Mpita Njia
06-12-2009, 11:44 AM
Katika mlolongo wa matukio, kubwa linalozungumzwa hivi sasa kuwahusu ni kujiuzulu kwa Wilfred Lwakatare kutoka kwenye nyadhifa zote alizonazo isipokuwa uanachama wa kawaida.
Lakini kwa wafuatiliaji wa mambo, hasa ya siasa, wanafahamu fika kuwa kuna msukosuko (hata kama ni wa chinichini) unaonedelea ndani ya Chama cha wananchi (CUF). Wenyewe CUF wanaweza kupinga hili kisiasa lakini ndai ya mioyo yao wanajua kuwa hilo lipo.
Mimi binafsi bado nakichukulia chama hiki cha upinzani kama kielelezo cha chama ambacho kimeoneysha kwa vitendo jinsi ambavyo siasa zinapaswa kuendeshwa. Najua kuwa wana makosa yao ya hapa na pale na naamini hilo ni jambo la kawaida.
Kinachonishangaza ni kuwa yanayotokea hivi sasa ndani ya chama hiki yanaonyesha kuporomoka kwa kasi na kwa kiwango kikubwa kwa chama ambacho uimara wake ulikuwa ni tishio kubwa kwa CCM. najua zipo sababu kadhaa zilizowahi kuanishwa, lakini siamini kwua ndizo hasa zinazosababisha mtikisiko mkubwa kiasi hiki ndani ya CUF kwa sababu hata viongozi walizijua na kutokana na utaalamu wao katika siasa, isingewawea vigumu kuzidhibiti.
Kwa nini viongozi wameshindwa kudhibiti hali hiyo kiasi kwamba chama hiki kinaonekana kipo hatarini?
Kuna lolote amballo CUF walitakiwa kulifanya, wakashindwa kulifanya au ambalo hawakutakiwa kulifanya na wao wakalifanya?
Najua kwua wengi wanaamini kuwa kujiuzulu kwa Lwakatare ambako kunaweza kuishia kwenye kujiondoa kabisa kwenye chama hicho, hautakuwa mwisho wa CUF, lakini je, huo hauwezi kuwa ndio mwanzo wa mwisho wa chama hicho?
Lakini kwa wafuatiliaji wa mambo, hasa ya siasa, wanafahamu fika kuwa kuna msukosuko (hata kama ni wa chinichini) unaonedelea ndani ya Chama cha wananchi (CUF). Wenyewe CUF wanaweza kupinga hili kisiasa lakini ndai ya mioyo yao wanajua kuwa hilo lipo.
Mimi binafsi bado nakichukulia chama hiki cha upinzani kama kielelezo cha chama ambacho kimeoneysha kwa vitendo jinsi ambavyo siasa zinapaswa kuendeshwa. Najua kuwa wana makosa yao ya hapa na pale na naamini hilo ni jambo la kawaida.
Kinachonishangaza ni kuwa yanayotokea hivi sasa ndani ya chama hiki yanaonyesha kuporomoka kwa kasi na kwa kiwango kikubwa kwa chama ambacho uimara wake ulikuwa ni tishio kubwa kwa CCM. najua zipo sababu kadhaa zilizowahi kuanishwa, lakini siamini kwua ndizo hasa zinazosababisha mtikisiko mkubwa kiasi hiki ndani ya CUF kwa sababu hata viongozi walizijua na kutokana na utaalamu wao katika siasa, isingewawea vigumu kuzidhibiti.
Kwa nini viongozi wameshindwa kudhibiti hali hiyo kiasi kwamba chama hiki kinaonekana kipo hatarini?
Kuna lolote amballo CUF walitakiwa kulifanya, wakashindwa kulifanya au ambalo hawakutakiwa kulifanya na wao wakalifanya?
Najua kwua wengi wanaamini kuwa kujiuzulu kwa Lwakatare ambako kunaweza kuishia kwenye kujiondoa kabisa kwenye chama hicho, hautakuwa mwisho wa CUF, lakini je, huo hauwezi kuwa ndio mwanzo wa mwisho wa chama hicho?