Mpita Njia
11-16-2008, 06:00 PM
Nimezungumza na Mwenyekiti wa Chama cha walimu, Bwana Gratian Mukoba leo anasema kuwa mgomo wao wa kesho upo palepale licha ya ahadi na vitisho vinavyotolewa na serikali. tena anasema kuwa ahadi na vitisho hivyo ni uthibitisho kuwa madai yao ni ya kweli.
Anachosema Mukoba:
Kwamba serikali imekwenda mahakamani kutaka mgomo huo uzuiwe haiitishi CWT kwa sababu hadi hivi sasa chama hicho hakijapokea summuns kutoka mahakama yoyote.
Tishio kuwa walimu watakaogoma watakatwa mishahara haliwatishi.
Ahadi kwamba fedha zimeanza kupelekwa wilayani haliwahusu, wanachotaka wao si fedha kupelekwa wilayani, bali walipwe madai yao.
Anachosema Mukoba:
Kwamba serikali imekwenda mahakamani kutaka mgomo huo uzuiwe haiitishi CWT kwa sababu hadi hivi sasa chama hicho hakijapokea summuns kutoka mahakama yoyote.
Tishio kuwa walimu watakaogoma watakatwa mishahara haliwatishi.
Ahadi kwamba fedha zimeanza kupelekwa wilayani haliwahusu, wanachotaka wao si fedha kupelekwa wilayani, bali walipwe madai yao.