PDA

View Full Version : Uchawi Upo??



Mama Askofu
09-07-2009, 11:41 AM
Heshima Mbele Wakuu

Naomba mnisaidie jibu!!

Hivi karibuni nimesimuliwa na Jirani yangu kuwa mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka kati ya 12 au 13 hivi, alirushiwa maruhani (majini) kama waswahili wanavyosema. Huyo mama anasema hayo Maruhani au Majini recently yakacharuka yanataka kuondoka na huyo mtoto.

Mama mtoto ni Mkatoliki mzuri tu, akaanzisha maombi. Anadai kuwa hayo madude yakasema yalikotoka na kuwa yametumwa na Mama mwingine (ambaye anaishi in the neighbourhood)

Sasa, According to huyo jirani yangu, Huyo Mtoto wake alikuwa anatumiwa na huyo mama kupita kwenye nyumba zingine usiku kukusanya watoto wengine, ages from 1 year kisha anaenda kuwatumikisha kama kukusanya kuni, kusomba pumba, kusomba maji kwenye vidumu vya lita tano na kuokota mavi (ambayo wanadai huyo Mama anayedaiwa ni mchawi anatumia kama one of ingredients za kupikia Vitumbua, Bajia na Kalimati).

Nilipowauliza majirani wengine, wanadai kuwa watoto wao wamekuwa na tendency ya kuweweseka usiku na hata wakiwa mashuleni wanapewa ripoti kuwa watoto wao wanalala sana wakiwa shuleni, kitu wanachodai kuwa waalimu wanadhani watoto wanacheleweshwa kulala.

Wengine wanadai kuwa watoto wao wamekuwa wakiugua mafua na kikohozi kisichopona mpaka wengine wanadai kuwa wameenda kucheki kama watoto wao wana asthma, lakini cha kushangaza ni kuwa majority ya watoto in the neighbourhood wana hicho kifua na mafua yasiyopona, je kama ni vumbi mbona wakubwa hawaugui?

Tafadhalini nielimisheni kuhusu hii "elimu dunia".... Ni kweli Uchawi Upo?

Respect.... Nawasilisha

Dua
09-09-2009, 01:13 AM
Hakuna jibu. Wachawi mko wapi mtoe jibu? Khe khe... ... kazi kweli kweli uchawi hadi kijijini.

Max Shimba
09-21-2009, 07:24 PM
Mama Askofu, uchawi upo, yaani hizo ni nguvu za giza, zipo na zinafanya kazi.

Kutokana na Waefeso 6 mstari wa 12 tunasoma kuwa "For we do not wrestle against flesh and blood, but against principalities, against powers, against the rulers of the darkness of this age, against spiritual hosts of wickedness in the heavenly places .

Hivyo basi uchawi upo. Ni Yesu tu ndiye ataye kuokoa na kukuwezesha kushinda hizi nguvu za giza.

mwanakijiji
09-26-2009, 09:18 PM
lakini nguvu ya uchawi hutokana na kukolezwa na hofu; tangu enzi na enzi watu wenye kusadikiwa kuwa wana nguvu zisizo za kibinadamu na wanaweza kuzitumia kwa ubaya wamekuwepo.

outlier
09-28-2009, 06:30 AM
Heshima Mbele Wakuu

Naomba mnisaidie jibu!!

Hivi karibuni nimesimuliwa na Jirani yangu kuwa mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka kati ya 12 au 13 hivi, alirushiwa maruhani (majini) kama waswahili wanavyosema. Huyo mama anasema hayo Maruhani au Majini recently yakacharuka yanataka kuondoka na huyo mtoto.

Mama mtoto ni Mkatoliki mzuri tu, akaanzisha maombi. Anadai kuwa hayo madude yakasema yalikotoka na kuwa yametumwa na Mama mwingine (ambaye anaishi in the neighbourhood)
huyo mtoto most likely kama sio wote na mama yake wana matatizo ya akili - zaidi ni mtoto; anahitaji kupata psychotherapy- hakuna kitu maruhani huwa ni matatizo tu ya kisaikolojia, na imani kuwa huyo jirani yao ni mtu mbaya!


Sasa, According to huyo jirani yangu, Huyo Mtoto wake alikuwa anatumiwa na huyo mama kupita kwenye nyumba zingine usiku kukusanya watoto wengine, ages from 1 year kisha anaenda kuwatumikisha kama kukusanya kuni, kusomba pumba, kusomba maji kwenye vidumu vya lita tano na kuokota mavi (ambayo wanadai huyo Mama anayedaiwa ni mchawi anatumia kama one of ingredients za kupikia Vitumbua, Bajia na Kalimati).

wewe pia jiulize mtoto wa mwaka 1 ama miaka 3 aweza kufanyishwa kitu kama hicho? hajajua hili wala lile, hizo ni kamba tu za watu, hizo lita 5 atabebaje hata kutembea hawezi! na hayo mavi utaanzia wapi kuyatengeneza vitumbua? c'mon! kwanza wanayatoa wapi, watu wa mtaa ule hawana vyoo? au wanatoa kwenye vyoo! hiyo kitu haiwezekani hata kama iandikwe kwenye "vitabu"


Nilipowauliza majirani wengine, wanadai kuwa watoto wao wamekuwa na tendency ya kuweweseka usiku na hata wakiwa mashuleni wanapewa ripoti kuwa watoto wao wanalala sana wakiwa shuleni, kitu wanachodai kuwa waalimu wanadhani watoto wanacheleweshwa kulala.watafute sababu zingine!


Wengine wanadai kuwa watoto wao wamekuwa wakiugua mafua na kikohozi kisichopona mpaka wengine wanadai kuwa wameenda kucheki kama watoto wao wana asthma, lakini cha kushangaza ni kuwa majority ya watoto in the neighbourhood wana hicho kifua na mafua yasiyopona, je kama ni vumbi mbona wakubwa hawaugui?
basi likely mtaa ama kitongoji hicho kimeingiliwa na mafua- eg swine flu au flu nyingine, na inashambulia watoto wa umri huo na wanapata mafua na kifiua na kusinzia shuleni shauri ya kukohoa usiku kucha basi, hakuna sababu nyingine


Tafadhalini nielimisheni kuhusu hii "elimu dunia".... Ni kweli Uchawi Upo?

Respect.... Nawasilisha
NADHANI UMENIPATA

Mama Askofu
10-13-2009, 10:19 AM
NADHANI UMENIPATA[/QUOTE]


Nimekusoma Mkuu, thanks