Obama kumbe siyo masihi!!
Alipoingia madarakani aliingia kwa mbwembwe na kwa ahadi tamu tamu kama za Kikwete. Aliingia kwa kauli mbiu ya "Change - Yes we Can". Wamarekani waliamini kauli hiyo kama vile wabongo walivyoamaini kauli ya "ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya" ya Kikwete.
Matokeo yake leo hii Obama anajikuta anapingwa na ajenda yake inakutana na vigingi kuliko ulivyotarajiwa. Umaarufu wake wa kisiasa umeshuka kwa kiasi kikubwa na licha ya mvuto wake ameshindwa kuzuia chama cha Republican kujitutumua katika chaguzi mbalimbali zilizofanyika ndani ya mwaka mmoja wa utawala wake.
Hatimaye sasa inaonekana Obama atalazimika kubadili kwa kiasi kikubwa ajenda yake na hatimaye kulazimisha kuzungumza na wapinzani wake wa kisiasa na kuwasikiliza kwani vinginevyo mambo yake hayatokwenda kabisa.
Wamarekani wamegundua kuwa Obama ni mwanasiasa kama wengine na siyo masiha waliyemtarajia. Tusipoangalia anaweza akawa kama Jimmy Carter aliyetawala kwa mhula mmoja tu!
Uhuru wa mbuzi zizini ni uhuru kwa kadiri ya kwamba chui hajasikia njaa - MM original
Bookmarks