... Mama anaamua kumrudisha. Wanakubaliana na mumewe kumrudisha kwao. Baba anasema ameshakata tiketi na kesho yake atampeleka yeye mwenyewe Ubungo kupanda basi...

Kumbe kampangia chumba, maeneo ya Sinza!

Baba ni kiongozi mkubwa serikalini na mama ni mmoja wa wabunge ....

Mtoto kazaliwa picha ya baba!!!

anonymous
11-14-2008, 02:22 AM
Mama ambaye ni mtu ambaye jina lake watu wanalifahamu tukilitaja; anaipenda kazi yake na anajitahidi kweli kuiangalia nyumba yake lakini majukumu ya kazi n.k yanamfanya awe busy muda mrefu na hivyo kulazimu kuwa na msaidizi nyumbani.

Kaenda mkoa fulani ambako rafiki yake alimuunganisha na binti aliyemaliza darasa la saba ili aje kumsaidia kumuangalia Junior na mdogo wake ambao ndio wameanza chekechea tu.

Kabinti kalipokuja kalikuwa kadogo dogo tu lakini mwaka wa kwanza na wa pili kakaanza kuchanuka kama maua. Mama akawa amemuahidi kumtafutia sekondari ya jioni ili ajiendeleze n.k Baba mwanzoni alikuwa hamuangalii namna hiyo hadi siku moja wamegongana wakati binti ametoka bafuni...

Wazo baya likaanza kumuingia Baba fulani, akajaribu kukwepa lakini kwa mawazo yake akawa anaona kuwa mkewe hampi mambo yanavyopasa halafu yuko busy sana kufanya mambo yale ya ujana wao. Siku moja wakati mama amesafiri kwenda Morogoro kikazi jamaa akasema leo ni leo.

Watoto wakiwa wamelala, akamuita yule binti akijifanya kuwa amekunywa akaanza kuka"sumbua" mara "njoo kaa hapa". n.k mwisho akatumia nguvu kukaingia akamuahidi maisha mazuri fedha ya matumizi n.k n.k

Mtumishi akaanza kunawiri na kupendeza zaidi na zaidi.. Mama mwenye nyumba akawa anafikiria ni kukomaa tu; mwisho kikaanza kiburi ndani ya nyumba...

Siku moja ikafika kuwa binti anaanza kuonesha dalili za mimba.. Mama kumuuliza mtoto hataki kusema anataka kurudi kwao... Mama anaamua kumrudisha. Wanakubaliana na mumewe kumrudisha kwao. Baba anasema ameshakata tiketi na kesho yake atampeleka yeye mwenyewe Ubungo kupanda basi...

Kumbe kampangia chumba, maeneo ya Sinza!

Baba ni kiongozi mkubwa serikalini na mama ni mmoja wa wabunge ....

Mtoto kazaliwa picha ya baba!!!

Du!!!
Hii kali. Lakini kwa nini tunaanza moja kwa moja kutafuta mtu wa kulaumiwa jamani!?
Je, hatuwezi kutoa ushauri na kungalia maisha ya hawa watatu na familia zao haziingii katika hali ya kuhatarisha amani na furaha ndani ya nyumba!?
Nafikiri hilo litakuwa jambo la maana kuliko kuanza kumtafuta mchawi wakati hakuna aliyologwa.
Na isitoshe, tukishamjua wa kulaumiwa, WHAT NEXT??

Kepa
11-22-2008, 10:53 PM
Anony Nakubali wazo, sasa basi tuanze kukata issue, tuwasaidiaje hawa watu watatu ( au tuseme hawa watu sita , yaani watoto 3 na wazazi 3) ili maisha yao yawe ya amani.

Wazo langu naona ili mambo yasiendelee kuharibika (ndoa ya waheshimiwa) Inabidi mambo yawekwe hadharani, Mke asomeshwe naa kisha aombwe msamaha na mume aache tena kuzengea kabinti ila atunze mtoto kama kawaida kama anavyowatunza akina Junior. Vinginevyo hatukawii kusikia mtoto wa pili , watatu,....nk. kazaliwa.

mwanakijiji
11-23-2008, 06:36 PM
Anony Nakubali wazo, sasa basi tuanze kukataa issue, tuwasaidiaje hawa watu watatu ( au tuseme hawa watu sita , yaani watoto 3 na wazazi 3) ili maisha yao yawe ya amani.

Wazo langu naona ili mambo yasiendelee kuharibika (ndoa ya waheshimiwa) Inabidi mambo yawekwe hadharani, Mke asomeshwe naa kisha aombwe msamaha na mume aache tena kuzengea kabinti ila atunze mtoto kama kawaida kama anavyowatunza akina Junior. Vinginevyo hatukawii kusikia mtoto wa pili , watatu,....nk. kazaliwa.


lakini kuna watu wanasema "once a cheater, always a cheater". Nadhani hata huyo mama akijua ukweli hawezi kumuacha mumewe kimoja kwani kisiasa itakuwa ni mbaya sana.

Mpita Njia
11-27-2008, 04:21 PM
Ahaaa, kwani kilichomfanya huyo bwana mkubwa ageukie kwa kabinti ni uzuri wa binti, uchu wake, au mwenzi wake kuwa busy na kushindwa kumpatia vitu kama enzi za ujana wao?

My more
11-29-2008, 11:12 PM
Ahaaa, kwani kilichomfanya huyo bwana mkubwa ageukie kwa kabinti ni uzuri wa binti, uchu wake, au mwenzi wake kuwa busy na kushindwa kumpatia vitu kama enzi za ujana wao?

Mmhhh sidhani!:mad:

duru langu
11-30-2008, 02:00 AM
Sijui huyo junior anaumri gani: Usijekuta na yeye alishaanza kujipongeza kwa
"dada" hasa baada ya mzee kuanza kutoa burudani kwani yawezekana kuna wakati
mzee mazingira hayakumruhusu kutoa huduma hivyo "dada" kutumia huduma ya junior