+ Reply to Thread
Results 1 to 7 of 7

Thread: Kesi ya Chenge, wakili aja juu

  1. #1
    Join Date
    Oct 2008
    Posts
    1,648

    Default Kesi ya Chenge, wakili aja juu

    Ummy Muya (Mwananchi)

    WAKILI Simon Mponda ambaye anamtetea Mwanasheria Mkuu wa zamani wa serikali (AG), Andrew Chenge katika kesi ya mauaji ya wasichana wawili amekuja juu na kuita mahakama iharakishe kutoa maelezo ya upande wa mashtaka dhidi ya tuhuma za mteja wake, ili kesi iendelee badala ya kuahirishwa mara kwa mara.

    Mponda alisema jana mbele ya Hakimu Kwey Rusema wa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kesi hiyo imekuwa ikiahirishwa mara kwa mara kutokana na kukosekana maelezo hayo.

    "Naomba mahakama iharakishe kutoa maelezo ya upande wa mashtaki ili kuliwezesha shauri hili kuanza kusikilizwa, kwani kila mara tunahudhuria mahakamani lakini huwa linapigwa tarehe kwa kukosa maelezo,"alisema Mponda.

    Kesi hiyo ambayo maelezo yake ya awali yalipangwa kuanza kusikilizwa jana ilishindikana hivyo kuahirishwa hadi Aprili 9, mwaka huu kwa sababu mwendesha mashtaka ambaye ni Wakili wa Serikali, Richard Rweyongeza alikuwa kwenye kesi nyingine katika mahakama ya rufaa.

    Chenge alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Machi 30 mwaka jana, akikabiliwa na mashtaka matatu kabla ya kuongezea moja na kufikia idadi ya mashtaka manne.

    Ilidaiwa mahakamani kuwa Machi 27 mwaka jana, Chenge alisababisha kifo cha Victoria George kwa kuendesha gari kizembe katika Barabara ya Haile Selassie, Wilaya ya Kinondoni akiwa na gari aina ya Toyota Hilux Double Cabin, kisha kuigonga pikipiki ya matairi matatu aina ya Bajaj na kusababisha kifo cha Victoria ambaye alikuwa abiria(katika Bajaj hiyo).

    Shtaka la pili, Chenge anadaiwa kuwa siku na muda huo huo, alisababisha kifo cha Beatrice Constantine kwa kuendesha gari kizembe.

    Shtaka la tatu ni kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha uharibifu wa Bajaj ambayo ilikuwa imebeba wanawake hao na la nne ni kuendesha gari bila kuwa na hati ya bima.

    Akimsomea mashtaka hayo, Mwendesha Mashtaka Mkuu, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), David Mafwimbo, alidai mbele ya Hakimu Mkuu Mfawidhi, Emiliusi Mchaulo, kuwa katika shtaka la kwanza, Chenge anadaiwa kusababisha kifo cha Victoria George kwa uendeshaji wa gari kizembe.

    Alidai kuwa Machi 27, mwaka jana, saa 10:30 alfajiri katika Barabara ya Haile Selassie, wilayani Kinondoni, akiwa anaendesha gari aina ya Toyota Hilux Double Cabin, kwa uzembe na kushindwa kuchukua tahadhari kama inavyotakiwa kwa watumiaji wa barabara, aligonga Bajaj na kusababisha kifo cha Victoria na Beatrice Constantine waliokuwa katika pikipiki hiyo.

    Mshtakiwa huyo alikana mashtaka yote na ASP Mafwimbo aliiambia mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

    Akitoa masharti ya dhamana, Hakimu Mchaulo, alisema ili mshtakiwa adhaminiwe, lazima awe na mdhamini mmoja ambaye atasaini bondi ya Sh1 milioni.

    Chenge alidhaminiwa na Mkurugenzi wa Fedha toka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHCR), Ezekiel Masanja na kesi hiyo ikaahirishwa hadi Aprili 30, mwaka jana.

    Chenge ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika serikali ya awamu ya tatu na Waziri wa Miundombinu katika serikali ya awamu ya nne, wakati ajali hiyo ikitokea, alikuwa akiendesha gari lake binafsi.
    Uhuru wa mbuzi zizini ni uhuru kwa kadiri ya kwamba chui hajasikia njaa - MM original

  2. #2
    Join Date
    Nov 2008
    Location
    Bongoland
    Posts
    3,407

    Default

    Ushahidi gani ambao bado haujapatikana, hizi kesi za bongo bwana jamaa kaua wampige miaka yake mambo kwisha hizi nahau hadi lini? Au wanaogopa kivuli chake?

  3. #3
    Join Date
    Dec 2009
    Location
    Tanzania
    Posts
    240

    Default

    Hii nayo vipi kama sikosei ni leo ... ....
    Follow the bee here

  4. #4
    Join Date
    Nov 2008
    Location
    Bongoland
    Posts
    3,407

    Default

    Chenge denies nine facts in traffic case



    Quote Originally Posted by NURU MANKO
    9th April 2010

    THE former Attorney General and Minister, Mr Andrew Chenge denied nine facts but accepted one in a traffic case he is facing at Kinondoni Court in Dar es Salaam today. Mr Chenge, an MP, allegedly failed to take proper precaution to other road users and knocked a bajaj with registration number T 736 AXC, causing the death of two women identified as Victoria George and Beatrice Constantine. Before Principal Resident Magistrate Kwey Rusema, Assistant Superintendent of Police (ASP), David Mwafimbo read 10 facts before the court. The accused admitted one fact, that he was the one who was driving the car involved in the accident.

    Advocate Simon Mponda, for the defence asked the court to give him a copy of illustrations and details which would be used as evidence in the case. These include vehicle inspection, reports of investigation, death report and map of the scene of the accident. The Principal Resident Magistrate Rusema adjourned the case to April 28, for witnesses to testify. The prosecution told the court that Mr Chenge allegedly committed the offence on March 27, last year, at around 4.30am along Haile Selassie Road, Karume area in Dar es Salaam. On the material day, Mr Chenge who was driving a Toyota Hillux Double Cabin with registration number T 513 ACE, allegedly drove recklessly and caused an accident.

    He is further accused of causing damage to the bajaj and driving a vehicle without insurance cover on a public road. Mr Chenge also served as Minister for East African Co-operation and later Minister for Infrastructure Development.
    Sishangai baada ya siku kadhaa watasema hakuna ushahidi ingawa Watanzania wawili wamepoteza maisha.

  5. #5
    Join Date
    Nov 2008
    Posts
    3

    Default

    Quote Originally Posted by mwanakijiji View Post
    Ummy Muya (Mwananchi)

    WAKILI Simon Mponda ambaye anamtetea Mwanasheria Mkuu wa zamani wa serikali (AG), Andrew Chenge katika kesi ya mauaji ya wasichana wawili amekuja juu na kuita mahakama iharakishe kutoa maelezo ya upande wa mashtaka dhidi ya tuhuma za mteja wake, ili kesi iendelee badala ya kuahirishwa mara kwa mara.

    Mponda alisema jana mbele ya Hakimu Kwey Rusema wa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kesi hiyo imekuwa ikiahirishwa mara kwa mara kutokana na kukosekana maelezo hayo.

    "Naomba mahakama iharakishe kutoa maelezo ya upande wa mashtaki ili kuliwezesha shauri hili kuanza kusikilizwa, kwani kila mara tunahudhuria mahakamani lakini huwa linapigwa tarehe kwa kukosa maelezo,"alisema Mponda.

    Kesi hiyo ambayo maelezo yake ya awali yalipangwa kuanza kusikilizwa jana ilishindikana hivyo kuahirishwa hadi Aprili 9, mwaka huu kwa sababu mwendesha mashtaka ambaye ni Wakili wa Serikali, Richard Rweyongeza alikuwa kwenye kesi nyingine katika mahakama ya rufaa.

    Chenge alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Machi 30 mwaka jana, akikabiliwa na mashtaka matatu kabla ya kuongezea moja na kufikia idadi ya mashtaka manne.

    Ilidaiwa mahakamani kuwa Machi 27 mwaka jana, Chenge alisababisha kifo cha Victoria George kwa kuendesha gari kizembe katika Barabara ya Haile Selassie, Wilaya ya Kinondoni akiwa na gari aina ya Toyota Hilux Double Cabin, kisha kuigonga pikipiki ya matairi matatu aina ya Bajaj na kusababisha kifo cha Victoria ambaye alikuwa abiria(katika Bajaj hiyo).

    Shtaka la pili, Chenge anadaiwa kuwa siku na muda huo huo, alisababisha kifo cha Beatrice Constantine kwa kuendesha gari kizembe.

    Shtaka la tatu ni kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha uharibifu wa Bajaj ambayo ilikuwa imebeba wanawake hao na la nne ni kuendesha gari bila kuwa na hati ya bima.

    Akimsomea mashtaka hayo, Mwendesha Mashtaka Mkuu, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), David Mafwimbo, alidai mbele ya Hakimu Mkuu Mfawidhi, Emiliusi Mchaulo, kuwa katika shtaka la kwanza, Chenge anadaiwa kusababisha kifo cha Victoria George kwa uendeshaji wa gari kizembe.

    Alidai kuwa Machi 27, mwaka jana, saa 10:30 alfajiri katika Barabara ya Haile Selassie, wilayani Kinondoni, akiwa anaendesha gari aina ya Toyota Hilux Double Cabin, kwa uzembe na kushindwa kuchukua tahadhari kama inavyotakiwa kwa watumiaji wa barabara, aligonga Bajaj na kusababisha kifo cha Victoria na Beatrice Constantine waliokuwa katika pikipiki hiyo.

    Mshtakiwa huyo alikana mashtaka yote na ASP Mafwimbo aliiambia mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

    Akitoa masharti ya dhamana, Hakimu Mchaulo, alisema ili mshtakiwa adhaminiwe, lazima awe na mdhamini mmoja ambaye atasaini bondi ya Sh1 milioni.

    Chenge alidhaminiwa na Mkurugenzi wa Fedha toka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHCR), Ezekiel Masanja na kesi hiyo ikaahirishwa hadi Aprili 30, mwaka jana.

    Chenge ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika serikali ya awamu ya tatu na Waziri wa Miundombinu katika serikali ya awamu ya nne, wakati ajali hiyo ikitokea, alikuwa akiendesha gari lake binafsi.
    Richard Rweyongeza?? huyu sio wakili wa kujitegemea?

  6. #6
    Join Date
    Dec 2009
    Location
    Tanzania
    Posts
    240

    Default

    Wanacheza tu hapo jamaa atatoka tena kwa fujo sana na hamuwezi kumfanya chochote. Kudos Jakaya Kikwete kwa utawala bora wa sheria.
    Follow the bee here

  7. #7
    Join Date
    Nov 2008
    Location
    Bongoland
    Posts
    3,407

    Default

    Chenge's car 'was not insured'


    Quote Originally Posted by JULIUS BWAHAMA
    8th June 2010 @ 12:00
    A THIRD witness in a case involving the former Minister for Infrastructure Development, Andrew Chenge, has told the Kinondoni District Magistrate's Court that the motor vehicle involved in the accident was not insured. Senior Superintendent of Police (SSP) Fortunatus Musilimu explained that on the day of the accident, he interrogated Chenge in front of his legal team. He said Chenge told him that it was the Bajaj rider who veered from his lane on the left to him causing the accident.

    "However, when the suspect presented his insurance documents some discrepancies were found. The documents showed that the motor vehicle involved in the accident was different from the one registered in the document," said SSP Musilimu. "The motor vehicle involved in the accident had Registration Number T512 ACE whereas the one reflected in the document was registered as T 512 AEC," testified the witness. SSP Musilimu noted that the fact that the motor vehicle involved in the accident was not insured is in itself an offence. Chenge, also served as Attorney General in the Third Phase Government.

    The witness also told the court that after the discrepancies were discovered, the accused claimed that it was his wife's company that issued the insurance cover. "But when I checked with the National Insurance Corporation, they said that they had never insured such a vehicle," said SSP Musilimu. He also alleged that Chenge was driving 'too fast' on the day of the accident. "Chenge told me that he was travelling at between 80 and 100 km per hour, whereas the permitted speed on that road is 30 km per hour," said Musilimu.

    Chenge's lawyer, Mr Simon Mbona, had no objection. Principal Resident Magistrate Kwey Rusemwa adjourned the case to June 18. It is alleged that on March 27, last year, along Haile Selassie Road in Dar es Salaam, Chenge failed to take proper safety precautions and knocked a Bajaj (three-wheel motorbike) with Registration Number T 736 AXC, causing the deaths of two women - Victoria George and Beatrice Constantine. On the fateful day, Chenge, who was driving a Toyota Hillux Double Cabin with Registration Number T 512 ACE, allegedly drove recklessly and caused the accident.

    He is further accused of causing damage to the Bajaj and driving a motor vehicle without insurance cover on a public road. Chenge, who also served as Minister for the East African Co-operation, is currently a Member of Parliament for Bariadi West.
    Hii kesi bado tu haiiishi? Ndiyo mambo ya serikali ya JK hayo .... ... ..

+ Reply to Thread

Thread Information

Users Browsing this Thread

There are currently 1 users browsing this thread. (0 members and 1 guests)

     

Similar Threads

  1. Chenge's trial
    By Dua in forum Mahakamani
    Replies: 2
    Last Post: 02-13-2010, 10:10 PM
  2. Chenge kizimbani
    By mwanakijiji in forum Mahakamani
    Replies: 0
    Last Post: 03-30-2009, 03:58 PM
  3. Zombe aachiwe- Wakili
    By Mpita Njia in forum Mahakamani
    Replies: 2
    Last Post: 02-05-2009, 09:10 AM
  4. Kesi ya Uraia wa Obama
    By mwanakijiji in forum Ushahidi, Vielelezo & Report
    Replies: 1
    Last Post: 12-13-2008, 08:17 AM
  5. Mashahidi kesi ya EPA watajwa
    By mwanakijiji in forum Mahakamani
    Replies: 0
    Last Post: 11-21-2008, 05:08 PM

Bookmarks

Posting Permissions

  • You may not post new threads
  • You may not post replies
  • You may not post attachments
  • You may not edit your posts